Atayaweza majukumu huyu kweli?

Atayaweza majukumu huyu kweli?

Hapana..nadhani anajaribu ku-test "breaking point" yako...Vumilia ukunjwe
 
Mh.. Hapo naona kuna hatari. Kama mtu hata kuchangia chakula anachokula hakumbuki, atakumbuka kweli kukuletea hata kijizawadi? Wadada mnapenda vijichokuleti..vi ais krimu.. mara vi naitdress.. vipafyum.. Utapata kitu hapo? Atakutoa out kweli huyo? Na bado unamuambia kiaina lakini waaala.. haiimuingii akilini? hapo kuna shida. Ukizingatia hiki ndio kipindi ilibidi aku-impress? Mwe! Halafu watu wa hivyo bwana.. huwa ni ngumu sana kubadilika!
 
Kuwa muwazi,mwambie mapungufu yake kama akwambiapo chakula asichokipenda.

Kama anweza yale majukumu mengine(kiini cha mahusioano) basi uliyoyataja yanarekebishika.
 
Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.

Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.

Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.

Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Kwa nini unamuona kuwa yeye ndiye mwenye tatizo badala ya kujiona wewe ndiye mwenye tatizo?
1. Kwa nini umeshindwa kumwambia kuhusu hili? Siku zote unamwangalia anakuja, anakula anaondoka. Yeye ameshaona kuwa huo ndio utaratibu wa maisha kwa sababu hukuwahi kumwambia kuwa anavyofanya si vizuri.
2. Kama unaiona hii tabia yake kuwa ni mzigo na bado unaendelea kuwa naye, basi inabidi ujichunguze kuona kama u mzima
 
Wanaume bwana,,,,,, mtelezo sio mzuri mwambie atimize wajibu wake hawezi kimbia.
 
Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.

Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.

Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.

Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?

kabla ya kuleta malalamiko yako hapa jukwaani umeishawahi kuongea nae kuhusu hii kitu au umekurupuka tu?kama unajitosheleza pengine mwenzio anaona hana haja ya kubebana na misosi.wakati mwingine inabidi ufikirie mambo kwa mapana yake,unaweza kushangaa akaja kuwa msaada mkubwa sana kwako katika mambo makubwa na ya muhimu kabisa kuliko hata huo msosi unaouligia kelele.unadhani asipokula kwako hana sehemu nyingine ya kula?au elf 3 ya ugali samaki inamkosa hadi adoee kwako?THINK BIG SISTER.LIFE IS MORE THAN JUST FOOD
 
Kuna topic fulan hapa iliwekwa na mwanaume akiomba ushauri juu ya mke wake ambaye hachangii chochote yaani hadi hela ya lunch kazini na vocha anaomba ilhali naye ni mwajiriwa, watu mlimponda sana eti analalamika vitu vidogo.

Jana kuna Topic ya jamaa aliyeibiwa Tsh 5000 Dodoma kwa mpenzi wake nayeye vivyo hivyo mlimponda. Hivi wanawake wamewapa nini nyinyi wanajukwaa?

Mwanamke akifanya lawama kwa mwanaume, mwanaume akifanya lawama kwa mwanaume...why? kuweni waungwana.
 
Hiyo tabia ya shemeji ni mbaya sana. Huyo ukimuendekeza utajikuta mkioana kila kitu unafanya wewe. Nimeyaona kwa shosti wangu. Wakati wa urafiki na shemeji alikuwa analalamika kuwa huyu mtu analeta nguo zake kila wiki nimfulie lakini haji na sabuni wala haachi hela ya sabuni. Chakula hivyo hivyo. Anatulalamikia sisi, tukimshauri anadai anaogopa kumuudhi. Wakaoana. Tunavyoongea hapa ana vidonda vya tumbo na presha. Yule baba hela yake haijulikani inakoendaga zaidi ya kujipara kwa nguo za gharama na saa. Mdada mzigo wote unaoujua unahusu hela ni wa kwake. Baba akijitahidi ni kununua kilo ya nyama jumapili. Silipendi mimi hili lishemeji!!! Kwanza jitambue, ukiona mwanaume wa aina hii haendani na matakwa yako jaribu kumweleza na uone kama atabadilika ingawa utu uzimani mabadiliko ni adimu, vinginevyo, anza mbele unless unataka kuolewa kuwafurahisha watu.
 
Mimi sisemi anihonge. Nataka walau achangie kile ambacho na yeye anakula. Inamaana mm ninapompa chakula mamhonga?

Mbona tatizo dogo kwanini usimwambie tu, Kama anajua majukumu yake atakuelewa hajui hawezi kukuelewa hapo utatakiwa kufikiria cha kufanya, Caution tengeneza njia nzuri ya kufikisha ujumbe.
 
Hakufai huyo ht haoni aibu kula bure ni mvivu wa kufikiri mkiowana cna hela ndo itakuwa kauli yake
 
Sikia my dear nikwambie dizain ya mwanaume kama huyo ni bahili.. tafuta siku akiwa na mood mnzuri sana mwambie "nataka niongeze stock ya chakula kuna vitu hivi na hivi hakuna kwa hiyo naomba niongezee pesa ninunue".
Then hapo msome uso wake atakavyo respond ndio utapata jibu uko na mwanaume wa aina gani.
 
Heeeeee mbona anakula basi, si asubiri atoe mahari ndo aje kula?! Hajui vile vyakula vinanunuliwa?? Mmmh uso umeumbwa na haya! Kila siku unakula una nawa unaondoka..! Mwanaume?!!!! Mfyuuuuuuu!

Na tena usikute huko kwengine anaitwa kimwaga makono..
 
Kwa nini unamuona kuwa yeye ndiye mwenye tatizo badala ya kujiona wewe ndiye mwenye tatizo?
1. Kwa nini umeshindwa kumwambia kuhusu hili? Siku zote unamwangalia anakuja, anakula anaondoka. Yeye ameshaona kuwa huo ndio utaratibu wa maisha kwa sababu hukuwahi kumwambia kuwa anavyofanya si vizuri.
2. Kama unaiona hii tabia yake kuwa ni mzigo na bado unaendelea kuwa naye, basi inabidi ujichunguze kuona kama u mzima

mi naona mdada hana kosa ana play part yake wanaume wengne wanapenda mteremko kuna vitu inabidi ufanye mwenyewe kwa kuona aibu si lazma uambiwe ndo mana bidada akataka ushaur.mwanaume unaenda kula kwa girlfriend hutoi hela unategemea nini
 
Back
Top Bottom