Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Kwa mawazo yangu nashauri vitu vifuatavyo vingine wengine mtajazia
ili kuliokoa shirika letu la ndege.
1.ATC wanabwata kuwa wanahitaji ndege nyingi zaidi (quantity) Swala si uwingi wa ndege kama wanavyodai bali ni uhakika wa HUDUMA hizo ndege (quality) bila kujali ni moja au nyingi.Mfano precision AIR walianza na ndege moja ikawa inaenda kwa wiki mara mbili bukoba kama sikosei lakini walikuwa waaminifu sana na hizo safari zao mbili kwa wiki.Serikali isiwape mabilioni wanayotaka kuomba kwanza.Ni heri waruke hata mara moja kwa mwezi lakini wawe reliable na quality za huduma zao ziwe nzuri.Watu wataanza kuwaheshimu na kuwaamini.Wapunguze wafanyakazi,routes,na gharama za uendeshaji na waweke menejimenti ndogo ya watu wachache wenye akili sana na wajuao kutumia hizo akili kuendesha shirika kwa faida.Inaelekea ATC kumejaa wajinga wengi kuanzia bodi,manajimenti hadi kwa wafanyakazi wa kawaida ndiyo maana haliendi vizuri.Kama haiwezekani serikali iajiri menejimenti yenye uwezo kutoka nje iendeshe kwa muda au iombe Ethiopian Airline watuazime baadhi ya watu wao waje watusaidie kwa posho kidogo Kwenye menejimenti.Kikwete aongee na Raisi wa Ethiopia ni mtu mzuri nadhani aweza msaidia.
2.Wawe makini kuchagua routes zenye faida ndani na nje ya nchi.Sasa hivi inaonyesha wanaruka tu kama vichaa.Kuna njia ATC haiwezi kushindana kabisa,Njia kama ya kwenda Johansburg wameshindwa kabisa wala huhitaji mtaalamu wa safari za anga kuwaeleza kuwa imewashinda.
3.Wawe na uhusiano mzuri na serikali na ma-ajents wa kukata tikiti.Serikali mara nyingi huwa na watumishi wanaosafiri mara kwa mara kikazi n.k ndege za ATC zikiwa za kuaminika na wakawa na uhusiano mzuri na serikali serikali ingaliweza kuwa inawapa tenda nyingi na ingeamuru wafanyakazi wake kuwa lazima wasafiri na ATC unless labda hiyo route ATC iwe haiendi.Lakini naona hata serikali inaogopa maana ATC wengine hupenda kuiita ANY TIME CANCELLATION AIRLINE .Uhusiano wa kuaminika na maajenti wakata tikiti ni muhimu mno.Kuna maajenti ukienda wakitaka kukukatia tikiti wanaanza kwanza kukutajia ndege zingine na siyo ATC.ATC nadhani kichwani mwao huwa haipo kabisa wanaanza kwanza mashirika mengine lakini siyo ATC kwa nini nadhani ATC wanalo jibu la kwa nini maajenti wa kukata tikiti hawawapi kipaumbele.
ili kuliokoa shirika letu la ndege.
1.ATC wanabwata kuwa wanahitaji ndege nyingi zaidi (quantity) Swala si uwingi wa ndege kama wanavyodai bali ni uhakika wa HUDUMA hizo ndege (quality) bila kujali ni moja au nyingi.Mfano precision AIR walianza na ndege moja ikawa inaenda kwa wiki mara mbili bukoba kama sikosei lakini walikuwa waaminifu sana na hizo safari zao mbili kwa wiki.Serikali isiwape mabilioni wanayotaka kuomba kwanza.Ni heri waruke hata mara moja kwa mwezi lakini wawe reliable na quality za huduma zao ziwe nzuri.Watu wataanza kuwaheshimu na kuwaamini.Wapunguze wafanyakazi,routes,na gharama za uendeshaji na waweke menejimenti ndogo ya watu wachache wenye akili sana na wajuao kutumia hizo akili kuendesha shirika kwa faida.Inaelekea ATC kumejaa wajinga wengi kuanzia bodi,manajimenti hadi kwa wafanyakazi wa kawaida ndiyo maana haliendi vizuri.Kama haiwezekani serikali iajiri menejimenti yenye uwezo kutoka nje iendeshe kwa muda au iombe Ethiopian Airline watuazime baadhi ya watu wao waje watusaidie kwa posho kidogo Kwenye menejimenti.Kikwete aongee na Raisi wa Ethiopia ni mtu mzuri nadhani aweza msaidia.
2.Wawe makini kuchagua routes zenye faida ndani na nje ya nchi.Sasa hivi inaonyesha wanaruka tu kama vichaa.Kuna njia ATC haiwezi kushindana kabisa,Njia kama ya kwenda Johansburg wameshindwa kabisa wala huhitaji mtaalamu wa safari za anga kuwaeleza kuwa imewashinda.
3.Wawe na uhusiano mzuri na serikali na ma-ajents wa kukata tikiti.Serikali mara nyingi huwa na watumishi wanaosafiri mara kwa mara kikazi n.k ndege za ATC zikiwa za kuaminika na wakawa na uhusiano mzuri na serikali serikali ingaliweza kuwa inawapa tenda nyingi na ingeamuru wafanyakazi wake kuwa lazima wasafiri na ATC unless labda hiyo route ATC iwe haiendi.Lakini naona hata serikali inaogopa maana ATC wengine hupenda kuiita ANY TIME CANCELLATION AIRLINE .Uhusiano wa kuaminika na maajenti wakata tikiti ni muhimu mno.Kuna maajenti ukienda wakitaka kukukatia tikiti wanaanza kwanza kukutajia ndege zingine na siyo ATC.ATC nadhani kichwani mwao huwa haipo kabisa wanaanza kwanza mashirika mengine lakini siyo ATC kwa nini nadhani ATC wanalo jibu la kwa nini maajenti wa kukata tikiti hawawapi kipaumbele.