Asiyekujua hakuibii mke/mme

Asiyekujua hakuibii mke/mme

Mwanapropaganda

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
4,235
Reaction score
2,512
Malalamiko ya wanandoa kutokuwa waaminifu miongoni mwao yamekuwa mjadala wa sasa kiasi cha watu kuanza kushutumiana na wakati mwingine kuharibu mahusiano yao na hatimaye kuachanisha mahusiano ya kindoa.

Pamoja na hayo nataka mikuambie asiyekujua hakuchukulii mkeo au mmeo, mbaya wako ni yule inayemuita rafiki, mshkaji, msela au hata wale majirani unaowapa heshima za uncle, sister, brother aunt, mdogo wako na hata father ilhali sio uncle, sister, brother, aunt, wala father kiuhalisia. Hao ndio wabaya wako, wanasubiri uwape fursa tu wakinukishe, kama unabisha fuatilia wale wanaolalamika kuibiwa ujuwe wanaowaibia ni akina nani kama sio hao niliokuambia hapo juu.

Hata wale wenye wake wanaofanya kazi kwenye mafiosi ya serikali na makampuni bado hakuna cha boss wala manager anayeweza kukuibia mke ikiwa hajui mwanaume wake yupoje au ni mtu wa namna gani, watategemea mkeo awaambie jinsi anavyokuchukulia ndio wapime ikiwa mamboozs yanaweza kuwa mabaya mbeleni. Ni nadra sana kusikia mwanaume anatembea na mke wa mwanaume mwenzake huku akiwa hafahamu alivyo.

Usaliti ni tabia mbaya kama zilivyo tabia zingine, watu wanasalitiana pale a kuwepo kwa fursa, kwahiyo kuwa makini na watu unaoishi nao karibu.
 
mara nyingine wanawake wenye waume hawaseme/.wanaficha hizo taarifa ili kufanikisha ubaradhuli wao.akishakumiliki ndio unakuja kuambiwa/kujua na kuacha inakuwa sheedah.hawasemi ukweli.mwanzoni baadhi ya wake za watu.
 
mara nyingine wanawake wenye waume hawaseme/.wanaficha hizo taarifa ili kufanikisha ubaradhuli wao.akishakumiliki ndio unakuja kuambiwa/kujua na kuacha inakuwa sheedah.hawasemi ukweli.mwanzoni baadhi ya wake za watu.
Kwani nyie hua mnasema mapema? Si mpaka mdakwe nyie
 
Kwani nyie hua mnasema mapema? Si mpaka mdakwe nyie
hata sisi.sijataja sisi kwa vile mada inasema mke /mume wa mtu! mimi kama mume naongelea upande wangu na uzoefu ninaoujua.upande wa wanaume kuwadanganya nyie ni nyie mchangie wanawake.
 
Kwa asiekujua kuelezea mtu/watu changamoto za mahusiano yenu let say ugomvi, ukata wa hela kwa mtu ni fursa ya kuiandaa chup**i yako ianze kuagana na mwili
 
Back
Top Bottom