Atheism: Imani nusu na robo

Atheism: Imani nusu na robo

Kwa nini dictionary zinakuwaga na edition mbali mbali? ni sababu ipi inayokufanya uiamini dictionary?

Hoja ilikuwa kuonyesha sio tu wadau wa JF bali source zingine pia zina unga mkono. By the way nini itakayo nifanya nikuamini na wewe?
 
Na huu ndio mkanganyiko mwingine nilioutaja kwenye post
Reasoning ipo pia kwenye Biblia sayansi imelala pale..kwahiyo haya uliyoyataja ni part n parcel ya Biblia
Ni vigumu kukubali kuwa Kristo alikuwepo lakini ukakataa uwepo wa Mungu
Mkuu biblia na reasoning ni mbali na mbali kabisa ni sawa na biblia na sayansi.
Ninavojua mimi lakini
 
Swali moja fupi sana na rahisi ambalo unaweza kumuuliza atheist na akashindwa kabisa kukujibu ni 'wewe ni nani'? Na hapa ndio inapokuja ile dhana ya reasoning
 
Unajua kuna vitu vingine vimejaa upotoshaji na atheism ni kimojawapo! Dhana ya uwepo wa Mungu ni ya kiroho zaidi kuliko kimwili, na vitu vya kiroho ni vya kiimani zaidi visivyoonekana na visivyoweza kuthibitishwa kisayansi lakini haiondoi ukweli na uhalisia wake
Ni kwa muktadha huu ndio maana wengine wakaamua kujitengenezea masanamu ili wayaabudu
Tukirejea kwenye msingi wa post atheism katika uhalisia wake ni imani..hata kamusi inathibitisha hivyo lakini kwangu mimi ni imani isiyotimia
Hapa mada imebadilika kutoka ''Atheism imani nusu na robo, hadi Atheism ni upotoshaji'' ili kujibu hii mada ya pili, yafaa kuleta shahidi sasa....maana kama mmoja atasema Atheism ni upotoshaji na mwingine akasema Dini ndio upotoshaji, nani atakaye kuwa sawa au atakayekosea? Hapo ni shahidi/Evidence ndizo zitakazo amua hiyo case.
 
Mkuu biblia na reasoning ni mbali na mbali kabisa ni sawa na biblia na sayansi.
Ninavojua mimi lakini
Sayansi inaonyesha jinsi vitu vilivyo, bila kuonyesha kusudi lake. Why are we here? What is purpose of life? Biblia inatoa maana na lengo la vitu ivo.
 
Hapa mada imebadilika kutoka ''Atheism imani nusu na robo, hadi Atheism ni upotoshaji'' ili kujibu hii mada ya pili, yafaa kuleta shahidi sasa....maana kama mmoja atasema Atheism ni upotoshaji na mwingine akasema Dini ndio upotoshaji, nani atakaye kuwa sawa au atakayekosea? Hapo ni shahidi/Evidence ndizo zitakazo amua hiyo case.
Hapana haibadiliki bali ni mwendelezo kitu ambacho hakijatimia kama mifano niliyotoa ya vipimo chaweza kuwa upotoshaji kwa yule asiyejua
Kwamba unajua kabisa hii sio kilo moja ni nusu na robo lakini unasema ni kilo moja!kwakuwa tu vinakaribiana uzito...! Huu ni upotoshaji
 
Hapana
Infact haujawahi kuwepo ushahidi makini kuwa kuna Mungu.
Wakati atheism ikiwa ni belief nadhani ina fall short kuwa Religion, japo ina viji character vya religion
Kwanza hakujawahi kuwepo kwa ushahidi kuwa Mungu yupo, hapo upo sawa....lakini kusema Atheism ni imani ambayo yaweza kuangukia katika jamii ya dini, siyo kweli.Narudia tena Atheism ni ukosefu/absence wa imani juu ya uwepo wa Miungu,Mungu,au Shetani(Deities).Kwa hiyo Atheism haina vigezo vya kuwa dini maana haina msingi (Imani) wa dini.
 
Aaah! Hapo sasa ndo utakuja kuachana na ma atheist, reasoning siku zote haina altenaltive mkuu.
Hapana ili uwe reasonable huwezi kuwa rigid kwahiyo reasoning ina mbadala
 
Imani ni kule kukubali kwamba kitu flani kipo.Na ili uamini lazima pawepo na ushahidi wa kuwepo kwa unacho amini kipo.Imani zipo za aina mbali mbali, kwa mfano mimi naamini kwamba Rais wa JMT ni JPM kwa kuwa kuna ushahidi.Lakini Atheism haikubali Imani inayosema Mungu yupo kwa sababu hakuna shahidi za kusapoti hiyo imani.
Kwa hiyo atheists wanategemea ushahidi ambao ni physical kama ulivyotoa wa JPM hapo juu. Kwa hiyo hawaamini katika gravitational na magnetic forces, maana hizi huzioni kwa macho. Ina maana hitimisho lao la kutokuwepo Mungu limetokana na kwamba hawakuwahi kumwona kwa macho, siyo? Je, wamewahi kuona kwa macho nguvu zinazoweka nyota na sayari kukaa sehemu zilipo bila kukaribiana au kugongana? au Je, wamewahi kuona kwa macho nguvu inayozuia maji ya bahari yasi overflow na kusambaa nchi kavu?
 
