Askofu Gwajima tunakuhitaji Kanisani Kawe

Askofu Gwajima tunakuhitaji Kanisani Kawe

fikirikwanza

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2012
Posts
7,452
Reaction score
3,073
Eeee Mungu, turejeshee Askofu wetu Kanisani, Iwapo kuna njama chafu na mungu mwenye nguvu ambaye wewe unamtumikia akulinde, ulimkemea askofu kwa kosa la usaliti, yuda alisaliti pia ndo maana ni nadra sana mtu kuzaa mtoto na kumwita yuda, usaliti ni mbaya tumeona kwenye maandiko kibao ktika vitabu vitakatifu, ulifanya lililojema.

Askofu aliyesaliti wengine alipaswa kutubu na kuomba radhi, matusi yapi ambayo gwajima kasema kuliko usaliti??? enyi wenye hekima, gwajima kaja anatembea arudi akiwa anatembea mwenyewe, hadithi na mambo kama hayo tusingependa kusikia.

Mungu aliyeweka mbingu na viongozi ktk duniani basi akulinde na uovu wa aina yoyote, iwapo utapotea kwa kukemea usaliti, wasaliti watamchukiza mungu hadi kiwango cha mwisho.

Naomba tumuombee askofu aliyejasiri ktk dunia ya leo ya mwenye nguvu mpishe.

Nawasilisha
 
Jamani tuache mapenzi ya ukatoliki tuseme ukweli kosa alilofanya gwajima nilipi ukisema ukweli unakuwa mtumwa kwenye nchi hii?mbona askofu amekula hela za escrow hajaitwa police mm ni mkatoliki ila cjapendezwa na hili jambo lililo mkuta gwajima ila Mungu hawezi kuwaacha wenye roho mbaya ipo cku ukweli utakuwa wazi naimani kanisa katoliki linauwezo wakubadilisha chama endapo wataamua kwani kuwa karibu na serikali kunafanya washindwe kujiamulia nihayo tu
 
Mamndenyi saha hatakama unaupenzi na imani yako ila penye ukweli pasemwe hatakama amefanya mzazi wqko usiwe mtumwa wa fikra kwamba ukisema itakuaje alimwambia ukweli japo maneno mengine yana upande si mzuri ila kama ni jibu limeshapasuka
 
Eeee Mungu, turejeshee Askofu wetu Kanisani, Iwapo kuna njama chafu na mungu mwenye nguvu ambaye wewe unamtumikia akulinde, ulimkemea askofu kwa kosa la usaliti, yuda alisaliti pia ndo maana ni nadra sana mtu kuzaa mtoto na kumwita yuda, usaliti ni mbaya tumeona kwenye maandiko kibao ktika vitabu vitakatifu, ulifanya lililojema.

Askofu aliyesaliti wengine alipaswa kutubu na kuomba radhi, matusi yapi ambayo gwajima kasema kuliko usaliti??? enyi wenye hekima, gwajima kaja anatembea arudi akiwa anatembea mwenyewe, hadithi na mambo kama hayo tusingependa kusikia.

Mungu aliyeweka mbingu na viongozi ktk duniani basi akulinde na uovu wa aina yoyote, iwapo utapotea kwa kukemea usaliti, wasaliti watamchukiza mungu hadi kiwango cha mwisho.

Naomba tumuombee askofu aliyejasiri ktk dunia ya leo ya mwenye nguvu mpishe.

Nawasilisha
Najaribu kufikiria, mwaka 2012 Kova alikuja na story kwamba kulikuwa na mkenya kwa jina Joshua Mulindi aliyekwenda kanisani kwa Gwajima kuungama kuhusika na kumteka Dr Ulimboka. Gwajima alipinga hadharani uongo huo wa kova. Sijui baada ya hapo uhusiano wa kova (serikali) na Gwajima ulikuwaje!
 
Mamndenyi saha hatakama unaupenzi na imani yako ila penye ukweli pasemwe hatakama amefanya mzazi wqko usiwe mtumwa wa fikra kwamba ukisema itakuaje alimwambia ukweli japo maneno mengine yana upande si mzuri ila kama ni jibu limeshapasuka
Ujumbe wako una mantiki ila jaribu kujifunza kutumia vituo na koma kwenye sentensi zako.
 
Hivi pale Pana kanisa?! Kweli hizi dini zinazochipuka kama uyoga ni balaa.. eti naye kajipachika cheo cha uaskofu, ukisikia viroja ndiyo hivi..
 
Jamaa alizimia kijinga sana...mikwara yote ya "mpuuzi yuleee...mpumbavu yuleeee..." Kumbe yeye ndio mweupe kuliko..
 
Isikilize clip ya Gwajima wako ndo utapata majibu ya swali lako. Madai yake juu ya Pengo alipashwa kuyatoa kwa lugha ya sitaha. Tunajua viongozi wa kiroho km Gwajima wana lugha zenye hekima ya kimungu ambazo hazichoshi hata kuzisikiliza. Lkn kauli alizotumia Gwajima juu ya Pengo ni za kihuni tena ni sawa na lugha za wapiga debe stendi!!! Matusi aliyomtukania Pengo hayafai kwa mtu yoyote bila kujali rika. Huwezi kumfananisha na mtoto aliyevikwa pampers kwa umri km huo wa Pengo achilia mbali uaskofu wake. Acheni polisi wamhoji mwisho wa cku yatajulikana mengi juu ya Gwajima kwani si msafi ktk mfumo wake wa mali alizonazo ndo maana anazimia ovyo!!!
 
Jamani tuache mapenzi ya ukatoliki tuseme ukweli kosa alilofanya gwajima nilipi ukisema ukweli unakuwa mtumwa kwenye nchi hii?mbona askofu amekula hela za escrow hajaitwa police mm ni mkatoliki ila cjapendezwa na hili jambo lililo mkuta gwajima ila Mungu hawezi kuwaacha wenye roho mbaya ipo cku ukweli utakuwa wazi naimani kanisa katoliki linauwezo wakubadilisha chama endapo wataamua kwani kuwa karibu na serikali kunafanya washindwe kujiamulia nihayo tu

Gwajima amekamatwa na Polisi sio kanisa katoliki. wewe kama unamuweka kati ya watu wenye hekima ni mapenzi yako. kumbuka hata kama Pengo alikosea hakupaswa kuitwa mpuuzi. Wewe kama ni mkatoliki kweli basi utaelewa kuwa jambo alilofanya Gwajima ni jambo la hatari kwani sio Wakotoliki wote walifurahi kiongozi wao kutukana na hata waumini wa medhehebu mengine. Any way Gwajima amesamehewa.
 
Back
Top Bottom