Asante sana Ngeleja

Asante sana Ngeleja

Huyu jamaa ni hatarii sana, mi namkubali kwa kweli ana uwezo wa kipekee, he deserves to be the president of Tanzania 2015

Join Date : 9th October 2014
Posts : 30
Rep Power : 317
Likes Received6
Likes Given0
 
Utendaji wake haswa ktk wizara ya nishati na madini unajiziilisha kuwa anaweza kuread the nation

Kuread the nation????
Join Date : 1st April 2012
Posts : 44
Rep Power : 450
Likes Received8
Likes Given16
 
Aisee huyu jamaaa anakuja kasi. Hapo mwazo alipotajwa ktk ban niliona km hakustahili kumbe legacy yake ni hatari tena ni tishio kwa wengine.

Wote mmefungua akaunti JF kwa ajili ya kupiga debe Ngeleja agombee urais??? Basi bila shaka ndio mtajua vizuri uchafu wake
 
Kwa kitabu sawa! lakini kwa maadili ni mpiga dili kama chenge, kumbe wanasheria ndo wanatudhoofisha sana nchi hii
 
shida ya kupiga viroba asubuhi ndo hii.......zinakuja thread za mazingaombwe ka hizi
 
ukiona mtu anamsifia mtu mchafu basi ujue yeye mchafu zaidi.
 
jizi mwizi jambazi, kabaji, haramia,jangili,za mali za watanzania arudishe hela zetu huyu
 
Hivi anawalipa pesa kiasi gani huyu mtu kuja kumpamba humu?

Watanzania tuna macho na masikio,tunasikia na tunaona wenyewe nani anayetufaa sisi na nani ni mwizi,fisadi na mwenye kujikweza(kufikia hatua ya kumzaba makofi mlinzi wa ATM)

This time kombe halifunikwi,na hata likifunikwa,mwanaharamu hapiti

Ndio hapiti!!

hizo ni cheap politics
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Ngeleja yuko vzur wadau, tuwe wachambuz wazur tusifanye vitu kwa kuangalia juu juu tuu yuko safii sana huyo...Dada celine sikujui lakini nakupa bigup

Hayo mazuri kaeni nayo wenyewe,sie wana Sengerema tumeshampa salamu kwa uchaguzi wa serikali za mitaa,twamsubiri kwa hamu 2015 if he will dare!!
 
Wote mmefungua akaunti JF kwa ajili ya kupiga debe Ngeleja agombee urais??? Basi bila shaka ndio mtajua vizuri uchafu wake

Waache wafu wazike wafu wenzao! Huyo wanaempigia debe anajua salamu alizopewa na Wanasengerema kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa.
 
MH.WILLIUM MGANGA NGELEJA SULUHISHO BORA MADINI

........................mh.Rais Kikwete pamoja na mh.Willium Mganga Ngeleja ndio waliokaa kwa muda mrefu kulingana na ugumu wa wizara hiyo,Mh.Kikwete alikaa miaka 6 na mh.Willium Mganga Ngeleja alikaaa miaka 5 na miez 8 kitu kinachoonyesha upambanaj mkubwa .......

mh.Ngeleja, kwaukweli mambo aliyoyafanya yatabaki kuwa msaada mkubwa kwa Tanzania yetu,yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo mh.Ngeleja aliyafanya alipokuwa ktk wizara ya Nishat na Madini ikiwa ni kwa muda wa miaka 5 na miez 8,:-

1.Itakumbukwa kuwa Ngeleja ndiye aliyepambana kwa hali na mali mpk kuhskikisha kunapatikana maeneo zaidi kwa ajili ya wachimbaji wadogowadogo.

2.Itaendelea kukumbukwa kuwa ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa mfuko maalum wa kuwasaidia wadogo nchini kitu ambacho kinazungumzwa na wachimbaji wadogo mpaka leo,na hata juzi nilipokuwa ziarani Geita nilipata kutembelea maeneo ya wachimbaji wadogo na walimtaja Ngeleja kama mkombozi wao,na daima wataendelea kumtukuza kwa anachokifanya kwani anafanya mambo mazur anapokabiziwa majukum ya kijamii.

4.Mh.Ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa kutoa hati ya uasili(certificate of origin) kwa wanaouza madini ya Tanzanite nje ya nchi ikiwa ni mkakati wa serikali kudhibiti uuzwaji haramu wa madini ya Tanzanite,kitu amabcho hata Prof.Muhongo anajivunia sasa na kipindi fulani hivi ktk ziara yake mererani yanapopatikana madini ya Tanzanite mh.Muhongo alimtaja Ngeleja kama msaada mkubwa katika hilo...

Mwisho
Watanzania tunapaswa kuwasemea watu kwa mabaya yao na mazuri yao yalio mengi kwani hakuna mwanadam aliye kamili,..Ngeleja kafanya mengi sana sekta ya madini na hayo hapo juu ni kwa uchache wake.

The writter must be a stupid creature of its own type! Una akili wewe? Zinakutosha?
Uandikaji wa aina hii niliusoma kwenye kitabu cha Shaában Robert akimsifu mkewe. Nahisi hata mkewe alimsifu hivyo mumewe Shaaban.

