Askofu Kasala awataka Watanzania kusimamia ukweli, haki

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Askofu Flavian Kasala amewataka Watanzania kusimamia ukweli na haki katika kumuenzi Rais wa awamu ya tano, hayati John Magufuli.

Askofu Kasala ametoa rai hiyo leo Alhamisi Machi 17, 2022 kwenye ibada ya misa ya kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati John Magufuli inayofanyika katika uwanja wa Magufuli Chato.

Amesema Hayati Magufuli alisimamia ukweli na kile anachokiamini, hivyo kuwataka wananchi na viongozi kushuhudia ukweli huo katika maisha yao.

“Tukisimamia ukweli na haki, marehemu wetu wanazo dhawabu walizoondoka nazo, tuko tayari kuyachukua hayo kuwa kama dira ya maisha yetu?” amesema na kuongeza:

“Njaa ya haki ni pale katika ubinadamu wako unaposema siwezi kushuhudia kuona mtu akiwa anaonewa, ananyanyaswa na kudhulumiwa.

“Maudhi kwa ajili ya haki yanakuja pale tu mmoja anaposimamia haki bila kijibakiza na kusimamia haki ni kujitoa sadaka lakini bora niudhiwe lakini haki itendeke,” amesema Askofu Kasala.

Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 kwa maradhi ya moyo katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu, mwili wake ulizikwa Ijumaa Machi 26, 2021 katika kijiji cha Mlimani wilayani Chato Mkoa wa Geita katika makaburi ya familia.

Chanzo: Mwananchi

Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Askofu Flavian Kasala.jpg
 
Ukweli na kutenda haki ndio vilifanya tumpende Magufuli.

Alikuwa akisema atafanya ujue kitafanyika kweli na akisema hafanyi sahau, ndio imetoka.

Alikuwa ni mwanasiasa wa tofauti sana. Hakuamini katika siasa za ulaghai na ku-sugarcoat.

Apumzike kwa amani mbinguni.
 
Huyu ndie askofu anaesimamia ukweli halisi bila kuwa na upande!
Ndio maana akaalikwa yeye kuja kuisimamia shughuli hii muhimu.

Achana na wale waomba misamaha ya kodi kina Niwemugizi.

Huyu anaongea na unaoiona karama ya Mungu ndani yake!
View attachment 2154023
 
Ukweli na kutenda haki ndio vilifanya tumpende Magufuli.

Alikuwa akisema atafanya ujue kitafanyika kweli na akisema hafanyi sahau, ndio imetoka.

Alikuwa ni mwanasiasa wa tofauti sana. Hakuamini katika siasa za ulaghai na ku-sugarcoat.

Apumzike kwa amani mbinguni.
Alisisitiza sana kuhusu amani na utulivu lakini si haki
 
Ni kosa kumsemea mabaya marehemu, pia ni kosa kumtwika mambo mazuri rukuki ambayo hakutenda, kwa uhalisia Magufuli kwenye haki alikuwa ameferi kabisaa alikuwa amejikita kwenye kudhulumu zaidi.

Mfano ni kwa alichomfanyia Tundulisu na alichokuwa anawafanyia wapinzani wake, pamoja na mambo aliyokuwa anayafanya kwenye chaguzi.
 
Ni kosa kumsemea mabaya marehemu, pia ni kosa kumtwika mambo mazuri rukuki ambayo hakutenda, kwa uhalisia Magufuli kwenye haki alikuwa ameferi kabisaa alikuwa amejikita kwenye kudhulumu zaidi.

Mfano ni kwa alichomfanyia Tundulisu na alichokuwa anawafanyia wapinzani wake, pamoja na mambo aliyokuwa anayafanya kwenye chaguzi.

Kwa hiyo hapo kwenye haki Askofu wenu amechapia?
 
Ukweli na kutenda haki ndio vilifanya tumpende Magufuli.

Alikuwa akisema atafanya ujue kitafanyika kweli na akisema hafanyi sahau, ndio imetoka.

Alikuwa ni mwanasiasa wa tofauti sana. Hakuamini katika siasa za ulaghai na ku-sugarcoat.

Apumzike kwa amani mbinguni.
Vipi aliowaumiza kwa chuki zake?
 
Ukweli na kutenda haki ndio vilifanya tumpende Magufuli.

Alikuwa akisema atafanya ujue kitafanyika kweli na akisema hafanyi sahau, ndio imetoka.

Alikuwa ni mwanasiasa wa tofauti sana. Hakuamini katika siasa za ulaghai na ku-sugarcoat.

Apumzike kwa amani mbinguni.

Aliwatesa sana watumishi na haki zao za kupanda madaraja na nyongeza za mishahara hazikuzingatiwa katika utawala wake
 
Back
Top Bottom