Askofu Pengo: Sikufahamu kuhusu waraka wa Kwaresma wa Baraza la Maaskofu Katoliki. Awaasa wasichanganye dini na siasa

Mkuu niah, huyu kiongozi wa sasa kajikita kwenye shida za kiuchumi, haya maneno eti tunakoelekea ni kubaya yanasikika humu mijini tena mitandaoni tu, mbona huko Kagera, Mbeya, Shinyanga na Pemba hatusikii maneno kama haya yanayosikika yakisemwa na wanaharakati?.

Wanaosema demokrasia imebanwa ni watu wa mijini wenye simu za viganjani na wenye akaunti za twitter, facebook na wenye uwezo wa kununua magazeti kama newsweek na mengine, wale wa vijijini ambao ndio wengi akili zao zipo kwenye utatuzi wa shida zao.

Wanaharakati bado wanayo ile superiority complex, yaani mawazo yao ndio yenye kuwakilisha mustakabili wa wengi, kiburi ambacho jaji Warioba aliwahi kukiongelea, wanadhani kuwa wale watu wa vijijini hawana uwezo wa kiakili wala hawana hekima ya kutambua lipi zuri na lipi baya.
Vipi samaki unapata hapo sokoni Kemondo? Sasa hivi watu watakuwa na utapia mlo wa kuzidi.
 
Vipi samaki unapata hapo sokoni Kemondo? Sasa hivi watu watakuwa na utapia mlo wa kuzidi.
Am not a politician but I speak my my mind na nimeona tangu Jakaya samaki walianza kudhibitiwa ila sasa it is too much. Maskini apate wapi protein?
 
Kwa nukuu isiyo rasmi: siku mmoja Yohana mbatizaji alikuwa akihubiri wakamfuata maaskari wakamuuliza na sisi tufanye nn tuone ufalme wa mbinguni? Yohana akawajibu "msimsingizie mtu uwongo toshekini na mishara yenu" watoza ushuru wakamuuliza na sisi Je? "msikusanya zaidi ya mliyoamriwa"...ukiangalia hiyo nukuu isiyo rasmi niliyoitoa ya Yohana utaona anatoa mwongozo kwa watendaji wa serikali, ivyo ivyo kanisa inapoona haki za raia zilizowazi kabisa zilizo ndani ya katiba zinakiukwa, lazima iwakumbushe watendaji wa serikali kuwa tendeni kadri ya sheria na katiba ya nchi ili waone ufalme wa mbingu
 
Sijawahi kuona askofu wa kipuuzi hapa ulimwenguni kama askofu mapengo. Hivi atastaafu lini au Kardinali ni kama Papa, ni hadi afie kitini? Inasikitisha sana kuwa na maaskofu wachumia tumbo kama huyu bwana mapengo.
 
Hivi kati ya maaskofu wote walioandaa waraka ule Pengo ana akili kubwa kuwazidi? Huyu babu anatia huruma sana. Wakati umefika sasa arudi kwao Sumbawanga akalee wajukuu.
 
Asee hii post yako imefanya nikumbuke ile clip ya baba askofu Gwajima ,nadhan ilihusu kuuliza sijui amekula maharage ya wapi, sasa may be kala maharage ya chattle

Umeandika kitu kibaya mno...shauri yako.huyo ni mtu wa dini...anasema maoni yake...sasa wewe unamtukana ...shauri yako...I mean it...
 
Wale wenye akili ya yule mnyama povu linawatoka. Kadinali Pengo yuko sahihi kabisa.

Hao Maaskofu wenu wenye njaa kama haki ya kujieleza imeminywa mbona yeye kajieleza?

Hongera Pengo na hongera Mr President JPM kaza uzi. Maaskofu wamesema na kazi na shughuli pevu inaendelea wale jamaa wakae pale mwezi
 
Katika hali ya kushangaza Askofu wa jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Kadinali Polycap Pengo amesema hakuwa anajua kama kuna waraka utatolewa kuhusu kwaresma na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania huku akisema waraka huo una mazuri mengi japo umechanganya dini na siasa.

Namnukuu

"Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazunguzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-

Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji...mimi nimeipokea baadhi yenu mmeshaipokea. Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu...naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.

Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa. Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.

Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi. Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa? Itakuwa namsaliti hata yule aliyenipa wito huu. Tuchambue yale yanayohusu imani yetu katika ule waraka. Yale ambayo moja kwa moja yanahusu imani yetu Katoliki na tuyashike tuyazingatie kwa dhati kabisa.

