Askofu Kinyaiya ahadharisha wasiokwenda Kanisani hadi waletwe ndani ya jeneza

Automata

JF-Expert Member
Mar 3, 2015
3,347
4,614
Cl0GVSHXIAApGuN.jpg

Baba Askofu Mhashamu Beatus Kinyaiya, O.F.M. Cap.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma, Mhashamu Beatus Kinyaiya, amewataka Wakatoliki kuhakikisha wanadumu katika sala na kwenda Kanisani na siyo kusubiri waletwe Kanisani wakiwa ndani ya jeneza.

Askofu Mkuu Kinyaiya aliyasema hayo hivi karibuni kwenye Ibada ya Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Peter Clavery, Mbezi Louis Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salaam.

Mjitahidi kwenda Kanisani kusali na ninyi waimarishwa yale mliokubaliana na Mwenyezi Mungu, mkayafanyie kazi siku zote za maisha yenu”, alisema Askofu Kinyaiya na kuongezea, “Hii isiwe ndiyo mwisho wenu wa kufika Kanisani baada ya kupokea Sakramenti ya Kipaimara…bali endeleeni kuja Kanisani kwa Ibada na Sakramenti mbalimbali, msisubiri mletwe Kanisani mkiwa ndani ya jeneza”, mwisho wa kunukuu.

Askofu Kinyaiya alisema kuwa vijana hao wanatakiwa kutambua kuwa wao kwa sasa ni mabalozi katika familia zao, kwa kuwaamsha wazazi na walezi wao kwenda Kanisani na kushiriki Jumuiya ili kuondoa hali ya ubaya ndani ya familia zao.


Source: Tumaini Letu
 
Mchungaji/padri au askofu ni wajibu wake kusisitiza watu waende kanisani, sababu ni kwamba wasipoenda hana kazi na hawezi kula wala kunywa.

Watu husisitizwa ili waende kanisani maana yake mwisho lazima watoe sadaka ambayo ndio roho ya kanisa au makanisa, bila sadaka hayo mambo hayapo.

Sio kwamba wanasisitiza kwa kua wanapenda watu, hapana, wanatetea matumbo yao na kazi zao.
 
Mchungaji/padri au askofu ni wajibu wake kusisitiza watu waende kanisani, sababu ni kwamba wasipoenda hana kazi na hawezi kula wala kunywa.

Watu husisitizwa ili waende kanisani maana yake mwisho lazima watoe sadaka ambayo ndio roho ya kanisa au makanisa, bila sadaka hayo mambo hayapo.

Sio kwamba wanasisitiza kwa kua wanapenda watu, hapana, wanatetea matumbo yao na kazi zao.
Mawazo potofu
 
Tatizo siyo kwenda kanisani mbali ni kuyaishi matendo mema ya Kristo, siyo kama mkuu wa nchi ya viwanda anaenda kanisani na matokeo yake anaratibu mipango ya kuondoa watu duniani kwa chuki zake, ni bora usienda kanisani kuliko kwenda alafu unamdhihaki Mungu.
 
Tatizo siyo kwenda kanisani mbali ni kuyaishi matendo mema ya Kristo, siyo kama mkuu wa nchi ya viwanda anaenda kanisani na matokeo yake anaratibu mipango ya kuondoa watu duniani kwa chuki zake, ni bora usienda kanisani kuliko kwenda alafu unamdhihaki Mungu.
Watu hawajui tu.....bora uwe wa moto au wa baridi....kuliko kua katikati jambo ambalo Mungu analichukia mno
 
Mchungaji/padri au askofu ni wajibu wake kusisitiza watu waende kanisani, sababu ni kwamba wasipoenda hana kazi na hawezi kula wala kunywa.

Watu husisitizwa ili waende kanisani maana yake mwisho lazima watoe sadaka ambayo ndio roho ya kanisa au makanisa, bila sadaka hayo mambo hayapo.

Sio kwamba wanasisitiza kwa kua wanapenda watu, hapana, wanatetea matumbo yao na kazi zao.
Biblia imesema mkikutana ma mimi nipo kati yenu, sasa hapo kuna ulazima gani wa kwenda kanisani?
 
Maaskofu wengi hasa Kanisa katoliki bado mmelala, hamtembelei parokia zenu mpaka siku ya Kipaimara tu. Kama mnataka kufufua ari ya waumini wenu tembeleeni parokia, kutaneni na waumini wenu mara kwa mara. ongeeni na kamati za walei, tembeleeni jumuiya. Maaskofu mmelala, hivyo maparoko na wasaidizi wao nao wamelala na waumini wamelala.

Mwezi huu wa Rozari, fanyeni suprise visits kwenye parokia, kwenye vigango na kusali na jumuiya. wekeni semina za mara kwa mara kila wiki parokia zote kufundisha hasa vizazi vipya ama waumini wapya juu ya hostoria ya kanisa, mfumo wa liturujia ya kanisa katoliki, maana ya ibadA MBALI MBALI, sacrament na pia mfundishe Biblia kwa kutumia Bibilia ambayo haijapotoshwa.
 
Hivi nikienda kanisani ili kujionesha tu lakini roho mbaya ya kishetani inanisonga kuna faida gani hapo?? Angehubiri zaidi kuhusu hofu ya dhambi kwa wanaosema wao ni wakristo huku wamevaa roho ya kishetani. Tumeona hata wengine wakilia kwa uchungu huku wakienda kuteka nyara kwa silaha
 
Huwa najiuliza; kwanini wakatoliki wanatoa kipaumbele Kwa kifo, tena Kwa kukosa kuombewa marehemu badala ya kuwasisitiza walio hao kuacha roho na mambo ya kishetani?
 
If you dont go to church vertically, one day you will be sent horizontally ...May Almighty God lead us in righteousness way!
 
Acha watu waruke debe, wanywe pombe,waibe wakifa kuna pagatori, ndugu watatoa hela wataombewa wataenda mbinguni....


ROMAN RAHA SANA, HATA UKIFA UNAZINI ,KUNA PAGATORE
 
Maaskofu wengi hasa Kanisa katoliki bado mmelala, hamtembelei parokia zenu mpaka siku ya Kipaimara tu. Kama mnataka kufufua ari ya waumini wenu tembeleeni parokia, kutaneni na waumini wenu mara kwa mara. ongeeni na kamati za walei, tembeleeni jumuiya. Maaskofu mmelala, hivyo maparoko na wasaidizi wao nao wamelala na waumini wamelala.

Mwezi huu wa Rozari, fanyeni suprise visits kwenye parokia, kwenye vigango na kusali na jumuiya. wekeni semina za mara kwa mara kila wiki parokia zote kufundisha hasa vizazi vipya ama waumini wapya juu ya hostoria ya kanisa, mfumo wa liturujia ya kanisa katoliki, maana ya ibadA MBALI MBALI, sacrament na pia mfundishe Biblia kwa kutumia Bibilia ambayo haijapotoshwa.
Haina haja ya yote hayo, waumin walishaambiwa kuna toharani, ukifa na mazambi, au ukifia kwenye kifua cha malaya, kama una hela ndugu zako watalipia, unaombewa unatoka pagatori unaenda mbinguni, SASA KWANINI WATU WAHANGAIKE KWENDA KANISANI WAKATI KUNA SHORTCUT tu
 
AROON
Nenda nyuma yangu shetani wee
Na ukae mbali na thread yangu

Nishakataza kejeli na matusi
 
Back
Top Bottom