Arusha wamvua nguo MIzengo Pinda!!

Arusha wamvua nguo MIzengo Pinda!!

Du!
Title imenistua.
Nikajiuliza,kama kavuliwa nguo,tigo yake imepona kweli?

...heh heh heh! mimi nilijikuta nikijiuliza wamemkuta na Boxer ama Zaibon ya rangi gani!! Vichwa vya Uzi vingine bhana....?!:smile-big:
 
Mkuu NasDaz kwenye weigh bridges wanaangalia/wanapima vitu viwili mainly. Wanaangalia Axle load na Gross Vehicle Mass.

Ikitokea axle load imezidi kwa sababu ya kupanga vibaya mzigo, au mzigo umesogea kutokana na kufukuzana au matuta ya barabarani basi transporter anapewa fursa ya kure-arrange mzigo wake.
Lakini ikitokea GVM imezidi basi hapo hakuna namna ni lazima mzigo upunguzwe.

Ukiangalia jinsi baranara zetu zilivyojaa mahandaki pamoja na matuta rasmi na yasiyo rasmi basi possibility ya mzigo kusogea na kusababisha axle load kuzidi au kupungua ni mkubwa sana.

Ninachofikiria mimi chanzo kikubwa cha weigh bridges variations ni kukosa ''proper and timely maintenance''. Wanachojali sana Tanroads ni kuingiza hela tu.
 
Last edited by a moderator:
sheria zivunjwe kunusuru uchumi? Magufuli is very right, kama sheria zipo zisimamiwe sio maswala ya kunusuru uchumi

Pinda amenusuru loss kiuchumi. Magufuli hakuangalia hilo, yeye katoa maamuzi kirobot robot bila kuangalia pande zote, kisha atoe uamuzi ambao ni balanced ili mambo yaendelee. Unavyoropoka eti mkapaki malori yenu upenuni kwenu hakujua anazungumzia loss kwenye sekta ya uchukuzi asilimia ngapi? Au alifikiri ni vilori viwili vitatu? je Mgufuli alikuwa waziri wa barabara miaka mingapi? Mbona hakuliona hilo ? Na hata baada ya kutoliona haoni ingekuwa busara kukaa nao na kuondoa mapungufu hayo? Hiyo asimilia 5 sio issue. Issue ni hilo lilioonekana Arusha. Huko mezani ndio kuna rushwa kubwa pengine kuliko sehemu nyingine zote nchini maana ni kila siku na kila mizani jamaa wanapokea mlungula ili uzito usioruhusiwa upite. Magufuli ni robot type maana hajui kama waendesha mizani ni janga.
 
Kama kuna kipindi nilipata kumdharau na kumchukia kupita kiasi Mheshimiwa Pinda ni pale alipoingilia maamuzi ya John Pombe Magufuri kuhusu suala zima la mizani! Wafanyabiashara wa malori wakacheza na akili ya Watanzania na Watanzania nao bila kujitambua wakawa upande wao na kuona alichofanya Magufuri sio sahihi! Watu wa malori wakafikia hadi kusema eti Tanzania ndiyo nchi pekee inayoruhusu uzito mdogo wakati ukweli ni kwamba Tanzania ndio miongoni mwa nchi zinazoruhusu uzito mkubwa zaidi wa Tani 56. Kenya labda wabadilishe sasa, wao ilikuwa maximum load ni 48 tonnes…..na ikiwa inazidi upande mmoja tu; unakula bonge la faini! Wafabiashara wa Tanzania wakawahadaa Watanzania kiasi cha kutuonesha as if suala la mzigo ku-move na kuegemea kwenye axle moja ni suala la Tanzania peke yake! Upumbavu mwingine ambao Wafanyabiashara waliwadanganya Watanzania na sisi kama mazuzu tukawaunga mkono ni suala la ubovu wa mizani!

Mungu hamfichi mnafiki. Kwa mujibu wa ITV saa 2 usiku huu; Wakala wa Vipimo Arusha ilifanya ukaguzi wa kushitukiza! Magari kibao yamejaza kupita kiasi. Aidha kuna gari limezidisha 30 tonnes, na baada ya kuona kimeo dereva ameingia mitini. Lakini madereva wengine kama kawaida yao; eti mizani mbovu! Upumbavu mtupu.

Habari hii ni aibu kwa Pinda, tena ni aibu iliyopitiliza aibu ambayo anapaswa kuwa nayo PM. Magufuri hakukosea hata chembe kuondoa nafuu ya 5% ambayo kimsingi ilikuwa ni favor na wafanyabiashara wakaibadilisha na kuiona ni right yao. Kwa upande mwingine, Magufuri sasa wakati umefika ukafahamu tafsiri sahihi ya kujihudhuru! Ikiwa mara kwa mara maamuzi unayofanya huwa yanatenguliwa na wakubwa wako; tafsiri yake ni kwamba wana mashaka na uwezo wako wa maamuzi….wanakuona unamudu sana kazi ya u-foreman kuliko kufanya maamuzi. Hiyo peke yake ni sababu tosha kabisa kukufanya kujihudhuru si kwa sababu umeshindwa kazi au umefanya makosa bali umeshindwa kufanya kazi na wakubwa wako ambao hawaamini katika maamuzi yako!


