The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,426
Kwa namna hayati John Pombe Magufuli alivyomtengeneza Samia Suluhu Hassan kIsiasa, wengi walidhani angekuwa mstari wa mbele kuhudhuria kumbukumbu yake. Kweli, binadamu tu viumbe wenye kusahau kirahisi na haraka.
Kwanini Samia hakuhudhuria kumbukumbu ya mwendazake? Ama kweli, asiyekuwepo na lake halipo. Isitoshe, paka akiondoka, panya hujitawala.
Inasikitisha. Pia, ni aibu na unyama sina mfano. Binadamu ni nani hadi ajilishe pepo na kujisahaulisha utadhani ataishi milele?