Ili kuzuia mafuriko lazima mafuriko yawepo au yawe yamewahi kutokea...kama hujawahi kuona mafuriko wala hayajawahi kuwako huwezi kuyazuia.Kwa hiyo Atheism haipingi uwepo wa Mungu bali haitambui uwepo wa Mungu kutokana na kukosekana kwa ushahidi wenye nguvu.Kupinga kitu ni kule kukataa kukikubali hata kama kitakuwepo, lakini kwenye Atheism ukipeleka ushahidi wa kueleweka kwamba Mungu yupo, basi Imani juu ya uwepo wa Mungu itakubalika.Kukataliwa kwa imani juu ya uwepo wa Mungu kwenye Atheism ni kutokana na ukosefu wa ushahidi wenye nguvu juu ya uwepo wake na siyo kwamba ni kasumba ya kukataa tu.Kama Mungu atajitokeza leo na kujidhihirisha kwa watu, Atheism itafikia ukomo wake.