WANAWAKE WASIKITISWA NA KAULI ZA GWAJIMA
Hatimaye kundi kubwa la wanawake Tanzania wakiongozwa na wenzao wa Dar es Salaam wamesikitishwa na kupinga kauli ya mchungaji Gwajima aliyoitoa hapo jana wakati anazungumza na wandishi wa habari. Katika maelezo yake mchungaji huyo anawaona wanawake kama ni viumbe dhaifu, wasio na maadili, wenye mapepo na wasio na thamani yeyote katika familia na jamii kwa ujumla. Akimtolea mfano mke wa Dr SLAA
Mchungaji huyo kutokana na kutofautiana kisiasa na Dr SLAA aliamua kufichua mambo yote ya siri za familia akieleza kuwa baada ya Dr SLAA kuondoka chadema amejitahidi kuongea na mke wa Dr SLAA ili wamshawishi abadilishe mawazo yake lakini hali ilikuwa tofauti.Nilimpa maneno ya matumaini, nitamtafuta mkewe niongee nae, nilimtafuta mkewe hadi Rose Garden, nilianza mimi kumbembeleza amruhusu baba aendelee na hayo maelezo nimeyarokodi na mimi ni mtu wa kurekodi.
Wanawake wanajiuliza kama ni kweli mtu anayejiita mtumishi wa Mungu kujihusisha na siasa hiyo haitoshi umeuthibishia ulimwengu kwa maelezo yako kutambua umuhimu wa wanawake afu bado unasema mama huyo hafai( WANAWAKE WOTE HAWAFAI), kama ulijua ana mapepo hafai kwa nni ulienda kumshawishi tena Hotelini na sio madhabahuni?.
Wanawake kweli wameshangazwa na mchungaji huyo kwa kusema hutambu umuhimu wa huyo mama wakati kuna kila dalili ya kutaka kumrubuni yeye na familia yake. Katika maelezo yake anasema siku iliyofata tarehe 28, nilimuita yule mama Kibo Complex, tukakaa ndani ya gari yake tunazungumza. Kweli mchungaji unakaa ndani ya gari na mke wa mtu afu unasema anamapepo HAFAI na ni maombezi gani unaweza kufanya na mke wa mtu zaidi ya masaa 3 kwenye gari?Hata hivo wanawake hao wameamua kufanya maandamano ya nchi nzima kupinga vitendo hivo vya kibaguzi, chuki, na unyanyasaji wa kijinsia aliofanyiwa mwanamke mwenzao.Pia taasisi mbalimbali za kiraia zitaungana na wanawake hao ktka kupinga kitendo hicho.