Watanzania bhana eti wazungu wenyewe wanaachana. Kwa hiyo kama wanaachana? Kwani wazungu ndio waanzilishi wa ndoa???
Daaah hawa wanawake bana, wakiwa na akili shida wakiwa vilaza shida
Kwanza inaonekana wewe alichofanya mwanamke mwenzio unaunga mkono`pili kama wewe uko kwenye ndoa ni kwa sababu huna kipato siku ukipata kipato jamaa utamkimbia au utamwambia muachane`......inawezekana huyo dada alikuwa anavumilia ndoa isiyokuwa na amani sababu hana kipato.
Sasa ana kipato chake na ataweza kujihudumia mwenyewe na mtoto wake, sasa ndoa ndoano ya nini tena? Tusilaumu tu kakimbia mume, kumbe kakimbia matizo ya ndoa.
wajanja wa raskazoni washamuwahi.....
Mwanamke mjinga hubomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe
Kwanza wanaume tukome kabisa kusomesha wanawake kama hajasoma kutoka kwao bora akae hivohivo maana mmezidi mnakwapua haf mbio......inawezekana huyo dada alikuwa anavumilia ndoa isiyokuwa na amani sababu hana kipato.
Sasa ana kipato chake na ataweza kujihudumia mwenyewe na mtoto wake, sasa ndoa ndoano ya nini tena? Tusilaumu tu kakimbia mume, kumbe kakimbia matizo ya ndoa.
Hii imemtokea mwenzetu hapa ofisini kwetu na tunae jamaa alifunga Ndoa na mkewe miaka mitano iliyopita na wakabahatika kupata mtoto wa kiume ambae walikua wanamsomesha Shule fulani ya watakatifu pale Kibaha.
Kwa kuwa mke wa jamaa alikua pass mark zake si nzuri jamaa akajipinda wife akarisiti na kufanikiwa kupata divisheni ya vijana ndipo jamaa akaamua kumpeleka chuo fulani baada ya kumaliza mke wa jamaa akapangiwa ajira mkoa uleee yalikozaliwa mapenzi na mitaa yake mingi inafahamika kwa Barabara ya kwanza hadi 22 kwa sasa.
Jamaa walivyokubaliana na mkewe kwamba afanye mishemishe ya kumrejesha hapa Dar na mipango yote tayari ili wife arudi kupiga kazi Dar es salaam cha ajabu mke kamhamisha mtoto shule anayosoma na kaenda nae huko TA na kwmwambia jamaa wewe na mimi basi oa mke mwingine na usinijue kuanzia leo na huna mtoto ma mimi.
Walifunga ndoa ya kanisani ambayo baadhi ya watu kwa ujinga wanafikiri hawaachani wakati wazungu wenyewe wanaachana taarifa hizo kaletewa Mwaka huu 2015
Tumeshauri jamaa yetu tulia jenga maisha na utapata mke mwingine walausimfuatilie uila tunza meseji zote alizokutumia.
Hayo ndo mambo ya wanawake wa sasa maisha sasa kila mtu anamlia timing mwenzie ukizubaa imekula upande wako wewe mwanamume mwenzangu.Kina dada hawa ambao ni wake zetu acha kabisa kuwaaamini`kama mke ndo amefanya hivyo nani mwingine umuamini`aliesema mke si nduguyo ni kweli kabisa.