Bila kujali sababu ya kuandika haya mimi nimekuweka kundi la wajinga kwa sababu hukuhangaika hata kidogo kujiuliza kwa nini alikaa miaka yote hiyo ktk wizara, hukuhangaika kueleza mafanikio yake badala yake unaandika mambo ya kizembe. Nani alikwambia Certificate of orifgin ilianzishwa na Ngereja? Huji kwamba Mwadui Diamond imekuwa na mtindo huo kabla hata Ngereja hajazaliwa? Shiiit!

Kama kweli Huko Geita wanamsifu ngereja, basi ni wale wenye akili kama zako. Geita kuna watu wamenyang'anywa maeneo, wakaishi kwenye magofu kwa zaidi ya miaka 4 bila hata serikali kuhangaika nao. Huko Geita ndiko GGM wanaishi utadhani hakuna serikali ya mkoa. Kisa wanawasiliana na wala rushwa wenzenu dar.

Umeshindwa hata kueleza kwamba kipindi cha Ngereja wako, ndo kipindi ambacho madini yametoroshwa kwa wingi kuliko kipindi kingine ktk historia ya nchi hii.

Kama huu ndo uandikaji wako kwa kiwango cha sasa naomba uwe kimya, usubiri upate uzoefu maana naona ulijiunga ili kumpa sifa Ngereja. Unajiunga, baada ya siku tano unabowa hivi?
Join Date : 12th December 2014
Posts : 3
Rep Power : 0
Likes Received 6
Likes Given 0
 
Kwani wewe Celine umelipwa shilingi ngapi kumfanyia huyo ngeleja kampeni ? Sifa ulizozitaja sijaona hata moja inayoweza kumfanya mtu ashtuke kuwa kuna jambo la maana kalifanya hadi watu tuanze kumfikiria urais.Hata CV yake mbona ni ya kawaida sana mbona ?
 
MH.WILLIUM MGANGA NGELEJA SULUHISHO BORA MADINI

Itakumbukwa kuwa sekta ya nishati na madini ilishawah kukaliwa na nawazir wengi mno wakuwemo kina Mzee Msabaha,Mzee Daniel Yona na wengine wengi tuu,lakini hao wote walikuwa wanaishia kuwa katika wizara hiyo kwa muda wa miaka 2 na nusu na muda mwingine miwili kamili, ni mawazir watatu tuu akiwemo mh.Rais Kikwete pamoja na mh.Willium Mganga Ngeleja ndio waliokaa kwa muda mrefu kulingana na ugumu wa wizara hiyo,Mh.Kikwete alikaa miaka 6 na mh.Willium Mganga Ngeleja alikaaa miaka 5 na miez 8 kitu kinachoonyesha upambanaj mkubwa kwenye wizara hii na mh.Ngeleja, kwaukweli mambo aliyoyafanya yatabaki kuwa msaada mkubwa kwa Tanzania yetu,yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo mh.Ngeleja aliyafanya alipokuwa ktk wizara ya Nishat na Madini ikiwa ni kwa muda wa miaka 5 na miez 8,:-

1.Itakumbukwa kuwa Ngeleja ndiye aliyepambana kwa hali na mali mpk kuhskikisha kunapatikana maeneo zaidi kwa ajili ya wachimbaji wadogowadogo.

2.Itaendelea kukumbukwa kuwa ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa mfuko maalum wa kuwasaidia wadogo nchini kitu ambacho kinazungumzwa na wachimbaji wadogo mpaka leo,na hata juzi nilipokuwa ziarani Geita nilipata kutembelea maeneo ya wachimbaji wadogo na walimtaja Ngeleja kama mkombozi wao,na daima wataendelea kumtukuza kwa anachokifanya kwani anafanya mambo mazur anapokabiziwa majukum ya kijamii.

3.Mwezi April 2010 mh.Ngeleja alipiga marufuku usafirishaji nje ya nchi wa madini ghafi ya Tanzanite yenye ukubwa unaozidi gramu1,kitu ambacho juzi nilivyokuwa nazungumza na baadhi ya mawazir na baadhi ya viongoz wa juu wa chama walikipenda na kusema Ngeleja anafaa kuingia wazir mkuu wa Tanzania au hata Raisi kama akiamua kugombea

4.Mh.Ngeleja ndie muasisi wa utaratibu wa kutoa hati ya uasili(certificate of origin) kwa wanaouza madini ya Tanzanite nje ya nchi ikiwa ni mkakati wa serikali kudhibiti uuzwaji haramu wa madini ya Tanzanite,kitu amabcho hata Prof.Muhongo anajivunia sasa na kipindi fulani hivi ktk ziara yake mererani yanapopatikana madini ya Tanzanite mh.Muhongo alimtaja Ngeleja kama msaada mkubwa katika hilo...

Mwisho
Watanzania tunapaswa kuwasemea watu kwa mabaya yao na mazuri yao yalio mengi kwani hakuna mwanadam aliye kamili,..Ngeleja kafanya mengi sana sekta ya madini na hayo hapo juu ni kwa uchache wake.

for this hakuna zaid yake.....next president
 
Ngeleja?????FOR WHAT!!!!!!!umekosa wa kumsifu mpaka utuletee huyu FISADI wa escrow???Mmmechelewa,he has to go even to HELL!!!
 
Back
Top Bottom