Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Ni masaa 60 yamepita toka hotuba ya Mh. Rais iishe pale Diamond Jubilee. Katika hotuba ile aliyoifanya mbele ya 'vikongwe' vya DSM (which to me is a wrong audience cosidering his theme) ilijaa mipasho mingi ya kimwambao.
Binafsi sikuweza kutofautisha 'mipasho' ya pale Lango la Jiji Bar au hotuba za Katibu Mkuu wa CCM Bw. Yusufu Makamba au hata mwanapropaganda Tambwe Hiza. Nili bahatika kuirekodi hotuba yote na kupata nafasi ya ku replay zaidi ya mara tano ili mradi nipate uhakika kama kweli niliyekuwa namsikia na kumtazama ni mkuu wa nchi? Ni yule yule anayetajwa kwenye katiba ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania? Ni yule yule aliyeshinda kwa kishindo (82%) mwaka 2005? Ni yule yule aliyetajwa kama "....Tumaini lililorejea"? Je ni yule yule aliyeahidi kuleta Maisha Bora kwa kila Mtanzania?
Jibu nikapata kuwa ndiye haswaaaaaaa!!
Mengi yamesemwa kuhusu hotuba ile, sitaki niyarejee hapa. Ingawa kuna mitizamo tofauti juu ya hotuba ile, yangu ni haya;
1. Amesema kuwalipa wafanyakazi kima cha chini cha Tsh. 315,000 ni kuwadhulumu majority ya watanzania, je anajua kiasi gani anacholipwa yeye kama mshahara na marupurupu mengine ya mikutano, safari na n.k. Je haoni kama na yeye anawadhulumu Watanzania?
2. Je ni kiasi gani kinalipwa kwa wabunge na mawaziri? Kwa maoni yake kinalingana na pato la taifa?
3. Vipi kuhusu gharama za magari ya kifahari yanayonunuliwa na serikali? Je yanalingana na pato la taifa?
4. Nini mantiki ya kutoa misamaha ya kodi kwa wawekezaji isiyo na lazima wala tija? Huko ni kuwatendea haki majority ya watanzania?
5. Je Mh. Rais anajua gharama ya maisha kwa sasa? Au kwa vile yeye kila kitu analipiwa? Namkaribisha aje aishi na sisi hapa Tandale kwa Mtogole kwa siku moja tu......naamini hatorudia kuongea yale aliyozungumza pale Diamond.
6. Je yale mahesabu ya Tirioni saba kwa mwaka aliyapiga vipi? Mbona sie tunapa TZS. 1.8 tilioni au alijumlisha na mshahara wa rais, mawaziri, wabunge?
MKAKATI WANGU
Kwa kuwa nimekuwa nikilitumikia Taifa langu katika utumishi wangu wa umma kwa unyenyekevu na uadilifu mkubwa, huku nikijituma pasipo kudai wala kutegemea chochote bali mshahara wangu tu wa Tzs. 163,000 huku nikihangaika huku na kule kulipa pango la nyumba, ada za shule kwa watoto wangu watatu wanaosoma sekondari, chakula, gharama za matibabu, mavazi na matumizi mengine ya msingi.
Nimegundua nchi hii kwa sasa unatakiwa kujali tumbo lako na si utumishi uliotukuka (public service), kwa sasa naahidi kula mezani kwangu kwa kila khali.
Regards,
Mlala hoi
Tandale kwa Mtogole
Binafsi sikuweza kutofautisha 'mipasho' ya pale Lango la Jiji Bar au hotuba za Katibu Mkuu wa CCM Bw. Yusufu Makamba au hata mwanapropaganda Tambwe Hiza. Nili bahatika kuirekodi hotuba yote na kupata nafasi ya ku replay zaidi ya mara tano ili mradi nipate uhakika kama kweli niliyekuwa namsikia na kumtazama ni mkuu wa nchi? Ni yule yule anayetajwa kwenye katiba ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania? Ni yule yule aliyeshinda kwa kishindo (82%) mwaka 2005? Ni yule yule aliyetajwa kama "....Tumaini lililorejea"? Je ni yule yule aliyeahidi kuleta Maisha Bora kwa kila Mtanzania?
Jibu nikapata kuwa ndiye haswaaaaaaa!!
Mengi yamesemwa kuhusu hotuba ile, sitaki niyarejee hapa. Ingawa kuna mitizamo tofauti juu ya hotuba ile, yangu ni haya;
1. Amesema kuwalipa wafanyakazi kima cha chini cha Tsh. 315,000 ni kuwadhulumu majority ya watanzania, je anajua kiasi gani anacholipwa yeye kama mshahara na marupurupu mengine ya mikutano, safari na n.k. Je haoni kama na yeye anawadhulumu Watanzania?
2. Je ni kiasi gani kinalipwa kwa wabunge na mawaziri? Kwa maoni yake kinalingana na pato la taifa?
3. Vipi kuhusu gharama za magari ya kifahari yanayonunuliwa na serikali? Je yanalingana na pato la taifa?
4. Nini mantiki ya kutoa misamaha ya kodi kwa wawekezaji isiyo na lazima wala tija? Huko ni kuwatendea haki majority ya watanzania?
5. Je Mh. Rais anajua gharama ya maisha kwa sasa? Au kwa vile yeye kila kitu analipiwa? Namkaribisha aje aishi na sisi hapa Tandale kwa Mtogole kwa siku moja tu......naamini hatorudia kuongea yale aliyozungumza pale Diamond.
6. Je yale mahesabu ya Tirioni saba kwa mwaka aliyapiga vipi? Mbona sie tunapa TZS. 1.8 tilioni au alijumlisha na mshahara wa rais, mawaziri, wabunge?
MKAKATI WANGU
Kwa kuwa nimekuwa nikilitumikia Taifa langu katika utumishi wangu wa umma kwa unyenyekevu na uadilifu mkubwa, huku nikijituma pasipo kudai wala kutegemea chochote bali mshahara wangu tu wa Tzs. 163,000 huku nikihangaika huku na kule kulipa pango la nyumba, ada za shule kwa watoto wangu watatu wanaosoma sekondari, chakula, gharama za matibabu, mavazi na matumizi mengine ya msingi.
Nimegundua nchi hii kwa sasa unatakiwa kujali tumbo lako na si utumishi uliotukuka (public service), kwa sasa naahidi kula mezani kwangu kwa kila khali.
Regards,
Mlala hoi
Tandale kwa Mtogole