Chief Kabikula
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 7,567
- 9,026
Askofu mkuu wa kanisa la kkkt dayosisi ya kaskazini mashariki amesema kuwa watanzania hatuwezi Kufungwa midomo ya kutetea haki za binadamu, demokrasia na utawala bora, kisa kuna mtu anasema analeta maendeleo. Ameyasema hayo katika sherehe za kutimiza miaka ishirini ya kituo cha sheria na haki za binadamu nchini. Ambapo ripoti ya hali ya haki za binadamu nchini ilijadiliwa. Bila woga wala kupepesa macho askofu Munga katoa maoni yake hayo ili hali hivi sasa viongozi wengi wa dini wamefunga midomo yao. Napenda nimpongeze baba askofu kwa kusimamia ukweli, Mungu ambariki sana.