“Attention + Repetition = Normalization”

“Attention + Repetition = Normalization”

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,065
Reaction score
1,412
Kwa nini mambo mabaya mengi huongezeka licha ya kukemewa ?

Kuna mdau ameniuliza swali hili

Pombe ni mbaya, kila siku tunaisema ila wanywaji wanaongezeka?
Mauaji ni mabaya, kwa nini kila siku yanaripotiwa ila hayapungui?

Jibu langu

Akili ya mwanadamu inahifadhi
Unaposema mara kwa mara:
“Usinywe pombe… usinywe pombe… usinywe pombe…”
Akili haisikii “usi-”
Inabeba “pombe.”
Hapa ndio inapoingia ile dhana ya kisaikolojia
Illusory truth effect — jambo likirudiwa mara nyingi, linaanza kuonekana la kawaida… hata kama ni baya.

Tatizo sio kusema — tatizo ni unasema vipi?.
Ukirudia kitu bila mwelekeo wa elimu na maadili, unakipa nguvu.
Ukikiweka hadharani kwa style ya kuvutia, unakitangaza.
Ukikizungumzia bila mipaka, unakifanya kiwe cha kawaida.

👉 “Attention + Repetition = Normalization”

Unachokipa attention, unakikuza.
Unachokirudia, unakijenga ndani ya akili za watu.

Sigara imeandikwa ni hatari kwa afya ila ni moja ya bidhaa zenye soko kubwa

Ndio maana wanazuoni walikuwa makini sana.
Madhambi makubwa hayakutajwa kwa lugha ya kuyafanya yaonekane ya kuvutia…
Bali kwa:
• Lugha ya kufundisha
• Lugha ya kuonya
• Lugha ya kukatisha tamaa
Sio lugha ya “kuchochea udadisi.”
Na ndivyo mafundisho mengi ya kidini yalivyo

Leo hii changamoto
Kuna mambo zamani yalikuwa yanazungumzwa kwa tahadhari…
Lakini leo:
• Yapo kwenye nyimbo
• Yapo kwenye mitandao
• Yapo kwenye TV
• Yapo hadi kwenye katuni
Sio kwa lengo la kufundisha… bali kuvutia.
Matokeo yake?
Watu hawaogopi tena…
Watu wanakuwa na curiosity ya kujaribu.
Ukirudia jambo bila hekima, unaligeuza kuwa wazo.

Ukilipa attention, unaligeuza kuwa hamu.
Ukili-normalize, unaligeuza kuwa tabia.

Hivyo basi:

Sio kila kitu kinahitaji kusemwa sana…
Na sio kila kinachosemwa kinahitaji kusemwa kwa style ya kuvutia.
Kuna mambo ukitaka yapungue,
yafundishe kwa ukali na hekima — sio kuyapa umaarufu.

Abuuabdillah ✍️
 
Kama repetition ndiyo inafanya kitu kiwe normal… mbona ‘usifanye ufisadi’ inarudiwa kila siku lakini mafisadi hawaishi?

Mbona elimu na maadili vinapewa attention kila siku ila havikui kwa speed hiyo hiyo?
 
Hapo kwa pombe nimefika nikaruka kama swala kutua chini yake. Imbeni hata ikiwezekana itengenezee na movie kabisaa lakin ujue pombe sio mbaya bali kupindukia ndo shda. Konyagi ilivotamu bro unambie ni mbaya. Kesho nunua nyama kilo mbili na mchele wakupikie kilo na nusu unywe soda 3 na maji unywe ya kutosha kama hatutakwambia r.i.p kwa kula excess. Kila kitu duniani nikibaya kikizidi, hata asali na utamu wake ukinywa nying utaharisha hadi pipe iseme poo. FREE Lissu
 
Kama repetition ndiyo inafanya kitu kiwe normal… mbona ‘usifanye ufisadi’ inarudiwa kila siku lakini mafisadi hawaishi?

Mbona elimu na maadili vinapewa attention kila siku ila havikui kwa speed hiyo hiyo?
MVUTO

Watu kwa sasa hawaangali faida na hasara, wanaangalia mvuto.

Mifano halisi:
I)nishasikia FB watu wengi wanapost ujinga sana. Na ukiangalia wanaoongoza kwa kuwa na likes nyingi, viewers na followers wengi, ni wanaopost ujinga.

II)wasanii wa muziki(wanamuziki) % kubwa wanaimba ujinga. Lakini hatuthubutu kaacha kuwafuatilia. Mfano halisi ni KONTAWA. Jamaa mistari yake haileweki lakini uimbaji wake una MVUTO. Kifupi nyimbo za zamani kiujumla, ni nzuri. Ila za sasa ni mbovu lakini zinamvuto.

Kama kwenye elimu ya madaftari ndo kabisaaaa hakuna mvuto.
 
MVUTO

Watu kwa sasa hawaangali faida na hasara, wanaangalia mvuto.

Mifano halisi:
I)nishasikia FB watu wengi wanapost ujinga sana. Na ukiangalia wanaoongoza kwa kuwa na likes nyingi, viewers na followers wengi, ni wanaopost ujinga.

II)wasanii wa muziki(wanamuziki) % kubwa wanaimba ujinga. Lakini hatuthubutu kaacha kuwafuatilia. Mfano halisi ni KONTAWA. Jamaa mistari yake haileweki lakini uimbaji wake una MVUTO. Kifupi nyimbo za zamani kiujumla, ni nzuri. Ila za sasa ni mbovu lakini zinamvuto.

Kama kwenye elimu ya madaftari ndo kabisaaaa hakuna mvuto.
Kontawa unaona haeleweki… lakini ana audience kubwa.

Kwahiyo tuseme tatizo lipo kwa msanii au kwa wewe kutokucatch wavelength yake?
 
Back
Top Bottom