Arusha wamvua nguo MIzengo Pinda!!

Arusha wamvua nguo MIzengo Pinda!!

Inaelekea kwa Tanzania mtu akifanya mema kwaajili ya taifa nia adui na anaharibu ulaji wa hao wenye roho mbaya. Haiji kichwani mtu anayetetea maslahi ya taifa apigwe vita. Media nyingine zinazoshabikia kuangamizwa kwa taifa, hazifai kabisa, na inafaa wamiliki wa media hizo waone ubaya wao kama wanashabikia kuhujumiwa kwa taifa. Nchi zilizoendelea kama Gewrmany zilisimamia sera hata kama wananchi waliumia kipindi fulani lakini maendeleo yanaonekana, vivyo hivyo kwa nchi zote zilizo serious katika maamuzi kama Angola, Namibia na hata Botwsana. Tanzania mara nyingi kuna watu wanataka umaarufu binafsi bila kujali utaifa. Namshukuru Magufuli kwa kuitetea nchi. Hao wafanyabiashara wanaompiga vita na kushangilia kuharibika kwa barabara ingekuwa nchi za wenzetu angesahau kabisa bisahara na kufilisiwa. Imefikia wakati kuwa na viongozi wenye mapenzi na nchi siyo manufaa binafsi. TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO, TUWASAPOTI HAO WACHACHE WENYE NIA THABITI!
 
Pinda amenusuru loss kiuchumi. Magufuli hakuangalia hilo, yeye katoa maamuzi kirobot robot bila kuangalia pande zote, kisha atoe uamuzi ambao ni balanced ili mambo yaendelee. Unavyoropoka eti mkapaki malori yenu upenuni kwenu hakujua anazungumzia loss kwenye sekta ya uchukuzi asilimia ngapi? Au alifikiri ni vilori viwili vitatu? je Mgufuli alikuwa waziri wa barabara miaka mingapi? Mbona hakuliona hilo ? Na hata baada ya kutoliona haoni ingekuwa busara kukaa nao na kuondoa mapungufu hayo? Hiyo asimilia 5 sio issue. Issue ni hilo lilioonekana Arusha. Huko mezani ndio kuna rushwa kubwa pengine kuliko sehemu nyingine zote nchini maana ni kila siku na kila mizani jamaa wanapokea mlungula ili uzito usioruhusiwa upite. Magufuli ni robot type maana hajui kama waendesha mizani ni janga.
Uchumi hauwezi kunusuriwa kwa kuharibu miuondo mbinu ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi, Magufuli kaona mbali zaidi kiuchumi kuliko huyo ambaye unayemshabikia. Watanzania tunatakiwa kuona mbali zaidi, wenzetu walioendelea hawakubembeleza watu wa aina hiyo ambao wananufaisha ubinafsi badala ya Taifa, ningekuwa mimi waziri husika , hata hayo malori yalipogoma ningeyatoza ushuru wa parking na kusababisha msongamano, tutawabembeleza hao wafanyabiashara ambao wengi wao wanakwepa hata kulipa kodi mpaka lini? Tubadilike kifikra, tutasonga mbele, tukibaki tu kushabikia wakwepa kodi hatotofika mbali. Kama wangekuwa wanalipa kodi sawa kama wafanyakazi basi nadhani tungefaidika sana na kama wanauchungu wa maendeleoa ya nchi wasingepingana na agizo la waziri, mimi nawaona kama wahujumu uchumi, natamani Sokoine angerudi awaonyeshe maana ya uzalendo.
 
Mkuu Mwita Maranya,
Sikatai kwamba kunakuwaga na variations kwenye mizani lakini haiwezekani kwamba kwavile kuna variations basi conclusion hapo ni kwamba hizo mizani ni mbovu (hi indo hoja ya wasafirishaji). Hata wewe leo ukitoka na dumu lako kisha ukaenda kupima lita 10 za diesel kwenye kituo X, kisha ukaenda tena kupima lita 10 kwenye kituo Y; lazima tu utakuta variations between volume from kituo X na kituo Y! Hilo la kwanza, lakini tuje hii hoja yao ya ku-demand 5% subsidy.

Kama wanataka 5% variation subsidy, ambayo kwa lugha ya kawaida ni kwamba ikiwa mzigo wao utakuwa umezidi for a maximum of 5% load weight, basi hiyo 5% itakuwa inatokana nah ii measurement variations but under normal condition, hiyo increase in 5% isingekuwepo! Sasa ikiwa 5% ni kama ina-adjust the increased load weight, ni kwanini wao wanapopakia wasifanye -5% of allowed load weight ambayo hata kama itatokea variation, finally itakuwa ime-hit kwenye maximum gross vehicle weight!!