Mzee wa kufunika kombe mwanaharamu apite!
 
Ndiyo mfumo wa CCM ni rushwa tuu. Malori yanaachiwa yaharibu barabara zetu kwa kisingizio cha uchumi. Reli inahujumiwa na CCM wako kimya. KIsa ni kuwa bila kuhujumu reli, barabara zetu hazitaharibika na rushwa kubwa kubwa katika tenda ya kuzijenga haitakuwepo. Uliona wapi barabara hizihizi zinajengwa upya kila baada ya mwaka mmoja ua miwili?
 
SIO siri, kama kuna jambo ambalo lilini-disappoint kweli kweli ni vile Magufuri alivyokuwa anashambuliwa kila kona na wananchi! Lakini hata hivyo, siwalaumu sana coz' wafanyabiashara wa malori walicheza sana na media, hususani Power Breakfast ya Clouds; waka-manipulate watu na bila kujijua raia tukaingia kichwa kichwa kuwaunga mkono bila kufahamu kwamba tunachezewa akili! Niseme wazi kwamba, huwa namkubali sana GERALD HANDO wa CLouds lakini katika sakata hili nae alitumika vilivyo, ama kwa kujua au kutojua! Huyu Gerald alinikera sana kwenye vipindi vyake!!

Msema hovyo Kibonde ndie pekee aliyekuwa amegundua ghiriba hii ya wafanyabiashara; lakini kwa bahati mbaya nae alishambuliwa kwenye kipindi chake hadi akafunga mdomo na siku zilizofuata ikawa ni nafasi ya POWER BREAKFAST peke yake kueneza propaganda za wafanyabiashara!

Hivi unajua watanzania wengi ni MAJANGA?huwa wanalewa na media sana na kuunga mkono vitu vya ki pum.bavu!Nalia na elimu yetu ndiyo imetufanya hivi!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Siku izi mizani hakuna hela ukiondoka jioni na laki tano au 3 tofauti ma zamani ml 1 jioni mpaka na nusu kila siku tz ni zaidi ya uijuavyo.
 
Kama kuna kipindi nilipata kumdharau na kumchukia kupita kiasi Mheshimiwa Pinda ni pale alipoingilia maamuzi ya John Pombe Magufuri kuhusu suala zima la mizani! Wafanyabiashara wa malori wakacheza na akili ya Watanzania na Watanzania nao bila kujitambua wakawa upande wao na kuona alichofanya Magufuri sio sahihi! Watu wa malori wakafikia hadi kusema eti Tanzania ndiyo nchi pekee inayoruhusu uzito mdogo wakati ukweli ni kwamba Tanzania ndio miongoni mwa nchi zinazoruhusu uzito mkubwa zaidi wa Tani 56. Kenya labda wabadilishe sasa, wao ilikuwa maximum load ni 48 tonnes…..na ikiwa inazidi upande mmoja tu; unakula bonge la faini! Wafabiashara wa Tanzania wakawahadaa Watanzania kiasi cha kutuonesha as if suala la mzigo ku-move na kuegemea kwenye axle moja ni suala la Tanzania peke yake! Upumbavu mwingine ambao Wafanyabiashara waliwadanganya Watanzania na sisi kama mazuzu tukawaunga mkono ni suala la ubovu wa mizani!

Mungu hamfichi mnafiki. Kwa mujibu wa ITV saa 2 usiku huu; Wakala wa Vipimo Arusha ilifanya ukaguzi wa kushitukiza! Magari kibao yamejaza kupita kiasi. Aidha kuna gari limezidisha 30 tonnes, na baada ya kuona kimeo dereva ameingia mitini. Lakini madereva wengine kama kawaida yao; eti mizani mbovu! Upumbavu mtupu.

Habari hii ni aibu kwa Pinda, tena ni aibu iliyopitiliza aibu ambayo anapaswa kuwa nayo PM. Magufuri hakukosea hata chembe kuondoa nafuu ya 5% ambayo kimsingi ilikuwa ni favor na wafanyabiashara wakaibadilisha na kuiona ni right yao. Kwa upande mwingine, Magufuri sasa wakati umefika ukafahamu tafsiri sahihi ya kujihudhuru! Ikiwa mara kwa mara maamuzi unayofanya huwa yanatenguliwa na wakubwa wako; tafsiri yake ni kwamba wana mashaka na uwezo wako wa maamuzi….wanakuona unamudu sana kazi ya u-foreman kuliko kufanya maamuzi. Hiyo peke yake ni sababu tosha kabisa kukufanya kujihudhuru si kwa sababu umeshindwa kazi au umefanya makosa bali umeshindwa kufanya kazi na wakubwa wako ambao hawaamini katika maamuzi yako!