Lakini yale ya kuanza kusema Serikali ya awamu ya 5 inagandamiza uhuru inafanya nini...wewe Askofu uhuru wa kisiasa umeujua wapi? Umeujuaje? Na mambo ya ndani ya kisiasa huyajui na bado uje kutamka...nadhani tumeelewana.

Yapo yaliyo mema mazuri kabisa katika waraka ule ingawaje sikujuia kama yameandikwa lakini siwezi kukataa yaliyo mema kwa sababu sikujua. Yanaendelea kuwa mema mpaka kesho na keshokutwa. Lakini yale ambayo yanachanganya Dini na Siasa hayo siwezi kuyakubali. Nyerere alifanya indoctrination kubwa mno kwa watu wa umri wetu. Mtu huwezi ukathubutu na ukalala salama usiku. Watu wa umri wangu ukichanganya dini na siasa utaota vitu vya ajabu utakosa usingizi(vicheko)

Sasa ninyi vijana ninalotaka ni hili, kwamba na ninyi mkichanganya dini na siasa muote vitu vibaya kama hivyo..muote vitu vibaya kabisa hata muone mnachungulia kaburi katika ndoto. Sisi sio wanasiasa, tunahitaji wanasiasa mtuendelee wale tunaokuwa wito huo. Wale tunaotaka kuwa mama wakuu, mababa padri, maaskofu. Fuateni wito kulingana na misimamo yake ya kiimani.

Mwisho wa Kunukuu

Ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana huku akihoji maaskofu wamejuaje kama haki na demokrasia inaminywa wakati hiyo sio kazi yao?

Pengo amekuwa akionyesha mapenzi yake waziwazi Kwa Chama cha Mapinduzi kiasi kwamba amekuwa akikingia kifua kila anapoulizwa kuhusu Serikali au anapoizungimzia Serikali huku akisema hawezi kumlazimisha mtu kuwa kama yeye kwa kuwa kila mtu ana upande wake anaouona unamfaa.



Chanzo: Radio Tumaini

Soma: WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Kardinali kapiga U turn alikuwa na misimamo mizuri sana kuhusu hizi nyaraka za maaskofu na aliziita maoni ya kimungu.
Kardinali Pengo: Wanasiasa waacheni Maaskofu wafanye kazi zao, msiwafundishe kazi
 
Katika hali ya kushangaza Askofu wa jimbo la Dar es Salaam, Mwadhama Kadinali Polycap Pengo amesema hakuwa anajua kama kuna waraka utatolewa kuhusu kwaresma na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania huku akisema waraka huo una mazuri mengi japo umechanganya dini na siasa.

Namnukuu

"Katika wiki chache zilizopita watu wamekuja kwangu wakaniuliza unaionaje ile barua ya Maaskofu kuhusu Kwaresma mwaka huu? Ninazunguzia hilo na wala mtu asiende aka-quote kitu kingine ndio maana nataka kusema wazi kabisa:-

Barua ile ijapokuwa hata jina langu mnaliona limeandikwa pale kwamba na mimi ni mmoja wa waandishi au watamkaji...mimi nimeipokea baadhi yenu mmeshaipokea. Kwahiyo sioni namna gani mimi naweza kuwa mwandishi au mhubiri kwenu wa ile barua ambayo imetungwa labda na maaskofu...naamini na baadhi ya maaskofu lakini mimi mwenyewe hata nilikuwa sijaiona, hata nilikuwa sijaambiwa kuna kitu cha namna hiyo kinakuja.

Tuelewane vizuri, ninaposema hivi sitaki kusema ile barua ni mbaya. Moja tu ni kwamba barua nzima imechanganya vitu viwili; Mwalimu angekuwepo angepiga kelele Maaskofu msichanganye Dini na Siasa. Angepiga kelele sana kuhusu waraka huu katika nyakati zake. Na hilo nawambia sina hofu, muende mkamwambie mtu yeyote nimesema hivi. Ndio wala msione aibu, najua labda hata wengine mmekunja nyuso, kunjeni tu lakini huo ndio msimamo wangu.

Zipo sehemu katika waraka huo zinazochanganya Dini na Siasa na si kazi ya maaskofu ni kazi yenu wanasiasa mkiwa ni wa CHADEMA, mkiwa ni wa CCM lakini haiwezi kuwa kazi yangu mimi. Siwezi kwanza nikaanza kuchambua na ku-criticize Serikali katika mambo yaliyo yake; sikupewa mamlaka hayo. Na kwanini niwe padri mpaka nikubali kuwa Askofu na huku kumbe wito wangu ni siasa? Itakuwa namsaliti hata yule aliyenipa wito huu. Tuchambue yale yanayohusu imani yetu katika ule waraka. Yale ambayo moja kwa moja yanahusu imani yetu Katoliki na tuyashike tuyazingatie kwa dhati kabisa.

