Baadhi ya matukio ya ulimbukeni wa madaraka

Baadhi ya matukio ya ulimbukeni wa madaraka

Ushimen

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2012
Posts
42,554
Reaction score
105,336
Jerry Muro aliwahi kumfokea Mkurugenzi wake Dr.Charless Machera hadharani kama mtoto. Pengine Jerry alijiona mkubwa (kwa cheo) kuliko DED na hivyo akaamua kumdhalilisha, kumbananga, na kumkejeli hadharani. Tena mbele ya RC wake Mrisho Gambo ambaye ni boss wake.

Leo Dr.Machera ameamka akiwa Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi. A far step ahead of Jerry. Hii inatufanya tujifunze kuwa madaraka ni kama kiti cha basi. Leo umekalia, kesho amekaa mwingine.

Wakati Kassim Majaliwa Naibu Waziri TAMISEMI alikua anaripoti kwa Kepteni George Mkuchika. Leo mzee Mkuchika ndiye anayeripoti kwa Majaliwa.

Maisha ni mzunguko. Ukifanikiwa leo, usijae kiburi ukadhani ndio mwisho wa safari. Al-Bashir alikua na madaraka makubwa na pesa nyingi. Lakini leo ni mfungwa. Anakula, kulala na kuamka kwa amri. Hana tena hiyari ya maisha yake.

Wana wa Israel walipowekwa mateka kule Babeli, Esta na mjomba wake Mordekai walikua watumwa. Esta akachukuliwa na Hegai kuwa kijakazi kwenye nyumba ya Mfalme.

Hegai alikua kama 'Afisa Utumishi' kwenye kasri la mfalme Ahasuero. Vijakazi wote wa mfalme waliripoti kwake akiwemo Esta. Lakini baadae Esta akawa Malkia, na Hegai akawa anaripoti kwa Esta. Life is circle.

Hakuna aliyejua kiongozi mwenye ulinzi mkubwa na fedha nyingi kama Gadafi siku moja angeweza kujificha kwenye mtaro wa maji taka kama mwizi wa kuku au kibaka wa Kariakoo.

Usijivune kwa kufanikiwa leo, na usivunjike moyo kwa kufeli leo. Maisha ni safari yenye milima na mabonde. Ishi vizuri na kila mtu. Winston Churchill aliwahi kusema Success is not final, failure is not fatal; it is the courage to continue that counts

 
Lakini ukifuatilia majibu ya DED kwa muro, utaona kabisa, ni MTU wa aina gani. Mwoga, mchumia tumbo na ni MTU wa kujipendekeza. Though, ujumbe umefika
 
Kwenye hii mada yako naomba nichangie japo nitatoa mfano ambao unaweza kuwa hauakisi sana mada yako.
Ilikuwa miaka hiyooo, Jimbo Katoliki la Moshi lilikuwa wazi kwenye nafasi ya Askofu. Basi bwana siku hiyo akapita padre hapo kwenye ofisi za jimbo, padre ambaye alitokea parokia za vijijini. Padre yule alikuwa ameishiwa mafuta ya gari hivyo alipita pale jimboni kuomba mafuta. Wali m "nyasa nyasa" tena kwa kuona ni padre wa parokia za bush. Yule padre akaondoka zake.

Kesho yake, Lahaulaaaaaaa. Taarifa ikatoka Vatican, "Baba Mtakatifu amemteua Padre Msarikie kuwa Askofu wa Jimbo la Moshi". Huyo Msarikie ndie padre aliyekuwa ametoka kunyimwa mafuta ya gari lake pale jimboni jana yake.....

Uwiiiii, aibu iliyoje kwa wale waliokuwa wamemfanyia mtima nyongo.

RIP Mhashamu Askofu Msarikie.
 
Lakini ukifuatilia majibu ya DED kwa muro, utaona kabisa, ni MTU wa aina gani. Mwoga, mchumia tumbo na ni MTU wa kujipendekeza. Though, ujumbe umefika
Pengine yawezekana nikawa nina makengeza, lakini binafsi nimwona DED alimpa DC na RC majibu kwa kujiamini kabisa, na wala sikuona akitetemeka kama tunavyo onaga kwa wengine ambao huwa wanashindwa hata kuongea kwa sauti
 
Kwenye hii mada yako naomba nichangie japo nitatoa mfano ambao unaweza kuwa hauakisi sana mada yako.
Ilikuwa miaka hiyooo, Jimbo Katoliki la Moshi lilikuwa wazi kwenye nafasi ya Askofu. Basi bwana siku hiyo akapata padre hapo kwenye ofisi za jimbo, padre ambaye alitokea parokia za vijijini. Padre yule alikuwa ameishiwa mafuta ya gari hivyo alipita pale jimboni kuomba mafuta. Wali m "nyasa nyasa" tena kwa kuona ni padre wa parokia za bush. Yule padre akaondoka zake.

Kesho yake, Lahaulaaaaaaa. Taarifa ikatoka Vatican, "Baba Mtakatifu amemteua Padre Msarikie kuwa Askofu wa Jimbo la Moshi". Huyo Msarikie ndie padre aliyekuwa ametoka kunyimwa mafuta ya gari lake pale jimboni jana yake.....

Uwiiiii, aibu iliyoje kwa wale waliokuwa wamemfanyia mtima nyongo.

RIP Mhashamu Askofu Msarikie.
Huu ni moja ya mfano hai kabisa mkuu, mamlaka na vyeo ni vitu vya kupita na maranyingi huwa tunasema kwamba hivi ni vitu temporary tu hivyo tunapaswa sana kuwa makini zaidi pindi inapo tokea tunabahatika kupata madaraka/vyeo
 
Back
Top Bottom