Sio mara ya kwanza watanzania kuchezewa akili.na taratibu Kuna Cku wataweza kupambanua maswala yanayowagusa Kwa akili yao bila kuckiza upande unaohc unaonewa.mfano mzuri ni swala la mgomo wa madaktari;serikali iliwalaghai watanzania Kua madaktari wanagoma ili waongezewe mshahara kitu ambacho kilikua ni cha mwisho ktk vilivokua vnadaiwa Na madaktari.matokeo yake ukienda kutbiwa hosp kubwa ya serikali ukikosa panadol unalalamika!!ugonjwa ambao ungetakiwa utibiwe mtwara inakulazmu kusafiri hadi muhimbili Kwa ukosefu wa vifaa..watanzania tubadlike tunachangia ugumu wa vitu vngi ambavo mwisho wa Cku cc Ndo wahanga.
 
Baadhi ya big fish ndo wamiliki wa magari ya mizigo, na uwepo wa reli bora utawapunguzia ulaji.
Kuna jamaa kwenye daladala nilimsikia akisema ujenzi wa barabara kilomita 1 gharama yake ni sawa na ya utengenezaji wa reli kilometa 6 (wataalamu wanisaidie). reli zingeungania mikoa inayozalisha mazao ya chakula na biashara na mikoa mingine, mfumko wa bei za vyakula ungepungua kwani mizengwe na gharama za usafirishaji vingepungua.

Pinda + Magufuli + JK = CCM aaambao ni wadudu walioua na kuitafuna reli yetu kwa manufaa ya wenye malori, acha waduduwafu wazike waduduwafu wao huku tukichemsha dawa ya kuua wadudu wote walioota magamba na kusafisha nyumba yetu
 
Sheria inaweza kubadilishwa kupitia viongozi wabovu kama Pinda lakini kiongozi anayeweka mbele maslahi ya nchi hawezi kuunga mkono!! Halafu ulivyo-stick kwenye suala la logic sijui ni logic gani unayozumgumzia wewe!! Hoja hapa ni Pinda kutetea upuuzi na jana upuuzi anaotetea umedhihiri bila kujali ikiwa alichoruhusu yeye ni tani 3 na zilizozidishwa ni tani 300!! Wavunja sheria wamepewa kiburi na huyo Pinda wako; kwamba hata siku wakigoma na kutokubali any any additional charge; basi viongozi wasiozingatia sheria kama Pinda wataingilia kati.Hapa hoja ya msingi ni ku-entertain upumbavu; kiongozi makini hawezi ku-entertain upumbavu! Uki-entertain upumbavu matokeo yake ndo hayo watu wanapitiliza hata kile ambacho walitetewa!
Unajua akili zako sio nzuri wewe jibu swali ni kipi kikuu kuliko mwenzake kati ya sheria na watu? kwanini sheria zinatungwa? ku harmonize activities au to disrupt them? Nini mantiki ya kutunga sheria? halafu jungu lako lili base kwenye tani 30 ambazo hazihusiani na pinda hilo nalo unasemaje au mantiki ya jungu lako ni nini hebu funguka; kwani umeambiwa wanaozidisha tani 30 hawabanwi na sheria? usiogelee tu jielekeze kwenye point husika.
 
Unajua akili zako sio nzuri wewe jibu swali ni kipi kikuu kuliko mwenzake kati ya sheria na watu? kwanini sheria zinatungwa? ku harmonize activities au to disrupt them? Nini mantiki ya kutunga sheria? halafu jungu lako lili base kwenye tani 30 ambazo hazihusiani na pinda hilo nalo unasemaje au mantiki ya jungu lako ni nini hebu funguka; kwani umeambiwa wanaozidisha tani 30 hawabanwi na sheria? usiogelee tu jielekeze kwenye point husika.
Naomba tu nikupuuze ndugu yangu manake you've all it take to qualify in the group of "IGNORED USER LIST." By the way, unasemaje kuhusu Gas, akina Mengi na wenzie akina Mafuruki wapewe vitalu, au?
 