Kwa upande mwingine, unaweza kuta tatizo sio mizani bali system inayotumika! Kwa bahati mbaya sana, system hii ni kwamba hii gross weight inatakiwa kuwa spread equally over available axles. What does it mean; say lorry lina seven axles na allowed limit ni 56 tonnes! According to this system; no one axle should exceed 8 tonnes! Sasa ikiwa mlikuwa mnafukuzana huko kwa road, kisha mzigo ukaegemea upande mmoja; obvious axle reading ya kule ulikoegemea mzigo itakuwa imezidi! Hata hivyo, hii si kwa Tanzania tu bali nchi nyingi kama sio zote wanafanya hivi!
 
Last edited by a moderator:
Pinda amenusuru loss kiuchumi. Magufuli hakuangalia hilo, yeye katoa maamuzi kirobot robot bila kuangalia pande zote, kisha atoe uamuzi ambao ni balanced ili mambo yaendelee. Unavyoropoka eti mkapaki malori yenu upenuni kwenu hakujua anazungumzia loss kwenye sekta ya uchukuzi asilimia ngapi? Au alifikiri ni vilori viwili vitatu? je Mgufuli alikuwa waziri wa barabara miaka mingapi? Mbona hakuliona hilo ? Na hata baada ya kutoliona haoni ingekuwa busara kukaa nao na kuondoa mapungufu hayo? Hiyo asimilia 5 sio issue. Issue ni hilo lilioonekana Arusha. Huko mezani ndio kuna rushwa kubwa pengine kuliko sehemu nyingine zote nchini maana ni kila siku na kila mizani jamaa wanapokea mlungula ili uzito usioruhusiwa upite. Magufuli ni robot type maana hajui kama waendesha mizani ni janga.
Ndugu yangu, usihadaike na Pinda! Ingawaje ni kweli inaweza kuonekana kwamba Pinda alifanya maamuzi yanayozingatia maslahi ya kiuchumi lakini alichofanya ni more political than economical decision making! Na kama alichofanya ni economic decision making basi alichofanya ni kuangalia maslahi kiuchumi in the SHORT RUN na sio in the LONG RUN! Hizi barabara tusidhani kwamba zinajengwa tu, nazo zinakuwa na maximum load limits. Sasa hebu angalia kama Yule aliyekamatwa jana Arusha, amezidisha 30 Tonnes halafu bado unasema kaangalia economical effects? Gimme a break! Hakuna shughuli za kiuchumi dunaiani zinazoendeshwa pasipo na utaratibu!
 
Ndugu yangu nakubaliana na wewe Kimsingi .Lakini jambo la kujiuliza ni Kwanini ASerikali haitaki kuboresha miundombinu ya RELI ilikuondokana na karaha hii....Hii mitandao ya Barabara zinazojengwa kwa mkopo ni mzigo mkubwa sana kwa wananchi wa tanzania.Pia udhibiti wake ni Mgumu. Mawaziri hawa kwa makusudi wanashiriki kuuwa usafiri wa RELI ambo kimataifa ndiyo usafiri unaotarajiwa kuwa more economic. Tungewekeza kwenye Reli kasheshe zote hizi zisingekuwepo.

Kwa makusudi hata hizi reli mbili (TAZARA na RELI YA KATI) zilizopo zinahujumiwa (YA TANGA ARUSHA NDO HIVYO TENA) nI KWA NINI wafanyakazi wa vitengo vy mizigo hulazimika kuchaji Bei kubwa kusafirisha mzigo kuliko Bei inayochajiwa kwa Gari kwa mzigo wa Uzito husika. Shida kubwa kwa hapa Tanzania ni namna tunavyopanga mipango ya maendeleo utafikiri wote tutakufa kesho...mipango yetu yote ni ya CHEKECHEA TU... Hakunaanayeangali maslhi mapana ya Taifa.