Lakini yale ya kuanza kusema Serikali ya awamu ya 5 inagandamiza uhuru inafanya nini...wewe Askofu uhuru wa kisiasa umeujua wapi? Umeujuaje? Na mambo ya ndani ya kisiasa huyajui na bado uje kutamka...nadhani tumeelewana.

Yapo yaliyo mema mazuri kabisa katika waraka ule ingawaje sikujuia kama yameandikwa lakini siwezi kukataa yaliyo mema kwa sababu sikujua. Yanaendelea kuwa mema mpaka kesho na keshokutwa. Lakini yale ambayo yanachanganya Dini na Siasa hayo siwezi kuyakubali. Nyerere alifanya indoctrination kubwa mno kwa watu wa umri wetu. Mtu huwezi ukathubutu na ukalala salama usiku. Watu wa umri wangu ukichanganya dini na siasa utaota vitu vya ajabu utakosa usingizi(vicheko)

Sasa ninyi vijana ninalotaka ni hili, kwamba na ninyi mkichanganya dini na siasa muote vitu vibaya kama hivyo..muote vitu vibaya kabisa hata muone mnachungulia kaburi katika ndoto. Sisi sio wanasiasa, tunahitaji wanasiasa mtuendelee wale tunaokuwa wito huo. Wale tunaotaka kuwa mama wakuu, mababa padri, maaskofu. Fuateni wito kulingana na misimamo yake ya kiimani.

Mwisho wa Kunukuu

Ameyasema hayo wakati akiadhimisha ibada ya Jumapili ya matawi huko Bagamoyo katika tamasha la vijana huku akihoji maaskofu wamejuaje kama haki na demokrasia inaminywa wakati hiyo sio kazi yao?

Pengo amekuwa akionyesha mapenzi yake waziwazi Kwa Chama cha Mapinduzi kiasi kwamba amekuwa akikingia kifua kila anapoulizwa kuhusu Serikali au anapoizungimzia Serikali huku akisema hawezi kumlazimisha mtu kuwa kama yeye kwa kuwa kila mtu ana upande wake anaouona unamfaa.



Chanzo: Radio Tumaini

Soma: WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

naziona busara katka kauli ya Cardinal Pengo! pilipili zilizo shamba zakuwashani?...kitanda usichokilalia wawajuaje kunguniwe? Maaskofu, lini mmezuiwa kuhutubu, kuhubiri injili ya Kristo? you are out of line this time!
 
Hivi hakuna kigezo maalumu cha kumstaafisha Askofu?huyu mzee amepitisha muda wake
 
Anaogopa ESCROW jamani.Hapo ndio shida ya kuchanganya pesa na Mambo yankiroho.Pole Kadinal your hands are tied
 
Pengo kama binadamu anaweza kuwa na tatizo lakini matatizo yako ni makubwa zaidi ya Matatizo ya Pengo.

Kumlinganisha Pengo na Gwajima ni kulitukana Kanisa la Roman Catholic.

Kumbuka ni wengi wanapenda kuwa katika wadhifa wa Pengo lakini uwezo wake umemfikisha hapo alipo. Tunaokufahamu wewe hata uchungaji ulikushinda!

Pengo kueleza maoni yake amekuwa hafai na mpuuzi! Ninyi mnaopiga kelele kuhusu uhuru wa kujieleza lakini kinachoshangaza hamtaki wengine wajieleze. Huu ni zaidi ya udikteta. Mkipewa fursa mtakuwa zaidi ya madikteta.

Pengo hajawahi kutaka kujiua kwa sababu ya kukosana na wazazi wake! Wewe ulitenda. Kwa mantiki hii, matatizo yako ni makubwa zaidi ya Pengo.

