Askofu Mihali Wakatoliki waliosimamia uchaguzi na kufanya Udanganyifu wakafanye kitubio

Askofu Mihali Wakatoliki waliosimamia uchaguzi na kufanya Udanganyifu wakafanye kitubio

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
780
Reaction score
1,831
Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Romanus Mihali, amewataka Wakristo, hususan waumini wa Kanisa Katoliki, kutimiza wajibu wao wa kusimamia haki, amani na uadilifu, hasa katika masuala ya uchaguzi, wakisisitiza kuwa kutotenda haki ni dhambi kubwa.

Askofu Mihali alitoa wito huo wakati wa homilia ya Misa ya Sikukuu ya Krismasi (Noeli) iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Kihesa, jimboni Iringa.
Akizungumza na waumini, Askofu Mihali alisema Mkristo Mkatoliki amepewa dhamana ya kusimamia taratibu za uchaguzi kwa haki na kwa kuzingatia dhamiri safi, bila kuyumbishwa na shinikizo au maelekezo yanayokiuka misingi ya haki.

“Wewe Mkristo Mkatoliki umepewa wajibu wa kusimamia uchaguzi. Je, unasimamia uchaguzi vizuri? Ukielekezwa kufanya kinyume cha haki, unapaswa kusimama imara kama Mkristo na kusema hili si la haki, sitafanya,” alisema Askofu Mihali.

Aliongeza kuwa Mkristo anayeshiriki au kunyamazia vitendo vya udhalilishaji wa haki anapaswa kutambua kuwa anafanya dhambi, akisisitiza kuwa kuchezea dhamiri za watu bila kutubu ni kosa kubwa mbele ya Mungu.

Katika ujumbe wake wa Krismasi, Askofu Mihali aliwakumbusha waumini kuwa maadhimisho ya Noeli yanapaswa kwenda sambamba na kuishi maisha ya haki, unyenyekevu na amani, kama kielelezo cha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Chanzo na SAUTDIGITAL
 
Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Romanus Mihali, amewataka Wakristo, hususan waumini wa Kanisa Katoliki, kutimiza wajibu wao wa kusimamia haki, amani na uadilifu, hasa katika masuala ya uchaguzi, wakisisitiza kuwa kutotenda haki ni dhambi kubwa.

Askofu Mihali alitoa wito huo wakati wa homilia ya Misa ya Sikukuu ya Krismasi (Noeli) iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Kihesa, jimboni Iringa.
Akizungumza na waumini, Askofu Mihali alisema Mkristo Mkatoliki amepewa dhamana ya kusimamia taratibu za uchaguzi kwa haki na kwa kuzingatia dhamiri safi, bila kuyumbishwa na shinikizo au maelekezo yanayokiuka misingi ya haki.

“Wewe Mkristo Mkatoliki umepewa wajibu wa kusimamia uchaguzi. Je, unasimamia uchaguzi vizuri? Ukielekezwa kufanya kinyume cha haki, unapaswa kusimama imara kama Mkristo na kusema hili si la haki, sitafanya,” alisema Askofu Mihali.

Aliongeza kuwa Mkristo anayeshiriki au kunyamazia vitendo vya udhalilishaji wa haki anapaswa kutambua kuwa anafanya dhambi, akisisitiza kuwa kuchezea dhamiri za watu bila kutubu ni kosa kubwa mbele ya Mungu.

Katika ujumbe wake wa Krismasi, Askofu Mihali aliwakumbusha waumini kuwa maadhimisho ya Noeli yanapaswa kwenda sambamba na kuishi maisha ya haki, unyenyekevu na amani, kama kielelezo cha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Chanzo na SAUTDIGITAL
Hajaongelea mapadri ambao wamezaa watoto kwa siri,wao hawatakiwi kutubu?
 
Hajaongelea mapadri ambao wamezaa watoto kwa siri,wao hawatakiwi kutubu?
Umezalishwa na padre unalia lia mtandaoni askofu akusemee?

Kama amekuzalisha akakukacha siyo haki kaidai haki yako mahakamani ndivyo imani inavyotaka huyo askofu hawezi zungumza kitu hakijui kama wewe unajua hayo yapo kuwa mjumbe wake.
 
Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Romanus Mihali, amewataka Wakristo, hususan waumini wa Kanisa Katoliki, kutimiza wajibu wao wa kusimamia haki, amani na uadilifu, hasa katika masuala ya uchaguzi, wakisisitiza kuwa kutotenda haki ni dhambi kubwa.

Askofu Mihali alitoa wito huo wakati wa homilia ya Misa ya Sikukuu ya Krismasi (Noeli) iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Kihesa, jimboni Iringa.
Akizungumza na waumini, Askofu Mihali alisema Mkristo Mkatoliki amepewa dhamana ya kusimamia taratibu za uchaguzi kwa haki na kwa kuzingatia dhamiri safi, bila kuyumbishwa na shinikizo au maelekezo yanayokiuka misingi ya haki.

“Wewe Mkristo Mkatoliki umepewa wajibu wa kusimamia uchaguzi. Je, unasimamia uchaguzi vizuri? Ukielekezwa kufanya kinyume cha haki, unapaswa kusimama imara kama Mkristo na kusema hili si la haki, sitafanya,” alisema Askofu Mihali.

Aliongeza kuwa Mkristo anayeshiriki au kunyamazia vitendo vya udhalilishaji wa haki anapaswa kutambua kuwa anafanya dhambi, akisisitiza kuwa kuchezea dhamiri za watu bila kutubu ni kosa kubwa mbele ya Mungu.

Katika ujumbe wake wa Krismasi, Askofu Mihali aliwakumbusha waumini kuwa maadhimisho ya Noeli yanapaswa kwenda sambamba na kuishi maisha ya haki, unyenyekevu na amani, kama kielelezo cha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Chanzo na SAUTDIGITAL
Hehehe Kama ni Mwanaccm asahau
 
Jamaa wanajiona Wana nguvu sana kwa waumini wao,yaani kama malaika wa Mungu, yaani wanaamini waumini wanawaamini sana
 
Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Romanus Mihali, amewataka Wakristo, hususan waumini wa Kanisa Katoliki, kutimiza wajibu wao wa kusimamia haki, amani na uadilifu, hasa katika masuala ya uchaguzi, wakisisitiza kuwa kutotenda haki ni dhambi kubwa.

Askofu Mihali alitoa wito huo wakati wa homilia ya Misa ya Sikukuu ya Krismasi (Noeli) iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Kihesa, jimboni Iringa.
Akizungumza na waumini, Askofu Mihali alisema Mkristo Mkatoliki amepewa dhamana ya kusimamia taratibu za uchaguzi kwa haki na kwa kuzingatia dhamiri safi, bila kuyumbishwa na shinikizo au maelekezo yanayokiuka misingi ya haki.

“Wewe Mkristo Mkatoliki umepewa wajibu wa kusimamia uchaguzi. Je, unasimamia uchaguzi vizuri? Ukielekezwa kufanya kinyume cha haki, unapaswa kusimama imara kama Mkristo na kusema hili si la haki, sitafanya,” alisema Askofu Mihali.

Aliongeza kuwa Mkristo anayeshiriki au kunyamazia vitendo vya udhalilishaji wa haki anapaswa kutambua kuwa anafanya dhambi, akisisitiza kuwa kuchezea dhamiri za watu bila kutubu ni kosa kubwa mbele ya Mungu.

Katika ujumbe wake wa Krismasi, Askofu Mihali aliwakumbusha waumini kuwa maadhimisho ya Noeli yanapaswa kwenda sambamba na kuishi maisha ya haki, unyenyekevu na amani, kama kielelezo cha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Chanzo na SAUTDIGITAL
Ameongea jambo jema sana
 
Ni sahihi kabisa. Mkristo yeyote akiambiwa na yeyote kutenda jambo lolote lililo kinyume na mapenzi ya Mungu anatakiwa kukataa, kama neno la Mungu lisemavyo, 'yakupasa kumtii Mungu kuliko mwanadamu'
 
Cheo cha uaskofu kimepoteza thamani yake. Maaskofu wa katoliki ni makanjanja kanjanja sana, nayo yanahitaji yatubu.

Tanzania ina Askofu mmoja tu kwa Jina la Malasusa na Mzee pengo
 
Back
Top Bottom