GE2020 Askofu Bagonza: Ujumbe kwa vyombo vya Ulinzi

GE2020 Askofu Bagonza: Ujumbe kwa vyombo vya Ulinzi

Hakuna laana mbaya kama usaliti kwa Nchi na ushoga
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
20201026_152723.jpg
 
Askofu Bogonza hudumia kondoo wako, mambo ya vyombo vya ulinzi kwako ni makubwa hujui kitu

Vyombo vya ulinzi ndio vinawapa waumini wako wasaa wa kutafuta sadaka wakuletee jumapili

Bila Amani, usingepata sadaka hapo kanisani kwako
Kwahiyo unasema hivyo vyombo vya usalama viue watu tu et?
 
KWA VYOMBO VYA ULINZI

Askofu Mkuu Oscar Romero wa El-Salvador ana ujumbe kwa vyombo vya ulinzi tunapoelekea Uchaguzi Mkuu tarehe 28/10/2020. Baba Mtakatifu Papa Francis alimtangaza kuwa Mtakatifu tarehe 14/10/2018. Askofu Romero alizaliwa 15/8/1917 na kufariki 24/3/1980. Alipadrishwa kuwa Padre 4/4/1942 na kuteuliwa kuwa Askofu Mkuu 1977. Alikufa kwa kupigwa risasi akiwa altareni akiadhimisha misa ya Sakramenti ya Meza ya Bwana. Muuaji wake, kachero wa serikali, aliingia kanisani kupitia mlango wa nyuma ya Kanisa na kumlenga kwa ustadi mkubwa wakati Askofu Mkuu Romero akiwa ameinua juu kikombe (chalice) cha divai kama ishara ya damu ya Kristo.

Baba Mtakatifu Francis alimtangaza Askofu Romero kuwa mfia dini.

Siku hiyo kabla ya kifo chake, alitoa ujumbe huu kwa vyombo vya ulinzi;

"Kaka zetu na ndugu zetu, mmetoka kwetu na mtarudi kwetu. Mnawaua ndugu zenu. Amri yoyote ya kibinadamu inayoagiza kuua ni batili
maana inajiweka juu ya amri ya Mungu isemayo USIUE. Hakuna Askari aliye juu ya Mungu na Askari halazimiki kutii amri iliyo kinyume na mapenzi ya Mungu. Hakuna anayelazimika kutii amri yenye dhambi ndani yake. Imewapasa maaskari kutii dhamiri hai za kimsingi zilizo ndani yao kuliko kutii amri batili.

Kanisa haliwezi kukaa kimya likiona amri za Mungu zinavunjwa na amri za wanadamu zinaheshimiwa, USIUE au USIIBE. KWA JINA LA MUNGU na kwa Jina la watu wanaoteseka na sauti zao kusikika mbinguni, ninawaamuru na kuwasihi, ACHA UKANDAMIZAJI, ACHA MAUAJI, ACHA DHULUMA".

Askofu Oscar Romero anaongea na wote waliokabidhiwa dhamana ya kulinda uhai wetu. Uamuzi wa kumtii Mungu uko katika vidole vilivyo jirani na kitufe kinachoruhusu risasi na mabomu. MSIKILIZE MUNGU PEKE YAKE.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.


Askofu Bagonza amefanya jambo jema sana kuwakumbusha vyombo vya ulinzi kuhusu umuhimu wa kulinda uhai wa watu. Abarikiwe sana Askofu



Na biblia katika 1Petro2:13-20 inatukumbusha utii.
13Kwa ajili ya Bwana, tiini kila mamlaka iliyowekwa na wanadamu: Kwa mfalme kwani ndiye aliye na mamlaka ya juu zaidi, 14au kwa maafisa aliowaweka, kwa kuwa mfalme amewatuma ili kuwaadhibu wale wanaokosa, na kuwapongeza wale watendao mema. 15Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe maneno ya kijinga ya watu wapumbavu. 16Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu. 17Mheshimuni kila mtu ipasavyo: Wapendeni jamaa ya ndugu waumini, mcheni Mungu, mpeni heshima mfalme.

18Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wema na wapole peke yao, bali pia wale walio wakali. 19Kwa maana ni jambo la sifa kama mtu akivumilia anapoteswa kwa uonevu kwa ajili ya Mungu. 20Kwani ni faida gani kwa mtu kustahimili anapopigwa kwa sababu ya makosa yake? Lakini kama mkiteswa kwa sababu ya kutenda mema, nanyi mkastahimili, hili ni jambo la kusifiwa mbele za Mungu.

Tufate sheria na taratibu za tume na mwombe Mungu atujalie uchaguzi wenye amani Mjep cocochanel Kawe Alumni Bia yetu Themagufulianz BUSH BIN LADEN mugah di mathew tameer IDEGENDA NAWATAFUNA Msengapavi Next Man Nguseroh minyoo Wakudadavuwa
stakehigh Daby Erythrocyte
Extrovert Kiwarhoapandenga Sky Eclat pilipili kichaa Kamakabuzi mkombengwa mwaimu @ issenye mwanateknolojia
GENTAMYCINE Village fooler Enlightening mjingamimi Gluk 4G LTE

Piga kura Rudi nyumbani
 
Jwtz na polisi punguzeni ukali huko Zanzibar.
Nyie ndo mtasababisha Zanzibar pachafuke.
Mnapiga Sana watu.
 