Naomba tu nikupuuze ndugu yangu manake you've all it take to qualify in the group of "IGNORED USER LIST." By the way, unasemaje kuhusu Gas, akina Mengi na wenzie akina Mafuruki wapewe vitalu, au?
Daaaa kimombo chako kimejaa tope aisee umesoma shule za kata nini; kwa suala la gesi wapewe kabisa ule ni uporaji wa wazi yani watu watoke kwao mikono mitupu waje wachukue pesa kwenye mabenki yetu halafu wachume rasilimali wapeleke kwao si utaahira huo: si bora serikali ingedhamini wazawa kwenye mabenki tukajichimbia wenyewe wazawa
 
yaani natamani nimuone akiwa uchi...yaani nimekuja mbio nikajua kuna picha ...aaaaghhhh
 
Daaaa kimombo chako kimejaa tope aisee umesoma shule za kata nini; kwa suala la gesi wapewe kabisa ule ni uporaji wa wazi yani watu watoke kwao mikono mitupu waje wachukue pesa kwenye mabenki yetu halafu wachume rasilimali wapeleke kwao si utaahira huo: si bora serikali ingedhamini wazawa kwenye mabenki tukajichimbia wenyewe wazawa
yaani wenzako wanazungumzia kutakak kumilikishwa vitalu vya gesi we unaona maujiko kufahamu kimombo!!! Lakini si nimepatia kidogo; au? mi nilidhani nimepiga kifrenchi; kumbe umekishtukia kwamba kimombo!!! Natisha aisee!
 
sheria zivunjwe kunusuru uchumi? Magufuli is very right, kama sheria zipo zisimamiwe sio maswala ya kunusuru uchumi

Sijui hata unaongea nini. Sheria ndio zinalinda uchumi. Sheria mbovu zinaharibu uchumi
 
Mkuu NasDaz Nimekuelewa vzr, kwamba ukweli unabaki palepale kuwa iwapo gari lilipimwa mara ya kwanza (mzani wa kwanza) na kuwa 8tonnes@Axle = tonnes48 (iwapo gari lina Axles 6), na iwapo itatokea kuwa kuhama kwa mzigo kutikisika kutokana na mwendo na kufika mzani wa pili na Axle 1-6 zina tonnes 6:6:9:9:9:9 hapa tatizo si ubovu wa mzani! ila ni suala la hesabu ya kujumlisha, sasa Pinda inakuwaje? hakuchanganya na akiri zake? alikubali za kuambiwa za upande mmoja tu? labda kama kuna jingine iwapo sisi TZ ndio tulikuwa na uzito wa juu kuliko wengine (EA) na bado wasafirishaji wetu wanapinga
Ndugu yangu,
Si mara zote kwamba kutokea kwa variations kunatokana na kwamba mizani ni mbovu; la hasha! System yenyewe ya upimaji ndiyo mara nyingi huleta variations. Kinachotokea ni kwamba, kama Load Limit ni 56 tonnes (as per Tanzania); hiyo 56 tonnes inakuwa equally distributed kwenye number of axles. Maana yake ni kwamba, ikiwa gari ina 7 axles, hapo maana yake ni kwamba wakati wa kupima hakuna axle inayotakiwa kuzidi 8 tonnes! Sasa ikiwa huko barabarani mlikuwa mnafukuzana to the point mzigo ukaegemea upande mmoja; then it's obvious kule ambako mzigo utaegemea axle weight itazidi hata kama hapo kabla ilikuwa sawa! Kwahiyo wanaposema kuna variation not necessarily kwamba mizani huwa zinakuwa mbovu; no! Lakini hata hivyo, hivyo ndivyo inavyofanyika katika kila nchi duniani....axle weight considered na hakuna suala la +5%!! But all in all, tusisahau kwamba variation kwenye measurement si jambo la ajabu hata kidogo. Ukitoka filling station A na kuweka lita 10 kisha ukaenda station B, it's more likely kutakuwa na variation tu!

Lakini ukija upande mwingine, Tanzania ni miongoni mwa nchi duniani amako maximum load weight ni kubwa sana; yaani hiyo 56 tonnes! Nchi zingine za East African Community ilibidi mwaka jana zibadilishe viwango vyao ili kuendana na hivi vya Tanzania ili kuweza pia ku-facilitate transportation. Before that, Tanzania ilikuwa ndo nchi pekee inayoruhusu uzito mkubwa; coz' Uganda na Burundi wao; and i think na Rwanda ilikuwa 53 tonnes wakati Kenya ilikuwa only 48 tonnes ambazo hata hivyo walisema wasingebadilisha hadi 2015. TANROAD ya Kenya, KeNHA washapelekwa sana Mahakamani na kusababisha migomo ya malori mara kadhaa, lakini waliendelea kukomaa coz' wanafahamu wanachojali wafanyabiashara ni faida tu na si vinginevyo!

Kwa bahati mzuri, wafanyabiashara wa Tanzania wakacheza na akili za Watanzania na watu wakawa upande wao bila kufahamu kwamba ilikuwa ni ghiriba tu.
 
Back
Top Bottom