Atayaweza majukumu huyu kweli?

Atayaweza majukumu huyu kweli?

Sikia my dear nikwambie dizain ya mwanaume kama huyo ni bahili.. tafuta siku akiwa na mood mnzuri sana mwambie "nataka niongeze stock ya chakula kuna vitu hivi na hivi hakuna kwa hiyo naomba niongezee pesa ninunue".
Then hapo msome uso wake atakavyo respond ndio utapata jibu uko na mwanaume wa aina gani.

Nlishawahi kumuambia naomba hela nikanunue gas nikaambiwa 'mwisho wa mwezi' heee! Kwa hyo nisipike mpaka mwisho wa mwezi? Nikanunua gas na siku alivyokuja hata hakuuliza nimeipataje na mwisho wa mwez ulifika akapiga kimya mpaka leo hii nnapoandika
 
Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.

Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.

Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.

Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Chumba nikodi mie, kitanda ninunue mie, Chakula ninunue mie, kula ule wewe x3. Majangaaa.......Eeeeeh.....Majangaaa.......x3
 
Kwani we ukienda kwake hutakuwa unakula au utakuwa waenda na chakula chako?

Mimi kwake sina kawaida ya kwenda sana. Kwanza sina muda af ramani imekaa vibaya yan nikitoka kazini niende kwake ndo nirudi kwangu tofauti na yeye akitoka kazini anapita kwangu then anaenda kwake. Au unazungumzia nini?
 
ulishamweleza mahitaji yako ? inawezekana anafikiri una hela za urithi ndiyo sababu hashituki, jaribu kumshitua kidogo utaona anatoa fedha zaidi ya unavyifuikiria

Anaelewa sana mazingira yangu kuwa ni magumu
 
Nina uhakika kuna makubalianao au mazoea ambayo mlianzishiana hapo mwanzoni ndiyo maana anajiamini kwa lolote, sidhani kama alikurupuka tu

Hapana. Hakuna makubaliano yoyote,yangekuwepo nisingekuja kuuliza hapa
 
Asante kwa ushauri ila mm huwa naogopa kuanza kulizungumzia maana ataona km namnyanyasa vile

Tamaduni zetu sometimes zinatufanya kuwa watumwa, just talk to him how can he bring his ass there and sit wait for free lunch! Ungekuwa demu wa kizungu yani wala usingehitaji kuja humu maana ni 50/50, hata mkitoka out kila mtu anajijua hadi train mnalipa separate!

Anyway poa tu mvumilie
 
kwa kweli tabia zake sio promising,lakini put that issue on table,hakuna mkamilifu hata mmoja huo ndio udhaifu wake kama utaubeba songambele,hata ukienda kwa mtu mwingine atakua na udhaifu mwingine hali kadhalika!love your man and let love take care of other things!

Asante
 
Ujue kuna wanaume wana nature ya kulelewa eeh huyo mmoja wapo!!! Em siku moja mwambie dia leo sijapika sina hata unga ndani.. !! Kama ajakwambia 'kakope' !!

Hahaaaa utaambiwa mwanamke gani unakaa bila unga ndani
 
Usimlaumu kabla hujamwambia.Hebu mwambie usikie jibu lake. Kwani wewe umekumbushwa vingapi. Watu wanakubushwa mpaka kuvaa ch*pi. !!
 
Huyo siyo huzband material tupa kule unajipalilia makaa ya moto kichwani mapema yote???ogopa sana mwanaume anaependa mteremko hachelewi kuja kukukimbia akipata jimama lampa kila kitu
 
Usimlaumu kabla hujamwambia.Hebu mwambie usikie jibu lake. Kwani wewe umekumbushwa vingapi. Watu wanakubushwa mpaka kuvaa ch*pi. !!

Sawa ila me najua kuna mengine sio ya kukumbushwa kama ambavyo mimi hanikumbushi kupika. Akiniambia anakuja najua kwa vyovyote atahtaji kula ko napika
 
Na kama akikimbia baada ya kumweleza ukweli au akilipuka pamoja na wewe kumweleza kwa lugha rahisi, basi pia hakufai kwa sababu msingi wa uhusiano thabiti ni maelewano na uwezo mlionao katika kutatua matatizo yenu kwa mazungumzo.
Kama hauko huru kuzungumza nae au yeye hayuko huru kukusikiliza basi huo uhusiano bado ni mchanga hamfahamiani vizuri na mjipe muda wa kufahamiana au hamuendani, yani wote mnaishi kwa kuficha uhalisia wa maisha yenu au tabia zenu.
Uhusiano mzuri ni ule ambao mtu anakuwa huru kutoa mawazo yake na kusikilizwa na pia kufikia muafaka bila shari au hata ikitokea, inasuluhishwa bila kuhusisha mtu wa tatu labda kwa maswala kama kukosa uaminifu na yenye nature hiyo.

Nimekupenda bure Uso wa nyoka.
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.

Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.

Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.

Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Halafu jianaume la aina hii ukitangaza kulistishia huduma tu linakutafuta likuchome visu! Uliipata ile ya Arusha dogo kapiga binti wa watu visu baada ya kustishiwa huduma?? WANAWAKE MNA KAZI!!!
 
Nlishawahi kumuambia naomba hela nikanunue gas nikaambiwa 'mwisho wa mwezi' heee! Kwa hyo nisipike mpaka mwisho wa mwezi? Nikanunua gas na siku alivyokuja hata hakuuliza nimeipataje na mwisho wa mwez ulifika akapiga kimya mpaka leo hii nnapoandika

Ulisema hana dharau. Sasa hii ni nin dada?
 
Kama ulikuwepo ila dharau sijaona labda km anazo za chinichini
Aisee kumbe hii kitu ni kweli eenh! Ubahili inawezekana il a nafkiri hili kabila kuna jinsi wanavyomchukulia mwanamke kwamba umnyenyekee kama Mungu. So katika hili anaweza kujua kabisa unahitaji ila nafikiri wakiombwa ndio hujisikia uanaume wao umekamilika. Dharau ndo ustake kujua. Ukitaka kuenjoy oa hilo kabila ila kamwe usiolewe maana wanadharau mwanamke na familia yake kiujumla. As long as utaamua kuolewa ukitaka amani itabidi unyenyekee kama unavoendaga kwenye madhabahu kunyenyekea. Halafu utaolewa na kila mtu inshort kila mtu atataka akuendeshe kigezo ni kua we ni mke kwa hiyo ni mke wao. Hata mtoto teenager wa kiume atataka akuendeshe.Kaa mkao was kuendeshwa na kama huombi hupewi. Haya akina Omera na Nyako nishambulieni ila ukweli ndo huo. Bila kusahau ni wakarimu sana.
 
Back
Top Bottom