JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Baada ya kuwepo kwa maneno mengi ya utani na mengine ‘serious’ kuhusu ahadi aliyoitoa kwa kwa baadhi ya wanakazi wa Kawe (Dar es Salaam) kuwa atawapeleka Jijini Birmingham Nchini England, hatimaye akizungumza katika mahojiano ya kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima amefunguka.
Amesema “Bahati mbaya watu wana misuse, Tanzania ina watu waliosoma na wasiosoma, wakati nazindua kampeni pale Bunju nilisema hivi:
“Nina uhusiano na Meya wa Birmingham na tunaweza kufanya exchange programs, kwamba vijana wetu wa huku ambao wana kidhi mahitaji wanakwenda kule na vijana wao wa kule wanakuja huku.
“Exchange Programs zinafanywa kwa Wanafunzi na watu wengine. Mungu akinisaidia ningependa kuitimiza ahadi niliyosema.”
Amesema “Bahati mbaya watu wana misuse, Tanzania ina watu waliosoma na wasiosoma, wakati nazindua kampeni pale Bunju nilisema hivi:
“Nina uhusiano na Meya wa Birmingham na tunaweza kufanya exchange programs, kwamba vijana wetu wa huku ambao wana kidhi mahitaji wanakwenda kule na vijana wao wa kule wanakuja huku.
“Exchange Programs zinafanywa kwa Wanafunzi na watu wengine. Mungu akinisaidia ningependa kuitimiza ahadi niliyosema.”