Baada ya kupata ajira amkimbia mumewe

Baada ya kupata ajira amkimbia mumewe

shikamoooooooooooo! ndoa[/QUOTE]
....Marhabaaa hujambo toto njuri?!..............
 
Tatizo la ndoa ni kwamba mnakutana watu wawili tofauti, mliokulia mazingira tofauti, lifestyle tofauti, ideologies tofauti etc. kwahyo usitegemee mtakuwa sawa hata kidogo. Ni lazima kila mmoja aamue ku-give up something he/she used to do, just for the sake of love. Mmoja anapojifanya yupo RIGHT kuliko mwenzake, hapo ndipo matatizo hutokea. Ila kiukweli, tho I'm married, I must admit that maisha ya ndoa ni magumu sana.


Sent from my iPad using JamiiForums app
 
Kuchepuka ni ishu mojawapo ya kupelekea kuachana. But ikumbukwe pia kuchepuka kunasababishwa na vingi sana, too many to mention.


Sent from my iPad using JamiiForums app
 
Kama wewe ni mnywaji pombe, ikitokea ukaoa mwanamke ambaye maisha yake yote na kutokana na mafundisho ya nyumbani kwao pamoja na watu wanaomzunguka mara nyingi, akaamini siku zote kwamba pombe ni dhambi. Na bahati mbaya sana kipindi chote cha uchumba wenu hakuwahi kukuonesha kwamba anachukia pombe ila si kwa kiasi hicho cha kudhani ni dhambi sn, yan alikuw anachukulia poa tu. Basi mtu huyo ukimuoa, lazima mtazinguana tuuu. Zile terms hazikuwekwa mapema, so mtu ukawa unachukulia fresh tu. ni balaa.


Sent from my iPad using JamiiForums app
 
Huyu msichana kenge sana, hapa ndo anapo haribu nafasi ya wanawake wachache wanaojua mahusiano na thamani ya ndoa.
Inaonyesha binti hakumpenda mshikaji tangu mwanzo, ila alipenda zake.

Mwambie mshkaji afatilie damu yake.

Mkuu kama kamwambia wasijuane isije ikawa na mtoto alibambikiwa sio wake.
 
Usijekuta hata mtoto mwenyewe jamaa alipewa(sio wake)
 
TANGA stand UP.!! asee kule bwana kama una akili za kushikiwa utasahau kila kitu.. kapata mwinyi wa Tanga kapelekwa forodhani.. deep sea kwenye samaki wa ukweli.. kanyweshwa juisi ya nazi, kapelekwa br ya 5 chips maini,, kazungushwa mji mzima hadi kamsahau mumewe.. huyo ndo kashazama huko kuibuka ni vigumu... Tanga Raha waja leo wakaa milele..lol
 
ndoa ndoanoooooo. lakini pia inawezekana bidada kuna vitu ambavyo havikumpendeza kwa mumewe ndio maana akaona bora akasome ili ajishie mwenyewe. wakati mwingine kumsomesha mtu sio sababu ya kumlaumu sanaaa au kuona ndio amekosea sana, yeye ashukuru anakazi hivo mwanae atakuwa na uhakiki wa matunzo. mengine wanajua wenyewe, sababu hizo wanazosema ni zile zinazoelezeka ila kiini huwa hata mchungaji aliyefungisha ndoa haambiwi.

Mwanae? atkuaa matunzo jamaa hana kitu hapo kumbuka kasema:
by Bonge the one said:
Cha ajabu mke kamhamisha mtoto shule anayosoma na kaenda nae hukooooo TA na kwmwambia jamaa wewe na mimi basi oa mke mwingine na usinijue kuanzia leo na huna mtoto ma mimi6¦1
 
TANGA stand UP.!! asee kule bwana kama una akili za kushikiwa utasahau kila kitu.. kapata mwinyi wa Tanga kapelekwa forodhani.. deep sea kwenye samaki wa ukweli.. kanyweshwa juisi ya nazi, kapelekwa br ya 5 chips maini,, kazungushwa mji mzima hadi kamsahau mumewe.. huyo ndo kashazama huko kuibuka ni vigumu... Tanga Raha waja leo wakaa milele..lol

Tunachojua n kumkaribisha mgeni kumwambia kwa her hatujui
 
Tunachojua n kumkaribisha mgeni kumwambia kwa her hatujui

haswaaa... katika miaka yote niliyoishi tanga sijawahi kuona wala kusikia mtu anataka kuhama tanga kirahisi rahisi tu..mwenyewe imebidi tu ila roho inaniuma kuondoka huko... nitarudi huko kuoa
 
Tatizo la ndoa ni kwamba mnakutana watu wawili tofauti, mliokulia mazingira tofauti, lifestyle tofauti, ideologies tofauti etc. kwahyo usitegemee mtakuwa sawa hata kidogo. Ni lazima kila mmoja aamue ku-give up something he/she used to do, just for the sake of love. Mmoja anapojifanya yupo RIGHT kuliko mwenzake, hapo ndipo matatizo hutokea. Ila kiukweli, tho I'm married, I must admit that maisha ya ndoa ni magumu sana.


