Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Wandugu,
Maandamano ni njia mojawapo ya kuonyesha kutokuridhika na mambo fulani. Kwa muda sasa CDM imeweza kufanya maandamano makubwa kwenye mikoa kanda ya ziwa.
Ni suala la msingi kuangalia mafanikio ya maandamano hayo na kujadili nini kifuate baada ya maandamano hayo. Haya ni mambo ya muhimu kufanyika. Ni jukumu letu wote kuangalia nini cha kufanya ili kuweza kuleta mabadiliko.
Serikali inakosea pale ambapo badala ya kujifunza na kutekeleza majukumu yake baada ya wananchi kuonyesha kutokuridhishwa kwao yenyewe inalalamika na kulaumu CHADEMA kwamba wana nia ya kuvunja amani.
Ni jukumu la serikali kutathmini wananchi wanapinga nini na hatua gani zichukuliwe. Endapo hilo litashindikana miaka mitano itakuwa migumu sana kwa upande wa serikali na haitakuwa sahihi kusema kwamba CDM wanachochea nchi isitawalike. Matatizo ya wananchi ndio yatasababisha nchi isitawalike, sio CDM.
CDM wanachofanya ni 'kusema' matatizo ya wananchi. Wananchi wanachofanya ni 'kusikiliza' matatizo wanayoyaishi kila kukicha. Watanzania wengi wanaowatetea hawana afya, elimu, ajira, nyumba bora za kuishi nakadhalika. CDM wanatoa tu ujumbe, wananchi wanaishi hayo matatizo.
Swali linabaki, nini kifanyike (wananchi na CHADEMA) baada ya maandamano? Toa mawazo yako na mapendekezo kwa faida ya taifa lako na chama chako.
Nawasilisha.
Maandamano ni njia mojawapo ya kuonyesha kutokuridhika na mambo fulani. Kwa muda sasa CDM imeweza kufanya maandamano makubwa kwenye mikoa kanda ya ziwa.
Ni suala la msingi kuangalia mafanikio ya maandamano hayo na kujadili nini kifuate baada ya maandamano hayo. Haya ni mambo ya muhimu kufanyika. Ni jukumu letu wote kuangalia nini cha kufanya ili kuweza kuleta mabadiliko.
Serikali inakosea pale ambapo badala ya kujifunza na kutekeleza majukumu yake baada ya wananchi kuonyesha kutokuridhishwa kwao yenyewe inalalamika na kulaumu CHADEMA kwamba wana nia ya kuvunja amani.
Ni jukumu la serikali kutathmini wananchi wanapinga nini na hatua gani zichukuliwe. Endapo hilo litashindikana miaka mitano itakuwa migumu sana kwa upande wa serikali na haitakuwa sahihi kusema kwamba CDM wanachochea nchi isitawalike. Matatizo ya wananchi ndio yatasababisha nchi isitawalike, sio CDM.
CDM wanachofanya ni 'kusema' matatizo ya wananchi. Wananchi wanachofanya ni 'kusikiliza' matatizo wanayoyaishi kila kukicha. Watanzania wengi wanaowatetea hawana afya, elimu, ajira, nyumba bora za kuishi nakadhalika. CDM wanatoa tu ujumbe, wananchi wanaishi hayo matatizo.
Swali linabaki, nini kifanyike (wananchi na CHADEMA) baada ya maandamano? Toa mawazo yako na mapendekezo kwa faida ya taifa lako na chama chako.
Nawasilisha.