Hoja ilikuwa kuonyesha sio tu wadau wa JF bali source zingine pia zina unga mkono. By the way nini itakayo nifanya nikuamini na wewe?
Kuungwa mkono na wengi kwa uwepo wa kitu flani, haitoshi kudhibitisha kuwa kitu flani kipo.Mimi sijakushawishi uamini uwepo wa kitu flani, ndio maana sina haja ya kukupa shahidi...lakini kama nitamtaka mtu aamini uwepo wa kitu flani, nitamjia na shahidi...sasa wewe unataka uniamini kwa lipi?
 
Sayansi inaonyesha jinsi vitu vilivyo, bila kuonyesha kusudi lake. Why are we here? What is purpose of life? Biblia inatoa maana na lengo la vitu ivo.
Hahaha
Sasa purpose of life ukisoma kwenye biblia ndo haileti maana yyte
Ki ufupi ni kuwa swali la purpose of life tumejitunguia wenyewe na kama ipo hiyo purpose sisi ndo tunaikamilisha ila kwenye bible hakuna reasonable answer
(Najibu ki atheist zaid)
 
Hapana ili uwe reasonable huwezi kuwa rigid kwahiyo reasoning ina mbadala
Ndio lakini reasoning pia haiwezi kuwa na mbadala kwamba usipo elewa kwenye hali moja ni kwa sababi hauko kwenye hali nyingine
Reasoning ikishaweka kiroho ina siz kuwa reasoning
 
Hapana haibadiliki bali ni mwendelezo kitu ambacho hakijatimia kama mifano niliyotoa ya vipimo chaweza kuwa upotoshaji kwa yule asiyejua
Kwamba unajua kabisa hii sio kilo moja ni nusu na robo lakini unasema ni kilo moja!kwakuwa tu vinakaribiana uzito...! Huu ni upotoshaji
Labda nikuulize, je Mungu/Shetani yupo? una ushahidi wa uwepo wake?....Ukijibu hayo maswali basi Atheism inakufa automatically.
 
Kwa hiyo atheists wanategemea ushahidi ambao ni physical kama ulivyotoa wa JPM hapo juu. Kwa hiyo hawaamini katika gravitational na magnetic forces, maana hizi huzioni kwa macho. Ina maana hitimisho lao la kutokuwepo Mungu limetokana na kwamba hawakuwahi kumwona kwa macho, siyo? Je, wamewahi kuona kwa macho nguvu zinazoweka nyota na sayari kukaa sehemu zilipo bila kukaribiana au kugongana? au Je, wamewahi kuona kwa macho nguvu inayozuia maji ya bahari yasi overflow na kusambaa nchi kavu?
NDIYO! Atheism inahitaji physical evidence ili kuamini uwepo wa Mungu.Magnetic force huchagizwa na mvutano wa kielektronic baina ya vitu viwili...Electron ni vitu vinavyoonekana....Kuhusu gravitational hiyo ipo wazi, inaweza kuchunguzika na kutoa majibu....je Mungu anachunguzika na kutoa majibu bila msaada wa akili ya binadamu?
 
Naamini katika Mungu mmoja na uwepo wa shetani-kwa maana ya kiroho na si kimwili lakini
Hebu ingia hapa nikiri wazi:namfahamu shetani
Atheism inahitaji physical evidence ili kuamini katika Mungu, haitambui uwepo wa roho....iweje uache kuleta physical evidence lakini useme roho ina affect mwili?...kipi kinakufanya uamini uwepo wa Shetani?
 
Atheism inahitaji physical evidence ili kuamini katika Mungu, haitambui uwepo wa roho....iweje uache kuleta physical evidence lakini useme roho ina affect mwili?...kipi kinakufanya uamini uwepo wa Shetani?
Una roho au huna roho?

Naenda kilingeni nina session nitarejea alfajiri..naamini utakuwa umenijibu
 
Kwanza hakujawahi kuwepo kwa ushahidi kuwa Mungu yupo, hapo upo sawa....lakini kusema Atheism ni imani ambayo yaweza kuangukia katika jamii ya dini, siyo kweli.Narudia tena Atheism ni ukosefu/absence wa imani juu ya uwepo wa Miungu,Mungu,au Shetani(Deities).Kwa hiyo Atheism haina vigezo vya kuwa dini maana haina msingi (Imani) wa dini.
Anhaa sasa nimekusoma

Wakati kuna vitu karibu sita atheist wanavyo na dini inavyo, mi ntakuoa baadhi tuu lakini navyo ni

masimulizi, mfano Mungu alimuumba adam, lakini atheist watakuja na evolution

Ethics/maadili, nadhami hapa sina haja ya kueleza wote wana futa hiyo kitu

Mafundisho(doctrine), dini zinatumia quran na bible lakin ma atheist wana tumia vitabu vyao vya kina dawkins, marx na drwin na wengine

Matirio (material), wakati dini ina vitu kama makanisa, sananu na vitu vingine ma atheist wana amini kwenye nature(yaani vitu asilia)

Rituals nadhani kwa kiswahili ni ibada, hiki ndio kigezo kikubwa ambacho ma atheist hawana na ndio kina watofautisha na dini hizo, huwezi kuta atheist anatoa sadaka au ana swali mainly kwa kuwa haamini Mungu

Kwa hiyo wakati ma atheist wana baadhi ya element za kidini, hawana zile za muhimu kuwafanya waifikie dini kabisa ndio maana ni kasema wana fall short kuwa religion ila tabia za ki religion baadhi zimo.
 
Back
Top Bottom