Sent from my iPad using JamiiForums app

Daniel mwinula said:
Kuchepuka ni ishu mojawapo ya kupelekea kuachana. But ikumbukwe pia kuchepuka kunasababishwa na vingi sana, too many to mention.

Apologise lady said:
kwa kwel tuache utani, katika mitihani yote, mtihani jaman mtihani wa ndoa ni kiboko, ukiufaulu utaiona dunia yako, ila ukiufeli utaona dunia inakuangukia.
mim habari ya mateso ndio sitaki kuisika, habari mume badala ya kuwa rafiki anageuka baba, amri kwa kwenda mbele, hapana, tene hapana

Ndoa ndoa ndoa unatufanya nin ndoa mmenena kwa hisia sana ambayo imenifanya nitafakari kwa kina sana sioi leo kwel wala kesho labda mtondogoo
 
haswaaa... katika miaka yote niliyoishi tanga sijawahi kuona wala kusikia mtu anataka kuhama tanga kirahisi rahisi tu..mwenyewe imebidi tu ila roho inaniuma kuondoka huko... nitarudi huko kuoa

Karib sana
 
Ndoa ya Kanisani inaweza kuvunjwa? Je atawezaje kuoa mke mwingine?
Huyu msichana kenge sana, hapa ndo anapo haribu nafasi ya wanawake wachache wanaojua mahusiano na thamani ya ndoa.
Inaonyesha binti hakumpenda mshikaji tangu mwanzo, ila alipenda zake.

Mwambie mshkaji afatilie damu yake.[/QUOTE]

Je akafuatilia hiyo damu na akagundua siyo yake atafanyaje?

Ushauri wangu ni huu, atulie kabisa,acha kupiga simu wala kuandika meseji,wala kulia lia,songa mbela, kama mtoto ni wake atarudi tu siku ikifika, unaweza fuatilia mtoto na ukaambiwa maneno magumu sana na huyo mdada. La mwisho, Mungu yupo, ili akutendee mema, basi usitendee dhambi. Shukuru kwa kuwa ametendewa akiwa na nguvu na akili. Mbona utapata mdada mwingine mzuri wa tabia kuliko huyo.
 
Tusiwe wepesi wa kuhukumu,huwezi kujua nini lililowatokea hawa ndugu.Mimi nilikutana na mke wangu mara baada ya yeye kumaliza kidato cha nne lakini hakuendelezwa kwa kuwa,wazazi wake walitengana hivyo familia nayo ikayumba.Nikamsomesha kidato cha tano na sita na baadae chuo cha uandishi wa habari.Dada yangu alimsaidia kupata kazi kwenye kituo kimoja cha televishen mpaka sasa anafanya kazi hapo.Tumekuwa tunaishi kwa mapenzi makubwa bila ya kudharauliana.Kwa hiyo kwa hao ndugu lazima kuna jambo tu siyo bure wawe wa wazi ili tuwasaidie.Huenda jamaa alikuwa na dharau na gubu kwa kuwa kamsomesha au dada baada ya kupata elimu naye akaanza dharau,yote yanawezekana.
 
Tatizo la ndoa ni kwamba mnakutana watu wawili tofauti, mliokulia mazingira tofauti, lifestyle tofauti, ideologies tofauti etc. kwahyo usitegemee mtakuwa sawa hata kidogo. Ni lazima kila mmoja aamue ku-give up something he/she used to do, just for the sake of love. Mmoja anapojifanya yupo RIGHT kuliko mwenzake, hapo ndipo matatizo hutokea. Ila kiukweli, tho I'm married, I must admit that maisha ya ndoa ni magumu sana.


Sent from my iPad using JamiiForums app

Mkuu nimeipenda hii!! Ndoa si mchezo hata kidogo, ila kwa msaada wa Mungu tutafika.
 
ghwe mwana ugwe, umundu mkusi une![/QUOTE]
......ukanginda une nlifyinja fingi fijo,...nkomene ku ww1 une...
 
Back
Top Bottom