Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Gazeti kiwango kwa habari za mastaa nchini, Risasi Mchanganyiko lipo kwenye nafasi nzuri ya kuliandika hilo baada ya kunasa matamshi ya Sarah ambaye ameeleza kuwa anafikiria kusoma albadili ili kukata mzizi wa fitina.
Sarah alisema, baada ya yeye kumfumania Aunt akiwa kwenye kitanda chake na Silva, huku wote wakiwa watupu, kumekuwa na kauli nyingi za upotoshaji, hivyo kusisitiza kuwa pengine ikisomwa albadili (dua ya kulaani), ukweli unaweza kujulikana.
Alisema, hapo kabla hakuwahi kuwa na ugomvi na Aunt kiasi cha kufikia hatua ya kumzushia fumanizi, isipokuwa alichokitekeleza ni kile alichokishuhudia kwa macho yake kwamba mrembo huyo alimsaliti kwa kutoka na aliyekuwa mchumba wake ambapo aliwanasa kitandani kwake.
Nimekuwa nikimsikia Aunt anatangaza kuwa sikumfumania, isipokuwa ni chuki zangu binafsi, ameniudhi sana, yaani anataka Watanzania wanione mimi ni muongo ila mkweli ni yeye, alisema Sarah na kuongeza:
Nafikiri ni lazima Watanzania waufahamu ukweli ni upi, mimi nilimfumania Aunt kwa macho yangu, kama anabisha basi awe tayari isomwe albadili ili imdhuru yule ambaye anasema uongo, nipo tayari wakati wowote.
Aliendelea kusema, Aut ni msaliti kwa sababu aliufahamu fika uhusiano wake na Silva, ila kwa sababu ana tamaa ndiyo aliona ni vema kuingilia penzi lake, kitu ambacho ni kibaya kwa watu wanaofahamiana.
Sarah alisema, baada ya kumfumania Aunt, mrembo huyo alitoka nguo mkononi, hivyo anashangaa kuona anavyowahadaa watu ili wadanganyike kuwa hakufumaniwa, bali anasingiziwa.
Nimsingizie kwa kipi hasa? Sina sababu ya kufanya hivyo wala siwezi kupata maslahi yoyote kwa kufanya hivyo, labda yeye ndiyo mwenye maslahi kwangu kwa sababu alikuwa anakula jasho langu kupitia kwa Silva ambaye nilikuwa namfadhili kila kitu.
Nipo tayari sasa, najua anatumia nguvu nyingi kujisafisha lakini tunaweza kumaliza ubishi, isomwe albadili halafu tuone nani ni mkweli. Muongo atadhurika, kwahiyo Watanzania watapata jawabu kupitia mimi na yeye, alisema.
Baada ya kuongea na Sarah, gazeti hili lilichoma muda wake kuongea na Shehe Yusuf Kinduka wa msikiti mmoja jijini Dar es Salaam ambaye alisema kuwa albadili ni kisomo cha kiapo kwa watu ambao wanasuguana.
Ni kiapo tu, huyu anaweza kumtuhumu mwenzake ambaye naye anakuwa anapinga, kwahiyo albadili husomwa hapo kwa lengo kwamba kama ni kweli mtuhumiwa ni mkosaji basi apate adhabu kutoka kwa Mungu endapo atakuwa amesingiziwa, adhabu itamrudia yule mlalamika.
Si dua nzuri kuisoma kwa mtu kwa sababu inapojibu, huwa inakuwa kali mno kwa yule inayemshukia. Kwa kawaida haina gharama, ni bure kwa sababu ni kumshtakia Mungu ila unaweza kuamua kutoa sadaka pale unapoona inabidi, alisema Shehe Yusuf.
Aunt, alifumaniwa hivi karibuni na Sarah, kisha gazeti hili katika toleo lake la Jumamosi ndilo lilikuwa la kwanza kuripoti habari hiyo, ingawa mrembo huyo anayewika kwenye kiwanda cha filamu hivi sasa, amekuwa akijitembeza kukanusha.
http://www.globalpublisherstz.com/2009/11/25/aunt_ezekiel_kusomewa_albadil.html