Nguruwe wewe, Nilikuwa na Miaka 11 1984, Nilikosea Kwa Utundu Tu kwa Baba Kunituma Dukani asubuhi muda wa shule nikakataa, Akatamka Laana, Nilichokuwa Nikisema Ni Kuwa Ukitamka laana Kwa Mtoto Unafuungua Mlango Kwa Shetani Kumdhuru. Wala Sijawahi Kugombana na Baba yangu Mtoto wa Miaka 11 anawezaje kuwa na Ugomvi na Baba yake. Na baada ya Tukio Hilo Aliyenipeleka Hospitalini Na Kukaa na Mimi siku Tatu Mpaka Nilipozinduka kwenye Coma ni Baba na Alinibariki. Wewe Ibilisi, Muuza Damu za Ndugu, Umeoza Moyo Kama Mzoga wa Nguruwe! Wewe Ni Tapeli, Unajifichia Jina Bandia Kuongea Usiyoyajua. Mimi Naitwa Thobias L. Marandu, Wewe Malaya kama Ni Jasiri na Msema Ukweli Nitajie Jina Lako, Wewe na Yuda Iskariot Ni Sawa! Mimi Ni Mkweli Kama Sufi, anayetaka Kujua Ukweli wangu na Niliyosema na Uwongo wako anaweza Kutafuta Kitabu changu. IT IS NOT TOO LATE YET, By TL. Marandu. Wewe Unayejifanya Msemaji Ukweli Huku Kila Nitajie Jina Lako hapa. Nguruwe Mchafu, Ulisema, "UKIMFANANISHA GWAJIMA NA PENGO NI KUDHALILISHA UKATOLIKI" Na wewe Ukijiita MKRISTO NI MATUSI NA KUIKANYAGA DAMU YA YESU. Unajisikiaje Ulivyofanya Ulivyorusha Hela za Mwal/Mwinjilisti J.K Mpaka Anakufa na Kuzikwa hata Mazishi Hukwenda!
 
Je, Ina maana Na yeye siyo Askofu??

Aende akawashtaki walioandika jina lake na siyo kukana madhabahuni. Kwani naye amechanganya dini Na siasa.

Hata Yesu Na Yohane Mbatizaji walikemea viongozi wa siasa walipofanya ndivyo sivyo.

Je Askofu Pengo Ni zaidi ya Yesu au Yohane Mbatizaji???

SIPATI PICHA!!!!!
 
kwa mtazamo huu pengo kalikosea kanisa na maaskofu wenzake. hivi hawa maaskofu na viongozi wengine wa dini walivyowakataza chadema kushughulika na UKUTA hawakuingilia siasa?
 
Nguruwe wewe, Nilikuwa na Miaka 11 1984, Nilikosea Kwa Utundu Tu kwa Baba Kunituma Dukani asubuhi muda wa shule nikakataa, Akatamka Laana, Nilichokuwa Nikisema Ni Kuwa Ukitamka laana Kwa Mtoto Unafuungua Mlango Kwa Shetani Kumdhuru. Wala Sijawahi Kugombana na Baba yangu Mtoto wa Miaka 11 anawezaje kuwa na Ugomvi na Baba yake. Na baada ya Tukio Hilo Aliyenipeleka Hospitalini Na Kukaa na Mimi siku Tatu Mpaka Nilipozinduka kwenye Coma ni Baba na Alinibariki. Wewe Ibilisi, Muuza Damu za Ndugu, Umeoza Moyo Kama Mzoga wa Nguruwe! Wewe Ni Tapeli, Unajifichia Jina Bandia Kuongea Usiyoyajua. Mimi Naitwa Thobias L. Marandu, Wewe Malaya kama Ni Jasiri na Msema Ukweli Nitajie Jina Lako, Wewe na Yuda Iskariot Ni Sawa! Mimi Ni Mkweli Kama Sufi, anayetaka Kujua Ukweli wangu na Niliyosema na Uwongo wako anaweza Kutafuta Kitabu changu. IT IS NOT TOO LATE YET, By TL. Marandu. Wewe Unayejifanya Msemaji Ukweli Huku Kila Nitajie Jina Lako hapa. Nguruwe Mchafu, Ulisema, "UKIMFANANISHA GWAJIMA NA PENGO NI KUDHALILISHA UKATOLIKI" Na wewe Ukijiita MKRISTO NI MATUSI NA KUIKANYAGA DAMU YA YESU. Unajisikiaje Ulivyofanya Ulivyorusha Hela za Mwal/Mwinjilisti J.K Mpaka Anakufa na Kuzikwa hata Mazishi Hukwenda!
Inaonyesha nyie mnafahamiana.

Je Ni kwanini msipeane maneno mazito hayo huko mtaani mlipo kuliko kuja kujidharirisha hapa??

Inaonyesha wote mna Kasoro ktk medula oblongata zenu. Nendeni Muhimbili mkapimwe Na muanze dose mapema.
 
Back
Top Bottom