Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 42,554
- 105,336
Jerry Muro aliwahi kumfokea Mkurugenzi wake Dr.Charless Machera hadharani kama mtoto. Pengine Jerry alijiona mkubwa (kwa cheo) kuliko DED na hivyo akaamua kumdhalilisha, kumbananga, na kumkejeli hadharani. Tena mbele ya RC wake Mrisho Gambo ambaye ni boss wake.
Leo Dr.Machera ameamka akiwa Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi. A far step ahead of Jerry. Hii inatufanya tujifunze kuwa madaraka ni kama kiti cha basi. Leo umekalia, kesho amekaa mwingine.
Wakati Kassim Majaliwa Naibu Waziri TAMISEMI alikua anaripoti kwa Kepteni George Mkuchika. Leo mzee Mkuchika ndiye anayeripoti kwa Majaliwa.
Maisha ni mzunguko. Ukifanikiwa leo, usijae kiburi ukadhani ndio mwisho wa safari. Al-Bashir alikua na madaraka makubwa na pesa nyingi. Lakini leo ni mfungwa. Anakula, kulala na kuamka kwa amri. Hana tena hiyari ya maisha yake.
Wana wa Israel walipowekwa mateka kule Babeli, Esta na mjomba wake Mordekai walikua watumwa. Esta akachukuliwa na Hegai kuwa kijakazi kwenye nyumba ya Mfalme.
Hegai alikua kama 'Afisa Utumishi' kwenye kasri la mfalme Ahasuero. Vijakazi wote wa mfalme waliripoti kwake akiwemo Esta. Lakini baadae Esta akawa Malkia, na Hegai akawa anaripoti kwa Esta. Life is circle.
Hakuna aliyejua kiongozi mwenye ulinzi mkubwa na fedha nyingi kama Gadafi siku moja angeweza kujificha kwenye mtaro wa maji taka kama mwizi wa kuku au kibaka wa Kariakoo.
Usijivune kwa kufanikiwa leo, na usivunjike moyo kwa kufeli leo. Maisha ni safari yenye milima na mabonde. Ishi vizuri na kila mtu. Winston Churchill aliwahi kusema Success is not final, failure is not fatal; it is the courage to continue that counts
Leo Dr.Machera ameamka akiwa Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi. A far step ahead of Jerry. Hii inatufanya tujifunze kuwa madaraka ni kama kiti cha basi. Leo umekalia, kesho amekaa mwingine.
Wakati Kassim Majaliwa Naibu Waziri TAMISEMI alikua anaripoti kwa Kepteni George Mkuchika. Leo mzee Mkuchika ndiye anayeripoti kwa Majaliwa.
Maisha ni mzunguko. Ukifanikiwa leo, usijae kiburi ukadhani ndio mwisho wa safari. Al-Bashir alikua na madaraka makubwa na pesa nyingi. Lakini leo ni mfungwa. Anakula, kulala na kuamka kwa amri. Hana tena hiyari ya maisha yake.
Wana wa Israel walipowekwa mateka kule Babeli, Esta na mjomba wake Mordekai walikua watumwa. Esta akachukuliwa na Hegai kuwa kijakazi kwenye nyumba ya Mfalme.
Hegai alikua kama 'Afisa Utumishi' kwenye kasri la mfalme Ahasuero. Vijakazi wote wa mfalme waliripoti kwake akiwemo Esta. Lakini baadae Esta akawa Malkia, na Hegai akawa anaripoti kwa Esta. Life is circle.
Hakuna aliyejua kiongozi mwenye ulinzi mkubwa na fedha nyingi kama Gadafi siku moja angeweza kujificha kwenye mtaro wa maji taka kama mwizi wa kuku au kibaka wa Kariakoo.
Usijivune kwa kufanikiwa leo, na usivunjike moyo kwa kufeli leo. Maisha ni safari yenye milima na mabonde. Ishi vizuri na kila mtu. Winston Churchill aliwahi kusema Success is not final, failure is not fatal; it is the courage to continue that counts
