Atayaweza majukumu huyu kweli?

Atayaweza majukumu huyu kweli?

Mkuu umenena vema ila huu uzi ni wa zamani sana
Walk away!
Kama vile unavyomuonjesha ladha ya mke bora kwa kumpikia n so n so. Na yeye anatakiwa akuoneshe ladha ya mume bora kwa kukuhudumia. Wanasema ukiona mwanaume anadiriki kula chakula hajui kilipotoka huyo ni janga...Tena janga la dunia (Imeandikwa mwanaume utakula kwa jasho)
 
Mbali na hayo maswala ya chakula,mahitaji yako mengine anakutimizia vizuri?
 
Habari zenu wanaMMU. Nina mpenzi wangu ambae nnategemea kuwa atakuwa baba watoto ila ana tatizo (mimi naliita tatizo). Ni kwamba yeye ni mfanyakazi wa kampuni moja binafsi,ni kawaida yake huwa anakuja kwangu mara nyingi nampikia chakula.

Anaweza akatoka kazini anapitia kwangu anakula then anaenda kwake.

Hakuna siku utamsikia anasema dia hela hii hapa kanunue mchele au hata yeye mwenyewe kwamba anapokuja abebe walau maji ya uhai, hana muda huo kabisa. Gharama zote nazijua mimi. Tena anaweza kudiriki hata kusema chakula nlichopika ye hakipendi.

Sasa nauliza eti huyu mtu majukumu anayajua? Hata tukiingia ndoani si atanitwisha majukumu yote huyu? Au labda nyie wenzangu mnaonaje tabia hii, ni ya kawaida?
Kuna jambo vijana wa leo huwa hamlifahamu na ndilo linawarudisha nyuma kila uchao kuhusu mahusiano.

Jambo lenyewe ni kuhusiana na kutambua kuwa si kila mtu amekamilika....

Huyu unaesema ana mapungufu kwenye kukuletea mahitaji, utashangaa kujua pengine ndie yupo vizuri katika majukumu pale tu atakapofundishwa namna ya kuyasimamia......

Vijana wa kileo especially wa mijini wamekuwa wakipewa mahitaji na wazazi, ndugu na jamaa. Kwa hivyo swala la wao kuhudumia ni swala geni na wanahitaji kufanyiwa training.

Kama kweli mnapendana na unamuhitaji hebu anza kumuintroduce katika kusimamia majukumu kwa kumjenga kidogokidogo uwe unamuelekeza akuletee mahitaji madogo madogo ya vitu vya gharama nafuu ambavyo unajua hatochukia kuagizwa kuvileta......na wewe jibidiishe kumpatia mahitaji yake binafsi na kidogo kidogo ataanza kuzoea na ataingia katika kuwajibika....

Usikate tamaa hata kidogo.....
 
Kuna jambo vijana wa leo huwa hamlifahamu na ndilo linawarudisha nyuma kila uchao kuhusu mahusiano.

Jambo lenyewe ni kuhusiana na kutambua kuwa si kila mtu amekamilika....

Huyu unaesema ana mapungufu kwenye kukuletea mahitaji, utashangaa kujua pengine ndie yupo vizuri katika majukumu pale tu atakapofundishwa namna ya kuyasimamia......

Vijana wa kileo especially wa mijini wamekuwa wakipewa mahitaji na wazazi, ndugu na jamaa. Kwa hivyo swala la wao kuhudumia ni swala geni na wanahitaji kufanyiwa training.

Kama kweli mnapendana na unamuhitaji hebu anza kumuintroduce katika kusimamia majukumu kwa kumjenga kidogokidogo uwe unamuelekeza akuletee mahitaji madogo madogo ya vitu vya gharama nafuu ambavyo unajua hatochukia kuagizwa kuvileta......na wewe jibidiishe kumpatia mahitaji yake binafsi na kidogo kidogo ataanza kuzoea na ataingia katika kuwajibika....

Usikate tamaa hata kidogo.....
Mkuu asante kwa ushauri ila hili lilishapita siku nyingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huijui hata unachokisema walah, I was talking about food! Anunue sabufa wapi ye mwenyewe sabufa.


Wewe mhehe ndio hujui unachokitaka..unampikia chakula akaf unataka aje na matunda kwenye getto lako...
Kwanza hana amani amini!!anawaza ukute kuna njemba nyingine huwa inaingia hapo getto huo mzuka wa kununua hata mtindi anauoata wapi..

Siku moja muombe ukampikie nyumbani kwake uone kama harudi na mkungu wa ndizi,mayai
 
Wewe mhehe ndio hujui unachokitaka..unampikia chakula akaf unataka aje na matunda kwenye getto lako...
Kwanza hana amani amini!!anawaza ukute kuna njemba nyingine huwa inaingia hapo getto huo mzuka wa kununua hata mtindi anauoata wapi..

Siku moja muombe ukampikie nyumbani kwake uone kama harudi na mkungu wa ndizi,mayai
Haha mimi sio mhehe bwana, anyway yalishapita mkuu
 
Back
Top Bottom