Uliyosema ndugu yangu ni kweli tupu kwamba suluhu hapa ni RELI! Usafiri wa treni ukishakaa sawa basi haya yote yatapungua; sisemi yataisha kabisa kwani hata huko Ulaya bado nao wanatumia Malori hadi kesho!
Hata hivyo, asikudanganye mtu haya mambo magumu sana! Hata kama tutajenga reli bado umuhimu wa barabara utabaki pale pale. Sasa basi, ugumu upo kwamba ni nini kianze kupitia hivi visenti tulivyo navyo au tunavyokopa! Tuanze na ujenzi wa barabara au ujenzi wa reli? Ujenzi wa reli una-promote commerce/trade/production lakini ujenzi wa barabara una-promote social requirements! Economically, ni more rationale kuanza na ujenzi wa reli kwa jili yak u-promote hivyo nilivyotaja lakini hakuna shughuli za kiuchumi zitakazoenda vizuri penye watu wasiopata huduma zao muhimu! Wajerumani waliweza coz' they were not here for people but for commerce; so wasingejali ikiwa watu walipita kwenye makorongo provided wao wanaweza kusafirisha mizigo hadi bandarini! Kwa hizi serikali zinazokaa madarakani kwa vipindi vifupi, itawachukua muda kum-favor producer na kumwacha consumers mwenye wingi wa kura!
 
God forbid Tanzania kupata tena Waziri Mkuu inept kama Mh. Mizengo Pinda.

Mimi huwa nawashangaa hata watu wanaopoteza muda kumsikiliza. Huyu alikuwa anafaa kuendelea kutengeneza chai kwenye ofisi ya Waziri Mkuu huku akisoma mafaili ya Regional Admin and Local Government.

Kwanza ofisi yake inaongoza kwa uozo kwa sababu hawezi kutoa maamuzi magumu ambayo ni jukumu la serikali katika utendaji wake.

The guy is shortchanging Tanzanian.
 
Kama kuna kipindi nilipata kumdharau na kumchukia kupita kiasi Mheshimiwa Pinda ni pale alipoingilia maamuzi ya John Pombe Magufuri kuhusu suala zima la mizani! Wafanyabiashara wa malori wakacheza na akili ya Watanzania na Watanzania nao bila kujitambua wakawa upande wao na kuona alichofanya Magufuri sio sahihi! Watu wa malori wakafikia hadi kusema eti Tanzania ndiyo nchi pekee inayoruhusu uzito mdogo wakati ukweli ni kwamba Tanzania ndio miongoni mwa nchi zinazoruhusu uzito mkubwa zaidi wa Tani 56. Kenya labda wabadilishe sasa, wao ilikuwa maximum load ni 48 tonnes…..na ikiwa inazidi upande mmoja tu; unakula bonge la faini! Wafabiashara wa Tanzania wakawahadaa Watanzania kiasi cha kutuonesha as if suala la mzigo ku-move na kuegemea kwenye axle moja ni suala la Tanzania peke yake! Upumbavu mwingine ambao Wafanyabiashara waliwadanganya Watanzania na sisi kama mazuzu tukawaunga mkono ni suala la ubovu wa mizani!

Mungu hamfichi mnafiki. Kwa mujibu wa ITV saa 2 usiku huu; Wakala wa Vipimo Arusha ilifanya ukaguzi wa kushitukiza! Magari kibao yamejaza kupita kiasi. Aidha kuna gari limezidisha 30 tonnes, na baada ya kuona kimeo dereva ameingia mitini. Lakini madereva wengine kama kawaida yao; eti mizani mbovu! Upumbavu mtupu.

Habari hii ni aibu kwa Pinda, tena ni aibu iliyopitiliza aibu ambayo anapaswa kuwa nayo PM. Magufuri hakukosea hata chembe kuondoa nafuu ya 5% ambayo kimsingi ilikuwa ni favor na wafanyabiashara wakaibadilisha na kuiona ni right yao. Kwa upande mwingine, Magufuri sasa wakati umefika ukafahamu tafsiri sahihi ya kujihudhuru! Ikiwa mara kwa mara maamuzi unayofanya huwa yanatenguliwa na wakubwa wako; tafsiri yake ni kwamba wana mashaka na uwezo wako wa maamuzi….wanakuona unamudu sana kazi ya u-foreman kuliko kufanya maamuzi. Hiyo peke yake ni sababu tosha kabisa kukufanya kujihudhuru si kwa sababu umeshindwa kazi au umefanya makosa bali umeshindwa kufanya kazi na wakubwa wako ambao hawaamini katika maamuzi yako!

