ATC chali tena.....!!!

ATC chali tena.....!!!

Sajenti

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2008
Posts
3,651
Reaction score
416
Habari za kuaminika ni kuwa shirika la ndege ATC limeshindwa kufanya safari zake kutokea Dar kwenda Kigoma tangu tarehe 10 May 2010.

Kwa mujibu wa mtu mmoja wa karibu aliyetakiwa kusafiri na ndege hiyo siku ya Jumatatu tarehe 10 kwenda kigoma, walifahamishwa kuwa ndege hiyo imefutwa bila ya kupewa maelezo yoyote ya maana. Baada ya sintofahamu ya muda mrefu ilikuja kubainika kuwa ndege iliyotakiwa kuruka siku hiyo kwenda kigoma kutoka Dar imevunjika kioo chake kimoja na kuwa ATC iko katika harakati za kuagiza kioo hicho kutoka nje. Hadi leo kioo hicho hakijapatikana na abiria waliotakiwa kusafiri kwa ndege hiyo kwa pande zote mbili baadhi walirudishiwa pesa zao ili wafanye mipango mingine wale wasio na haraka wanaendelea kusubiri na wengine walisafiri kwa Precision Air mpaka Mwanza na Shinyanga....Ndio ATC hiyo kuna mtu aliwahi kuniambia ATC ni kirefu cha Any Time Cancellation...
 
Wakati mwingine huwa nafikiria kuwa ni bora hilo shirika lingefutwa kabisa then biashara ya ndege wangeachiwa watu wenye pesa zao waendeshe kuliko eti kujifanya kuwa tuna shirika la ndege kumbe ni usanii kwa kwenda mbele!
 
Ukifika huko utakuja na

bora nchi ingefutwa kabisa na isahaulike tanzania ...nahisi wana matatizo na wanaitaji kusaidiwa kisaikolojia...
 
Airline of Total Cancellation

Majina mengi kama haya ndiyo yanyowafaa.

Airline of Total Collapse.
Lakini ina uma sana ninapofikiria kwamba hamna kitu tunachoweza kusema tunaweza.
basi tu.
Lkn tusife moyo, tupiganie kuitoa ccm, nadhani tutasuruhisha mambo mengi.
 
1. Nimuunge Mkono PDIDY Kuhusu kusaidiwa kisaikolojia. Maana haiyumkiniki Nchi zote zilizotuzunguka ziwe na ndege na safari za uhakika sisi tuwe hivi. Ona Rwanda, Burundi,Uganda. Kenya usiseme kabisa.!!!!!!!!!Tunani sisi??????????? Kama hizo habari za kuaminika kuwa shirika la ndege ATC limeshindwa kufanya safari zake kutokea Dar kwenda Kigoma tangu tarehe 10 May 2010. Baada ya kubainika kuwa ndege iliyotakiwa kuruka siku hiyo kwenda kigoma kutoka Dar imevunjika kioo chake. Ipo siku watarusha ndege angani huku tanki la mafuta linavuja. TUOMBE MUNGU HAYA YASITOKEE HAPA KWETU WALA YASITOEE WAKATI WA BARIDI!

ATC = Anyway,Time Counts!
 
Nakumbuka huko nyuma niliwahi kuuliza katika mojwapo ya threads on ATC woes: Hivi kweli ni lazima tuwe na shirika la ndege la umma? Nilishauri ni vyema serikali ingetumia nguvu zake na fedha kusitawisha usafiri wa reli kuliko ule wa ndege. sababu ya hii iko wazi kabisa.
 
Back
Top Bottom