Azam Marine boresheni vyoo vilivyoko kwenye boti zenu za Unguja kwenda Pemba

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,615
Nimesafiri na Boti za Azam kutoka Dar kwenda Unguja mara nyingi, wamefanikiwa kuwa wasafi, ndani ya boat na hata kwenye vyoo vyao.

Zile "boat" zinazofanya safari ya Unguja kwenda Pemba na Pemba kuja Unguja kwa kweli ni chafu. Ni chafu kuanzia kwenye viti hadi vyooni.

Sielewi ni kwa nini mamlaka hazifanyi ukaguzi ila kusema ukweli unaweza kutoka na maradhi ya kuhara mara baada ya kusafiri na hizi boat. Ni uchafu mtupu.

Tazameni baadhi ya Picha zilizopigwa kwenye vyoo vya wanaume. Nimeelezwa na mhudumu mmoja ndani ya hizo "boti" kuwa vyoo vya wanawake ni vichafu mara kumi ya vyoo vya wanaume.

Azam Marine, boresheni hivi vyoo kwa kweli.

IMG_20211022_072615.jpg


IMG_20211022_072621.jpg


IMG_20211022_072635.jpg


IMG_20211022_072640.jpg


IMG_20211022_072647.jpg


IMG_20211022_072653.jpg
 
Vyoo low quality hivo na havidekiwi viko ka vyoo vya bar za uswahilini.
Boti za Dar-Unguja vyoo vyake ni classic. Sijui kwa vile wanapanda wazungu sanakwenda kutalii Unguja? Maana kutoka Unguja kwenda Pemba hakuna Mtalii anayekwenda huko
 
Back
Top Bottom