Azam Tv mihemko itawapeleka shimoni

Azam Tv mihemko itawapeleka shimoni

Azam wanajua kuwa yale ni maigizo ndiyo maana hawakuipa kipaumbele.
Husiwapangie azam namna ya kufanya kazi na ninyivanzisheni uhuru tv muone kama ata mende wa kijani wataangalia
Siku nyingine husiandike upumbavu, mwambie babako aheshimu uhuru wa vyombo vya habari na pia sifa za kijinga hazifahi
Jana nilishtushwa kuona mnashindwa kujua uzito wa habari, kubalansi, kutawaliwa na mihemko zaidi ya kujua umuhimu wa vipaumbele kwa watu na nchi yetu.

Hakuna namna unaweza kunishawishi nikaelewa kwamba ni bora zaidi kuongelea "personality" tena kwa dakika5 kuliko kuongelea namna nchi yetu inavyoliwa na kuibiwa tukio lililokuwa likimhusisha raisi. Kwamba kukamatwa makontena 20 yenye kuhisiwa yanatoroshwa yakibeba dhahabu si habari nzito kwenu. Kwamba Nape ni habari nzito na muhimu kwenu kuliko mali na utajiri wa nchi yetu.

Lakini pia, hivi unaanza habari gani kwa siku, ya raisi ama ya aliyefukuzwa uwaziri? Tena mlivyo wa hajabu wakati mkitoa dakika 5 na kukaribisha wazungumzaji kwa tukio la mtu, upande wa pili mnatoa dakika1 halafu mnafukia as if anayeongea ni balozi wa nyumba kumi na kilichotokea ni kama mtu kutema mate.

Yawezekana hao wanaotuibia mali zetu waliwaambia msiwaoneshe sana ili wananchi wasipige kelele dhidi yao na badala yake muonesheni fulani ili wananchi wapige kelele dhidi ya utawala. Kama na nyie mlikubali hili na mkauvaa mkenge basi anzeni kujichunguza kabla, nchi yetu inaliwa na sote tunajua ila nyie hamuoni kama la kuliwa nchi yetu ni hoja. Mnatakiwa kuelewa hao wezi hawamuibii JPM tu, hawamwibii fulani tu, wanatuibia sisi sote na tunapopoteza wakati wenzenu wanapata ni kuihujumu nchi yetu. Ni kuhujumu serikali kwa kile inachojaribu kukifanya katika maendeleo, msivimbe vichwa mkajiona tayari.
 
Mkuu umetokwa na povu utadhan TV ya taifa Ile, hata wasingerusha kbs ni sawa
 
Tukio unalolitolea povu lilikuwa linamhusu raisi kumuondoa kazi waziri kwa ishu inayomhusu mkuu wa mkoa,unafikiri kuna habari gani kubwa zaidi ya hiyo? walitakiwa waipe dakika 10 hizo tano ni chache sana.
 
Leta cheti chao cha usajiri ili tuone majukumu yao ni yapi kwa Tz. Na hakuna anayewapangia as tunaamini sie tunawakumbusha tu yale yaliyo kwenye kibari chao cha kazi. Kama kibari uliwapa wewe pia tupe tuone ni nini jukumu lao wakiwa Tz.
Wewe inawrzekana hauna akili au zimepungua
Unapewa elimu bure bado unabisha.
 
Jana nilishtushwa kuona mnashindwa kujua uzito wa habari, kubalansi, kutawaliwa na mihemko zaidi ya kujua umuhimu wa vipaumbele kwa watu na nchi yetu.

Hakuna namna unaweza kunishawishi nikaelewa kwamba ni bora zaidi kuongelea "personality".

lamba ndimu mkuu kama imekuuma sana maana inaonekana unaskia na kichefu chefu
 
Wee jamaa umelazwa Wodi namba ngapi milembe nije kukuonaa...!!!???
 
Tulia dawa ikuingie......

Si ulisema kwa kejeli kwa wapiga kura wako kuwa wasikupangie la kufanya kwa kuwa Urais ni 'Mali' yako?

Sasa inakuwaje kwa wamiliki wa vyombo vya habari ambavyo ni Mali zao binafsi wewe uwapangie cha kuandika na kutoandika!?
hata mimi NashIndwa kushangaa kabisa..
 
Jana nilishtushwa kuona mnashindwa kujua uzito wa habari, kubalansi, kutawaliwa na mihemko zaidi ya kujua umuhimu wa vipaumbele kwa watu na nchi yetu.

Hakuna namna unaweza kunishawishi nikaelewa kwamba ni bora zaidi kuongelea "personality" tena kwa dakika5 kuliko kuongelea namna nchi yetu inavyoliwa na kuibiwa tukio lililokuwa likimhusisha raisi. Kwamba kukamatwa makontena 20 yenye kuhisiwa yanatoroshwa yakibeba dhahabu si habari nzito kwenu. Kwamba Nape ni habari nzito na muhimu kwenu kuliko mali na utajiri wa nchi yetu.

Lakini pia, hivi unaanza habari gani kwa siku, ya raisi ama ya aliyefukuzwa uwaziri? Tena mlivyo wa hajabu wakati mkitoa dakika 5 na kukaribisha wazungumzaji kwa tukio la mtu, upande wa pili mnatoa dakika1 halafu mnafukia as if anayeongea ni balozi wa nyumba kumi na kilichotokea ni kama mtu kutema mate.

