Mtukudzi
Senior Member
- Nov 14, 2013
- 103
- 408
Tanzania ni nchi tajiri sana. Serikali ya awamu ya tano imetukumbusha kuwa tuna vyanzo vingi vya mapato vinavyoweza kuleta makusanyo mengi ya kodi kupitia serikali kuu, mashirika ya umma na Mamlaka za serikali za Mitaa.
Baada ya kugundua chanzo kipya ambacho ni leseni za kurusha ndege zisizo na na rubani(drones) naomba igeukie upande wa hizi CCTV camera. Leseni hizi pamoja na kuingiza kipato kwa serikali zitazuia matumizi holela ya Camera hizi. Camera hizi zimekuwa zikileta mtafaruku kwenye jamii na kwa ajili hiyo zinatakiwa kudhibitiwa.
Mara kadhaa Mh. Mkuu wa Wilaya ya Hai Bw. Sabaya amejikuta kwenye matata kwa sababu ya CCTV hizi. Tunajua kuwa teknolojia imekuwa kubwa na inawezekana mara zote serikali imefanya uchunguzi kubaini kuwa Bw. Sabaya amekuwa anaandamwa kwa sababu za kisiasa.
Kuonyesha matukio ya kuhusishwa na uingiaji wa nguvu kwenye mahoteli ya wawekezaji na kwenye studio za TV usiku wa manane siyo vizuri yakaachwa. Watakaopewa leseni wapewe na miiko ya matumizi yanayofaa ya picha zinazokutwa kwenye hizi Camera.
Baada ya kugundua chanzo kipya ambacho ni leseni za kurusha ndege zisizo na na rubani(drones) naomba igeukie upande wa hizi CCTV camera. Leseni hizi pamoja na kuingiza kipato kwa serikali zitazuia matumizi holela ya Camera hizi. Camera hizi zimekuwa zikileta mtafaruku kwenye jamii na kwa ajili hiyo zinatakiwa kudhibitiwa.
Mara kadhaa Mh. Mkuu wa Wilaya ya Hai Bw. Sabaya amejikuta kwenye matata kwa sababu ya CCTV hizi. Tunajua kuwa teknolojia imekuwa kubwa na inawezekana mara zote serikali imefanya uchunguzi kubaini kuwa Bw. Sabaya amekuwa anaandamwa kwa sababu za kisiasa.
Kuonyesha matukio ya kuhusishwa na uingiaji wa nguvu kwenye mahoteli ya wawekezaji na kwenye studio za TV usiku wa manane siyo vizuri yakaachwa. Watakaopewa leseni wapewe na miiko ya matumizi yanayofaa ya picha zinazokutwa kwenye hizi Camera.