At your own risk

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2012
Posts
3,401
Reaction score
1,618
Hapa duniani hakuna mtu anayeishi maisha magumu kama yule aliyefiwa na mama yake mzazi.

Ni bora ya mtu asiye na pesa, atahangaika atatafuta na ipo siku atazipata hata kama ni uzeeni atapata tu lakini ukimpoteza mama ndio imetoka hiyo. Mama hautaweza kumtafuta, mama hana mbadala, mama ni mmoja tu, ukimkosa huyo uliyenae hutampata mama mwingine.

Mtu asiye na mama anakuwa kwenye wakati mgumu sana hasa nyakati za:
1. GRADUATION 2. HARUSI 3. MAFANIKIO 4. WAKATI WA SHIDA (Karibia nyakati zote tu kiukweli)

Katika hayo matukio ndio ambapo kila mtu anamkumbuka sana mama yake, utakapokuwa kwenye harusi unatamani mama yako angekuwepo, utakapokuwa kwenye graduation unawish mama yako angekuona unapomaliza chuo.

Mtu anapomzungumzia mama yake basi nawewe unatamani mama yako angekuwepo, mtu akipigiwa simu na mama yake unatamani mama yako angekuwepo labda angekupigia simu.

Mtu asiye na mama kila akikumbuka mama yake alipokuwa akimuita, akimfulia nguo, akimnyooshea nguo, akimuwekea chakula na kumfundisha mambo mengi ya kimaisha ataishia kulia tu.

Uchungu wa kumkosa mama hauna kifani wanajamiiforums, ukimkosa mama unaweza ukajiuliza unaishi ili iweje sasa?

POLENI WOTE MLIOFIWA NA MAMA ZENU PIA NISAMEHENI KWA KUWAKUMBUSHA MACHUNGU NA KUWATOA MACHOZI.

Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)
 
Ni kweli kabisa,ni uchungu usio na kifani. Mama yangu ni mwaka mmoja na miezi kadhaa ulipotuacha kwa ghafla uchungu ninaousikia hauna maelezo yoyote! Mpaka leo kuna vitu huwa nawaza nitamwambia mama yangu ndio atakaenielewa , baadae nakumbuka kuwa hatunae tena,ila kwa uhakika kiroho bado niko nae!
 
Umesema kweli maana inauma sana yani sana tu kutokuwa na mzazi wako
 
Daaah poleni wote mliofiwa na Mama....real fact
 
Ni kweli kabisa,aliniacha nikiwa nimemaliza tu highschool,namkumbuka sana,na bado siamini kama naota vile!
 
namkumbuka mama yangu Mwenyezi Mungu amuweke mahala pema pepuni
 
Daaah poleni wote mliofiwa na Mama....real fact

Mama yangu alifariki miaka 2 baada ya kuanza kazi. Huwa natamani angekuwepo maana hakuwahi kufaidi matunda ya kazi yangu
 
Sina budi kusema huu uzi umenigusa 100% na umenifanya niwaze mpaka basi....
 
It pains sana kumkosa mama,usiombe kuondokewa na mm machungu yake hayaelezeki,miss you mamy,pumzika kwa amani.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…