Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,499
- 51,092
*Lwakalinda Kalikawe Bagonza kaandika hivi:*
NEC WAHURUMIENI WANANCHI
NEC WAHURUMIENI VIONGOZI.
Kuna jambo haliko sawa. Kama liko sawa, basi kuna jambo haliko sawa ndani yangu.
1. Ni mzigo na adhabu kubwa kwa Wananchi kuongozwa na kiongozi ambaye hawakumchagua. Ni kuwatesa wananchi, ni kuwadharau, na kuwadhalilisha. Tuliwakataa wakoloni kwa sababu walitutawala bila sisi kuwachagua. Desemba 9 kila mwaka ni muhimu kwetu kwa sababu tunakumbuka siku tulipoamua kuchagua Viongozi na watawala wetu.
2. Ni mzigo mzito kwa kiongozi kuwaongoza watu ambao hawakukuchagua. Ni dharau na mateso kwake kulazimika kuwaongoza watu ambao hujui kama wanakupenda au hawakupendi kwa sababu hawakupiga kura kukuchagua.
Yote mawili hapo juu ni uchokozi. Tume inawachokoza wananchi kwa kuwalazimisha kuongozwa bila kuchagua. Ni kuwachokoza Viongozi kwa kuwalazimisha kuongoza bila ridhaa ya wananchi. Uchokozi haujawahi kuwa na matokeo mazuri.
Vigezo vya mtu kugombea vinafahamika kikatiba: Raia, umri, dhamana ya chama, kutohukumiwa kifungo, kutohukumiwa kukwepa kodi, muda wa kurejesha fomu nk. Haya hayahitaji wiki kuyaamua
Viongozi wetu uteuliwa/upendekezwa na vyama na kuchaguliwa na wananchi. Tume imeanzisha kundi jipya la Viongozi wanaoteuliwa na tume. Jimbo liitwalo TUME liko mkoa gani? Kata iitwayo TUME iko wilaya gani?
Tulifanya hivyo serikali za mitaa na sasa tunataka kufanya hivyo kwenye bunge. TUNAKOSEA. Hatutakuwa na uhalali wa kudai utii na Maendeleo kwa watu waliolazimishwa kuongozwa na watu wasiochaguliwa. Hatutakuwa na uhalali wa kudai matokeo chanya kwa Viongozi tuliowalazimisha kuongoza bila kuchaguliwa.
Hata baadhi ya mifumo ya kidini isiyochagua Viongozi kidemokrasia hailazimishi muumini kuikubali. Ni kwa mujibu wa Imani, si Sheria.
NEC WAHURUMIENI WANANCHI
NEC WAHURUMIENI VIONGOZI.
Kuna jambo haliko sawa. Kama liko sawa, basi kuna jambo haliko sawa ndani yangu.
1. Ni mzigo na adhabu kubwa kwa Wananchi kuongozwa na kiongozi ambaye hawakumchagua. Ni kuwatesa wananchi, ni kuwadharau, na kuwadhalilisha. Tuliwakataa wakoloni kwa sababu walitutawala bila sisi kuwachagua. Desemba 9 kila mwaka ni muhimu kwetu kwa sababu tunakumbuka siku tulipoamua kuchagua Viongozi na watawala wetu.
2. Ni mzigo mzito kwa kiongozi kuwaongoza watu ambao hawakukuchagua. Ni dharau na mateso kwake kulazimika kuwaongoza watu ambao hujui kama wanakupenda au hawakupendi kwa sababu hawakupiga kura kukuchagua.
Yote mawili hapo juu ni uchokozi. Tume inawachokoza wananchi kwa kuwalazimisha kuongozwa bila kuchagua. Ni kuwachokoza Viongozi kwa kuwalazimisha kuongoza bila ridhaa ya wananchi. Uchokozi haujawahi kuwa na matokeo mazuri.
Vigezo vya mtu kugombea vinafahamika kikatiba: Raia, umri, dhamana ya chama, kutohukumiwa kifungo, kutohukumiwa kukwepa kodi, muda wa kurejesha fomu nk. Haya hayahitaji wiki kuyaamua
Viongozi wetu uteuliwa/upendekezwa na vyama na kuchaguliwa na wananchi. Tume imeanzisha kundi jipya la Viongozi wanaoteuliwa na tume. Jimbo liitwalo TUME liko mkoa gani? Kata iitwayo TUME iko wilaya gani?
Tulifanya hivyo serikali za mitaa na sasa tunataka kufanya hivyo kwenye bunge. TUNAKOSEA. Hatutakuwa na uhalali wa kudai utii na Maendeleo kwa watu waliolazimishwa kuongozwa na watu wasiochaguliwa. Hatutakuwa na uhalali wa kudai matokeo chanya kwa Viongozi tuliowalazimisha kuongoza bila kuchaguliwa.
Hata baadhi ya mifumo ya kidini isiyochagua Viongozi kidemokrasia hailazimishi muumini kuikubali. Ni kwa mujibu wa Imani, si Sheria.