Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.
Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.
Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.
Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Wanaume bwana,,,,,, mtelezo sio mzuri mwambie atimize wajibu wake hawezi kimbia.
Nina uhakika kuna makubalianao au mazoea ambayo mlianzishiana hapo mwanzoni ndiyo maana anajiamini kwa lolote, sidhani kama alikurupuka tuHabari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.
Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.
Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.
Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Mmh hapa kunakitu kilichojificha mbona hali hii siyo ya kawaida.Jaribu kutafuta namna nzuri ya kumwambia ukweli wote uone atasemaje .Hapa ni kumwambia ukweli tu kwa busara zaidi .Ukiona anauchukia ukweli unaomwambia mkifunga ndoa sijui kama itadumu kweli.Mwambie ukweli lakini tumia busara sana.
Mh.. Hapo naona kuna hatari. Kama mtu hata kuchangia chakula anachokula hakumbuki, atakumbuka kweli kukuletea hata kijizawadi? Wadada mnapenda vijichokuleti..vi ais krimu.. mara vi naitdress.. vipafyum.. Utapata kitu hapo? Atakutoa out kweli huyo? Na bado unamuambia kiaina lakini waaala.. haiimuingii akilini? hapo kuna shida. Ukizingatia hiki ndio kipindi ilibidi aku-impress? Mwe! Halafu watu wa hivyo bwana.. huwa ni ngumu sana kubadilika!
Nimeipenda hii.Sasa we endelea kumuagiza usiache mpaka atajenga mazoea!
Kwa nini unamuona kuwa yeye ndiye mwenye tatizo badala ya kujiona wewe ndiye mwenye tatizo?
1. Kwa nini umeshindwa kumwambia kuhusu hili? Siku zote unamwangalia anakuja, anakula anaondoka. Yeye ameshaona kuwa huo ndio utaratibu wa maisha kwa sababu hukuwahi kumwambia kuwa anavyofanya si vizuri.
2. Kama unaiona hii tabia yake kuwa ni mzigo na bado unaendelea kuwa naye, basi inabidi ujichunguze kuona kama u mzima
kabla ya kuleta malalamiko yako hapa jukwaani umeishawahi kuongea nae kuhusu hii kitu au umekurupuka tu?kama unajitosheleza pengine mwenzio anaona hana haja ya kubebana na misosi.wakati mwingine inabidi ufikirie mambo kwa mapana yake,unaweza kushangaa akaja kuwa msaada mkubwa sana kwako katika mambo makubwa na ya muhimu kabisa kuliko hata huo msosi unaouligia kelele.unadhani asipokula kwako hana sehemu nyingine ya kula?au elf 3 ya ugali samaki inamkosa hadi adoee kwako?THINK BIG SISTER.LIFE IS MORE THAN JUST FOOD
Kuna topic fulan hapa iliwekwa na mwanaume akiomba ushauri juu ya mke wake ambaye hachangii chochote yaani hadi hela ya lunch kazini na vocha anaomba ilhali naye ni mwajiriwa, watu mlimponda sana eti analalamika vitu vidogo.
Jana kuna Topic ya jamaa aliyeibiwa Tsh 5000 Dodoma kwa mpenzi wake nayeye vivyo hivyo mlimponda. Hivi wanawake wamewapa nini nyinyi wanajukwaa?
Mwanamke akifanya lawama kwa mwanaume, mwanaume akifanya lawama kwa mwanaume...why? kuweni waungwana.