Aziz Ki hatakuja kuuzwa Wydad AC

Aziz Ki hatakuja kuuzwa Wydad AC

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,470
Nafikiri hizi stori za Aziz Ki kuuzwa Wydad tuzizike rasmi na tuachane nazo.

Yanga haijawahi kutaka kumuachia Aziz Ki na kitendo cha aliyekuwa kocha wa Mamelodi, Rulani Mokwena kumsogeza na kuanza "kumnong'oneza" baada ya ile mechi ya robo fainali kati ya Mamelodi na Yanga ilichukuliwa kama ishara ya dharau kwa Yanga na ikawapa hasira, kiburi na kisingizio cha kuapa kwamba hawatakuja kumuuza kwa Mamelodi au popote pale Mokwena atakapokuwa.

Harakati za kumuozesha kwa Hamisa Mobetto zilikuwa zina nia hiyo hiyo ya kumnasa katika tundu bovu. Sasa hivi Aziz Ki anajinenepea tu, hana habari za Club World Cup wala nini.

Mokwena mwenyewe amekalia kuti kavu huko Wydad, muda wowote kibarua chake kinaota nyasi.

Ninachoona siyo tu Yanga wamekwepakwepa fursa za kumuachia Aziz Ki kwa Wydad, ila pia wametoa masharti magumu yasiyotekelezeka ili tu dili lijifie. Kiufupi wanataka wapigiwe magoti huku wakiwa na dhamira ya dhati ya kutomuuza.

Club World Cup inaanza mwezi June, Wydad hawawezi kumnunua mchezaji kwa pesa ndefu na kutekeleza masharti ya kiduwanzi wanayopewa na Yanga halafu wategemee kumuandaa kwa wiki mbili tu kabla ya mashindano makubwa kama ya CWC kuanza na wakati huo huo anayetaka kumleta wanataka kumtimua muda wowote.

Tufunge stori za Aziz Ki. Huyu tupo naye hapa hapa hadi kiama.
 
Kumbe unafuatilia habari za Yanga ila ndio ukweli wenyewe Mokoena anamtaka Ki na CRB.
Kwani nimewahi kusema sifuatilii habari za Yanga?

Na uzi tayari unasema Mokwena alishaonyesha kumtaka Aziz Ki toka baada ya mechi ya Mamelodi ila viongozi wa Yanga wakaapa hawatampa kisa dharau wanazodhani alizionyesha ingawa wote tunajua hiko ni kisingizio tu maana Yanga haina utamaduni wa kumuachia mchezaji kwa amani.
 
Kwani nimewahi kusema sifuatilii habari za Yanga?

Na uzi tayari unasema Mokwena alishaonyesha kumtaka Aziz Ki toka baada ya mechi ya Mamelodi ila viongozi wa Yanga wakaapa hawatampa kisa dharau wanazodhani alizionyesha ingawa wote tunajua hiko ni kisingizio tu maana Yanga haina utamaduni wa kumuachia mchezaji kwa amani.
Hamna timu inayo muuza mchezaji kisa tu anatakiwa? Kama ingekuwa hivyo Kibu mngemwachia au mmesahau mchezaji mpaka katoroka au Kibu sio mchezaji wenu.Meneja wake akadai kila offer ikiletwa mnaitia kapuni, mpaka watu wakaamua waingie kwenye DM ya mchezaji Instagram.
 
Hamna timu inayo muuza mchezaji kisa tu anatakiwa? Kama ingekuwa hivyo Kibu mngemwachia au mmesahau mchezaji mpaka katoroka au Kibu sio mchezaji wenu.Meneja wake akadai kila offer ikiletwa mnaitia kapuni, mpaka watu wakaamua waingie kwenye DM ya mchezaji Instagram.
Jikite kwenye mada. Hakuna anayeongelea habari za Kibu hapa. Usigeuze hii mada kuwa ya Usimba na Uyanga.
 
Jikite kwenye mada. Hakuna anayeongelea habari za Kibu hapa. Usigeuze hii mada kuwa ya Usimba na Uyanga.
Wewe si umesema Yanga haina utamaduni wa kuuza wachezaji?,mimi nikaonesha utamaduni wenu kwa Kibu au sio mchezaji wenu. Nijikite na mada mara ngapi Ki anatakiwa na timu mbili Wydad na CRB ,hata Kaizer walimtaka ila kwa sasa wameamua kuachana nae. Hapo kinacho subiriwa mwenye hela kubwa,ndiye anaye ondoka na mchezaji.
 
Azizi Ki kwa kipaji chake anahitaji kuandaliwa Nini?!! Kua Azizi Ki wiki 2 hazimtoshi kuingia kwenye timu?!! Ama magozi ya Moroco na Club World Cup yapo tofauti na ya kwetu hapa?!!
Maandishi ya mtu aliyekurupuka na asiyejua lolote kuhusu mambo ya mpira.
 
Wewe si umesema Yanga haina utamaduni wa kuuza wachezaji?,mimi nikaonesha utamaduni wenu kwa Kibu au sio mchezaji wenu. Nijikite na mada mara ngapi Ki anatakiwa na timu mbili Wydad na CRB ,hata Kaizer walimtaka ila kwa sasa wameamua kuachana nae. Hapo kinacho subiriwa mwenye hela kubwa,ndiye anaye ondoka na mchezaji.
Kwa hiyo kuonyesha utamaduni "wetu" kwa Kibu ndiyo kujikita kwenye mada?
 
Back
Top Bottom