KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 278
Nimeianza safari mapema leo asubuhi nikiwa njia moja kwendda kulitumikia Taifa langu baada ya kuhamishwa kituo changu cha kazi kutoka Wilaya ya Serengeti kwenda Wilaya ya Chato Mkoa wa Geita niko ndani ya lori ndogo aina ya Canter ikiwa na vyombo vyangu nimefika Mwanza nikafanya mahitaji baadae njia. moja kwenda kivukoni nimetumia kivuko cha Kigongoni-Busisi.Duh saa saba mchana nilikuwa tayari kwenye foleni ya kuvushwa ila sasa tokea saa saba mchana hadi hivi sasa saa mbili kamili usiku ndio niko ndani ya pantoni navuka kwenda ng'ambo ya pili nawauliza wenyeji wananiambia mbele yangu nasubiliwa na masaa matatu ya kukimbia kwenye lami ya kwenda kwao na Mh Magufuli.Ninachompongeza Mh ni jinsi gani alivyoboresha suala la tiketi za kielectroniki tofauti na awali unaambiwa watumishi wa Temesa walikuwa na kaescrow kao hapo.Bado nipo katikati ya maji ikiwa ni mara yangu ya kwanza kabisa kusafiri na chombo kinachotumia maji kama sehemu ya barabara yake.WanaJf wa Chato naombeni mnipokee jamani.