Askari wenye vyeti feki

Askari wenye vyeti feki

Usijifanye huelewi.
Kuna vitu hatutavielewa kwa urahisi,tuwaachie serikali. Hivi,unatarajia kulundika askari 2000 pale necta wakikata rufaa ya vyeti ni vyema! Tofautisha na ilivyo kwa waalimu na nurses.
 
Wafukuzwe tu hamna namna. Mbona wengine wanafukuzwa? Kama walienda CCP bila vyeti ni sawa, lakini kama walienda vyeti feki wafukuzwe
 
Mfano mkoa mmoja ukishakuwa na manjagu feki 100 unadhani watashindwa kuwasiliana? Unadhani watakaa tu ndani? Halafu ukiwafukuza kwa vyeti ndio lazima warudi mikoani kwao? Familia zao watazihamisha vipi na hakuna motisha?

Hawa askari wakitaka kuwaweza wawashike kwenye kigezo cha UMRI tu. Waluofikisha muda wa kutumikia watolewe. Waingize nguvu mpya.wafanye screening na vetting ya kueleweka ili kupata vijana wapya.

Askari hawashughulishi vichwa sana kwenye utafutaji. Kitambulisho,uniforms ndio mtaji wao. Wakibanwa sana watatuletea design za kina mungiki.
 
Kumekuwepo na hoja mitandaoni kuwa askari wenye vyeti feki wakifukuzwa basi uharifu utaongezeka hii ni dhana tu ambayo haina ukweli kwanini nasema hivyo

Tukumbuke hawa askari si kwamba wote wanatoka mkoa mmoja, au wilaya moja hawa askari kila mtu anakwao tukumbuke ile dhana ya watawanye kisha watawale ndio sawa na hii kwa askari endapo wakitimuliwa kwa kutumia vyeti feki hawa kila mtu ataenda kwao hivyo ni ngumu sana kushawishika akaanza uharifu

Mfano kituo au kambi moja wakapatikana askari ishirini hawa lazima kila mtu akitimuliwa atarudi kwao mfano mmoja arudi kwao nkasi rukwa uko mwingine aende lindi uko unafikilia nini hapo kuna munganiko tena

Kitu kingine mtaani kuna askari wengi ni wastafu na wamepigika ila hii hali ya kufanya kila anayestaafu anarudi kwao imewatawanya hivyo basi hata ile dhana ya kuanzisha genge la kihuni haipo maana wanesambaa wamepoteana kabisa

Hivyo basi suala kufukuza kazi askari wenye vyeti feki linawezekana kabisa
Unataka wakifukuzwa uchukue nafasi zao?
 
Wameshaanza kukaguliwa jaman haya mambo hakuna atakaepona
 
Huyu aliyechukua fomu mwenyewe ameshafanikiwa kutugawa watanzania kwa hali hii chuki hazitokwisha mioyoni mwa wa Tz na wataibuka majambaz wengi zaidi ya hao wanaowahofia
 
Watu wengi wamepita jeshini na wapo mtaani....hao watamfanyia nani uhuni....yaani kama hawana vyeti wafukuzwe tu...tuonane mtaani
 
tumeanza kukaguliwa jamani hatari sana hapa gumbo koto harafu naenda doria
 
Hapo kila mtu atafanya uhalifu mahala pake, sio mpaka waungane
 
Je umewahi kushuhudia jambazi akiwa kazini? chezea ugali unaokula si 92KJ
 
Kumekuwepo na hoja mitandaoni kuwa askari wenye vyeti feki wakifukuzwa basi uharifu utaongezeka hii ni dhana tu ambayo haina ukweli kwanini nasema hivyo

Tukumbuke hawa askari si kwamba wote wanatoka mkoa mmoja, au wilaya moja hawa askari kila mtu anakwao tukumbuke ile dhana ya watawanye kisha watawale ndio sawa na hii kwa askari endapo wakitimuliwa kwa kutumia vyeti feki hawa kila mtu ataenda kwao hivyo ni ngumu sana kushawishika akaanza uharifu

Mfano kituo au kambi moja wakapatikana askari ishirini hawa lazima kila mtu akitimuliwa atarudi kwao mfano mmoja arudi kwao nkasi rukwa uko mwingine aende lindi uko unafikilia nini hapo kuna munganiko tena

Kitu kingine mtaani kuna askari wengi ni wastafu na wamepigika ila hii hali ya kufanya kila anayestaafu anarudi kwao imewatawanya hivyo basi hata ile dhana ya kuanzisha genge la kihuni haipo maana wanesambaa wamepoteana kabisa

Hivyo basi suala kufukuza kazi askari wenye vyeti feki linawezekana kabisa
wanagroup lao la police force ni rahisi kukutana
 
Kazi za askari wala hazihitaji elimu kubwa. Hao wachache wenye vyeti halali wanatosha.
Hao wenye vyeti feki waachwe waendelee kupiga paredi. Paredi haihitaji form four
 
Kuna vitu hatutavielewa kwa urahisi,tuwaachie serikali. Hivi,unatarajia kulundika askari 2000 pale necta wakikata rufaa ya vyeti ni vyema! Tofautisha na ilivyo kwa waalimu na nurses.
Walimu na nurses sio watu?? Polisi ndio watuu
 
He he! ukatupe watu wanaojua kutumia siraha na mbinu za mapambano! hlf haohao wewe unapokuwa umelala usiku wenyewe wanaangaika na vibaka,majambazi,wezi na mitandao ya kiharifu,wauza ngada n.k hii tayari ni connection moja kubwa kwao!! sasa mbaya zaidi hebu chukulia unafukuza makomando hata 20! vyeti feki wakuu wa jeshini hata 50..!! unategemea nini..?!

Ni kweli,endeleeni navyo tu!
 
Back
Top Bottom