Baada ya Venance kukosa goli la Ubingwa timu yake imeyumba hadi leo

Baada ya Venance kukosa goli la Ubingwa timu yake imeyumba hadi leo

The Burning Spear

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
8,551
Reaction score
20,346
GT.
Venance alikuwa ni namba sita machachari kweli kweli alikuwa tegemeo kubwa sana la timu yake . Kile kitendo cha kukosa goli la wazi akiwa yeye na golikeeper kimeigharimu timu yake hadi leo.

Namba kumi wao tegemeo alikula umeme hivyo Venance akashikilia dimba, wapinzani walizidisha mashambulizi na kujilinda, lakini katika hali isiyotarajiwa ilipigwa counter attack moja na Venance akajikuta yeye na golikeeper badala ya kufunga goli aliteleza na kuanguka.

Mashabiki walimlaumu sana venance na toka kipindi hicho timu yake imeyumba motisha umepotea kabisa kila mtu anajipigia tu haina tofauti na Manchester united, kila mchezaji mzuri anayesajiliwa ana underperform wamefanya hata rotation ya makocha lakini haijasaidia lolote.

Kilichobaki ni mwekezaji aliyepo kuachia timu apatikane tajiri mwingine huenda akaleta mapinduzi. Mashabiki hawataki kabisa hata kumsikia huyu mwekezaji aliyepo maana anaoneka ameridhika na hana msaada kwa timu.

Kinachomfanya huyu mwekezaji aliyepo azidi kung'ang'ania ni mapato ya timu, Maana pamoja na timu kufanya vibaya ila mapato bado yapo juu kwa sababu ilijijengea jina kubwa. Shinikizo kubwa la mashabiki pekee ndo linaweza kumfanya aachie timu la sivyo mashabiki wasubiri hadi Mkataba wake utakapoisha.
 
Humu Kuna kachumbali, nyama kidogo, Mchele wa kamsamba na tumawe twa Chunya.
 
Ni vigumu sana kwa vitoto vya afu 2 kukuelewa
 
Sasa ndugu mambo ya akina hadija kopa yamekujaje kwenye jukwaa la sports? halafu mtoto wa kiume haimpendezi kuimba taarab.
 
Hivi kuna sababu ya mtu kuumiza kichwa kama umesoma kitu, halafu hujakielewa!! cc Venance!
 
GT.
Venance alikuwa ni namba sita machachari kweli kweli alikuwa tegemeo kubwa sana la timu yake . Kile kitendo cha kukosa goli la wazi akiwa yeye na golikeeper kimeigharimu timu yake hadi leo.

Namba kumi wao tegemeo alikula umeme hivyo Venance akashikilia dimba, wapinzani walizidisha mashambulizi na kujilinda, lakini katika hali isiyotarajiwa ilipigwa counter attack moja na Venance akajikuta yeye na golikeeper badala ya kufunga goli aliteleza na kuanguka.

Mashabiki walimlaumu sana venance na toka kipindi hicho timu yake imeyumba motisha umepotea kabisa kila mtu anajipigia tu haina tofauti na Manchester united, kila mchezaji mzuri anayesajiliwa ana underperform wamefanya hata rotation ya makocha lakini haijasaidia lolote.

Kilichobaki ni mwekezaji aliyepo kuachia timu apatikane tajiri mwingine huenda akaleta mapinduzi. Mashabiki hawataki kabisa hata kumsikia huyu mwekezaji aliyepo maana anaoneka ameridhika na hana msaada kwa timu.

Kinachomfanya huyu mwekezaji aliyepo azidi kung'ang'ania ni mapato ya timu, Maana pamoja na timu kufanya vibaya ila mapato bado yapo juu kwa sababu ilijijengea jina kubwa. Shinikizo kubwa la mashabiki pekee ndo linaweza kumfanya aachie timu la sivyo mashabiki wasubiri hadi Mkataba wake utakapoisha.
Venance hakika alituangusha sana! Sasa ona tunavyoburuzwa kama mazoba! Lakini nasikia za chini chini kama timu ya Venance haitaki tena hata kumsikiliza imetoa masharti magumu ya usajili huenda ikajikomboa!
 
Venance hakika alituangusha sana! Sasa ona tunavyoburuzwa kama mazoba! Lakini nasikia za chini chini kama timu ya Venance haitaki tena hata kumsikiliza imetoa masharti magumu ya usajili huenda ikajikomboa!
Ngoja tusubiri
 
Kwa jinsi Pushgang mlivopokwa power, majuto hayana mwisho.
 
Ingekuwa Club za Colombia Venance tusingekuwa nae! Huyu namba kumi mpya hawezi kupiga hata danadana mbili lakini ndio kapteni kwenye timu yake ya Taifa na anakaribia kuipa kombe la Afcon!
 
Back
Top Bottom