Yawezekana hao wanaotuibia mali zetu waliwaambia msiwaoneshe sana ili wananchi wasipige kelele dhidi yao na badala yake muonesheni fulani ili wananchi wapige kelele dhidi ya utawala. Kama na nyie mlikubali hili na mkauvaa mkenge basi anzeni kujichunguza kabla, nchi yetu inaliwa na sote tunajua ila nyie hamuoni kama la kuliwa nchi yetu ni hoja. Mnatakiwa kuelewa hao wezi hawamuibii JPM tu, hawamwibii fulani tu, wanatuibia sisi sote na tunapopoteza wakati wenzenu wanapata ni kuihujumu nchi yetu. Ni kuhujumu serikali kwa kile inachojaribu kukifanya katika maendeleo, msivimbe vichwa mkajiona tayari.
Unapoandaa habari iwe kwenye televisheni au magazeti unapima watazamaji au wasomaji wako wanataka nini kwenye siku husika.
Watoto wa mjini wanasema catchy news!
Habari ya rais kufanya ziara za kustukiza siyo mpya wala catchy tena kwa wasomaji/watazamaji, kwa sababu hakuna jipya. Habari ya Nape ilikuwa ni hot news na wengi walitaka kujua nini kimemsibu.
Habari ni taaluma watu wameisomea na wanajua wanachofanya, acheni kuwapangia wafanyeje shughuli zao kama vile 'wengine' wasivyotaka wapangiwe!
 
Yani unazungumzia yale maigizo ya bandari?!!
Hahahaha lile lilikuwa ni movie la kihindi la kuondoa attention ya Nape kwa raia, lakini uzuri wana habari wameitendea haki taaluma yao maana huwezi kuonesha drama za kutunga ukaacha habari za maana kama za Nape
 
wewe nimpumbavu sana kwani tbc haitoshi kuonyesha maigizo yenu ya bandarini???


kila habari muwe nyie tu kwani nyie ndio kina nani
Una tatizo la malezi kutoka kwa wazazi wako
 
Rwenye uko sawa ila kumbuka mitandao yote imeshikwa na upinzani wasikusumbuebumesema vyema.
Wako wehu wachache humu ndo wanataka tuwaachie nchi liwe kama soko la ndizi
 
24ec39d622456e098dfbe655c31fdc6b.jpg


Ilitaka iandikwe habari ya gari ati imekutwa kwenye kontena????
Huyu Malisa anafikiri aliposoma akafikia ndo ukomo wa akili za binadamu wote, kichwa chake kinaonekana kikubwa lakini ni mzigo kwake
 
Pole sana kwa kutokwa na Povu kumbe mmeumia sana kuona drama imepotezewa na ishu ya nape imepewa uzito. Labda nikufundishe kwann vyombo vya habari sio tu azam vingi vilipotezea, ni hivi ishu ya bandarini japo ni public interest ishu ina uzito mdogo sana ukilinganisha na ishu ya nape ambayo ni HUMAN RIGHT ishu sasa huwezi kuacha kuipa coverage ishu inayovunja haki ya kibinadam ya uhuru wa kuongea ukaipa mashiko ishu ya wizi. Hahahaha wizi ni kitu kidogo sana hata km thamani ya hicho kilichoibiwa itakua matrilion. Lakin ishu ya mtu kunyimwa haki ya kikatiba ya uhuru wa kujieleza. Hivyo sikulaumu hata waliokutuma pia hawajui. Halafu umesema eti peraonality. Unatakiwa kujua haki ya kikatiba ikivunjwa kwa mtu mmoja au kundi ina uzito ule ule. Ishu sio Nape ishu kuvunjwa kwa katiba kipengele cha haki za binadam. Halafu napata shida unaelewa nini kuhusu neno "maendeleo" kwa mtazamo wako maendeleo ni ya uchumi tu na barabara na vitu vingine tangible? Ukisema maendeleo ni pamoja na ukiwaji wa demokrasia, uhuru wa kujieleza utawala wa sheria na kuheshimu haki za binadamu. Sasa usitulazimishe tuelekeze fikra zetu kwenye mankontena ukadhani ndio ishu ya maendeleo pekee, kilichotekea jana pia ni kipimo kikibwa sana ya kujua tumeudishwa nyuma kiasi gani na utawala huu kwenye maendeleo ya uhuru wa kujieleza. Nenda kajifunze tena maana ya mandeleo halafu uje ulete uzi mwingine. Wana JF Mtakubaliana na mm kua ktk ishu mbili hizi jana ishu ya Nape ndi ilikua na uzito mkubwa kiliko kontena kwa mujibu wa katiba yetu.
Nimecheka sana baba mtu. Hoja yako ni ya kitoto mno mkuu, maana ya human rights ni nini? Maana ya uhuru wa kujieleza ni nini? Unawezaje ukanishawishi kwamba chini ya Nape nyinyi wananchi mkazuiliwa kuona na kupata habari za bunge kwamba haikuwepo tatizo lolote kwa mujibu wa uelewa wako wa "freedom of speech"? Ukiwa kweli wewe ni mdau na kama kweli wewe ni msomi, ukinijibu hili basi tutaendelea na mjadara.
 
Back
Top Bottom