Askofu Bagonza amefanya jambo jema sana kuwakumbusha vyombo vya ulinzi kuhusu umuhimu wa kulinda uhai wa watu. Abarikiwe sana Askofu




Na biblia katika 1Petro2:13-20 inatukumbusha utii.
13Kwa ajili ya Bwana, tiini kila mamlaka iliyowekwa na wanadamu: Kwa mfalme kwani ndiye aliye na mamlaka ya juu zaidi, 14au kwa maafisa aliowaweka, kwa kuwa mfalme amewatuma ili kuwaadhibu wale wanaokosa, na kuwapongeza wale watendao mema. 15Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe maneno ya kijinga ya watu wapumbavu. 16Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu. 17Mheshimuni kila mtu ipasavyo: Wapendeni jamaa ya ndugu waumini, mcheni Mungu, mpeni heshima mfalme.

18Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wema na wapole peke yao, bali pia wale walio wakali. 19Kwa maana ni jambo la sifa kama mtu akivumilia anapoteswa kwa uonevu kwa ajili ya Mungu. 20Kwani ni faida gani kwa mtu kustahimili anapopigwa kwa sababu ya makosa yake? Lakini kama mkiteswa kwa sababu ya kutenda mema, nanyi mkastahimili, hili ni jambo la kusifiwa mbele za Mungu.



Piga kura Rudi nyumbani.
 
KWA VYOMBO VYA ULINZI

Askofu Mkuu Oscar Romero wa El-Salvador ana ujumbe kwa vyombo vya ulinzi tunapoelekea Uchaguzi Mkuu tarehe 28/10/2020. Baba Mtakatifu Papa Francis alimtangaza kuwa Mtakatifu tarehe 14/10/2018. Askofu Romero alizaliwa 15/8/1917 na kufariki 24/3/1980. Alipadrishwa kuwa Padre 4/4/1942 na kuteuliwa kuwa Askofu Mkuu 1977. Alikufa kwa kupigwa risasi akiwa altareni akiadhimisha misa ya Sakramenti ya Meza ya Bwana. Muuaji wake, kachero wa serikali, aliingia kanisani kupitia mlango wa nyuma ya Kanisa na kumlenga kwa ustadi mkubwa wakati Askofu Mkuu Romero akiwa ameinua juu kikombe (chalice) cha divai kama ishara ya damu ya Kristo.

Baba Mtakatifu Francis alimtangaza Askofu Romero kuwa mfia dini.

Siku hiyo kabla ya kifo chake, alitoa ujumbe huu kwa vyombo vya ulinzi;

"Kaka zetu na ndugu zetu, mmetoka kwetu na mtarudi kwetu. Mnawaua ndugu zenu. Amri yoyote ya kibinadamu inayoagiza kuua ni batili
maana inajiweka juu ya amri ya Mungu isemayo USIUE. Hakuna Askari aliye juu ya Mungu na Askari halazimiki kutii amri iliyo kinyume na mapenzi ya Mungu. Hakuna anayelazimika kutii amri yenye dhambi ndani yake. Imewapasa maaskari kutii dhamiri hai za kimsingi zilizo ndani yao kuliko kutii amri batili.

Kanisa haliwezi kukaa kimya likiona amri za Mungu zinavunjwa na amri za wanadamu zinaheshimiwa, USIUE au USIIBE. KWA JINA LA MUNGU na kwa Jina la watu wanaoteseka na sauti zao kusikika mbinguni, ninawaamuru na kuwasihi, ACHA UKANDAMIZAJI, ACHA MAUAJI, ACHA DHULUMA".

Askofu Oscar Romero anaongea na wote waliokabidhiwa dhamana ya kulinda uhai wetu. Uamuzi wa kumtii Mungu uko katika vidole vilivyo jirani na kitufe kinachoruhusu risasi na mabomu. MSIKILIZE MUNGU PEKE YAKE.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Alinena vyema mtumishi huyo wa Mungu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Unadhani ni kwanini wanaitwa polisiccm na siyo polisichadema au polisiact!?
Ni kweli mkuu, askari hana chama. Kazi yao kubwa ni kulinda wananchi na mali zao. Nasi tunaolindwa tufate taratibu tusiwapige mawe askari
 
Unafikiri wanaweza pigwa mawe bila sababu???

Kwa sababu yoyote Ile sio sawa kuwapiga watu wengine mawe hata wewe vibaka. Sasa tunaona hao wameamua kuwapiga mawe wenye mamlaka.

Wewe na familia yako unaweza kwenda barabarani kuwarushia police mawe?? Acheni kuwatumia vijana vibaya
 
Acha kujitoa ufahamu! Watanzania wengi wanawaita hivyo bila woga wala aibu si BAK peke yake.
Ni kwa sababu wewe umeamua kuwaita hivyo. Mimi nawaita police
 
Kama ni uoga vunja sheria tu kiongozi

Watu wako nyuma ya keybords, watoto wao wako sehemu salama halafu wanachochea watoto wa maskini wakawapige police mawe

Yaani hawa CHADEMA wako tayari hata kutoana roho ili wapate dola
 
Askofu Bogonza hudumia kondoo wako, mambo ya vyombo vya ulinzi kwako ni makubwa hujui kitu

Vyombo vya ulinzi ndio vinawapa waumini wako wasaa wa kutafuta sadaka wakuletee jumapili

Bila Amani, usingepata sadaka hapo kanisani kwako
Ulaaniwe wewe na kizazi chako chote mwenyezi Mungu pokea sala yangu Amen
 
Back
Top Bottom