Unajua wewe unachekesha sana kwa hiyo unataka Makufuli ajionyeshe anajua kazi kuliko bosi wake? unajua vizuri mfumo wa kutawalana serikalini? halafu unaongea vitu vya ajabu asilimia iliyoruhusiwa haifiki hata tani 3 za ziada sasa huyo aliyezidisha tani 30 kapewa kibali na Pinda? na kama Pinda karuhusu huo mzigo ulikamatwaje? acha chuki binafsi ulitaka nchi ilale chali kwa mgomo? Huyo Makufuli anawaamrisha watu wa malori kwa kuwafokea kama watoto wadogo amewazaa? uliona nchi gani duniani inaendeshwa kwa kiboko? na huyo Makufuli wako ni waziri wa barabara pekee? mbona majengo yanaporomoka na kuuwa watu kibao hatumsikii aking'aka? nani hajui barabara karibia zote zimejengwa chini ya kiwango? huyo ni fisadi tu kauza nyumba za serikali milioni 15 leo wahusika wanaziuza kwa bilioni 15 kabla hata ya kumaliza deni
 
Uchumi hauwezi kunusuriwa kwa kuharibu miuondo mbinu ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi, Magufuli kaona mbali zaidi kiuchumi kuliko huyo ambaye unayemshabikia. Watanzania tunatakiwa kuona mbali zaidi, wenzetu walioendelea hawakubembeleza watu wa aina hiyo ambao wananufaisha ubinafsi badala ya Taifa, ningekuwa mimi waziri husika , hata hayo malori yalipogoma ningeyatoza ushuru wa parking na kusababisha msongamano, tutawabembeleza hao wafanyabiashara ambao wengi wao wanakwepa hata kulipa kodi mpaka lini? Tubadilike kifikra, tutasonga mbele, tukibaki tu kushabikia wakwepa kodi hatotofika mbali. Kama wangekuwa wanalipa kodi sawa kama wafanyakazi basi nadhani tungefaidika sana na kama wanauchungu wa maendeleoa ya nchi wasingepingana na agizo la waziri, mimi nawaona kama wahujumu uchumi, natamani Sokoine angerudi awaonyeshe maana ya uzalendo.

Ndugu yangu kwa taarifa yako simpendi kabisa huyu PM nyambaf hivyo simshabikii hata kidogo. Halafu issue sio kodi bali ni uharibifu wa barabara kwa ajili ya uzito usiokubalika. Hiyo 5% ilikubalika siku nyingi ila watu wanazidisha mizigo na wanapitisha pamoja na hiyo 5%. Wanaopitisha ni watu wa mizani. sasa badala ya kuthibiti mizani unazuia malori ni akili gani hiyo? Hili ndilo aliloangalia Pinda na alikuwa sahihi.
 
Ndugu yangu, usihadaike na Pinda! Ingawaje ni kweli inaweza kuonekana kwamba Pinda alifanya maamuzi yanayozingatia maslahi ya kiuchumi lakini alichofanya ni more political than economical decision making! Na kama alichofanya ni economic decision making basi alichofanya ni kuangalia maslahi kiuchumi in the SHORT RUN na sio in the LONG RUN! Hizi barabara tusidhani kwamba zinajengwa tu, nazo zinakuwa na maximum load limits. Sasa hebu angalia kama Yule aliyekamatwa jana Arusha, amezidisha 30 Tonnes halafu bado unasema kaangalia economical effects? Gimme a break! Hakuna shughuli za kiuchumi dunaiani zinazoendeshwa pasipo na utaratibu!

NassDaz nakubaliana na wewe. Sasa kuzuia malori ni soltution ya long run au? My point is , this trend has been there for many years and probably with Magufulis knowledge. Ukizidisha tani unalipia,Tatizo ni wanaokudai ulipe wanakudai kidogo nyingine wanatia ndani.Sasa tuanzie wapi, kupaki malori au kupakua hao wala rushwa kwenye mizani. Uamuzi wa kuwaambia wasfirishaji wapaki ulikuwa wa kitoto zaidi. He had so many alternatives to reach a prudent decision.
 
Unajua wewe unachekesha sana kwa hiyo unataka Makufuli ajionyeshe anajua kazi kuliko bosi wake? unajua vizuri mfumo wa kutawalana serikalini? halafu unaongea vitu vya ajabu asilimia iliyoruhusiwa haifiki hata tani 3 za ziada sasa huyo aliyezidisha tani 30 kapewa kibali na Pinda? na kama Pinda karuhusu huo mzigo ulikamatwaje? acha chuki binafsi ulitaka nchi ilale chali kwa mgomo? Huyo Makufuli anawaamrisha watu wa malori kwa kuwafokea kama watoto wadogo amewazaa? uliona nchi gani duniani inaendeshwa kwa kiboko? na huyo Makufuli wako ni waziri wa barabara pekee? mbona majengo yanaporomoka na kuuwa watu kibao hatumsikii aking'aka? nani hajui barabara karibia zote zimejengwa chini ya kiwango? huyo ni fisadi tu kauza nyumba za serikali milioni 15 leo wahusika wanaziuza kwa bilioni 15 kabla hata ya kumaliza deni
Ile kuendelea kumuita Makufuli badala ya jina lake halisi inaonesha kwamba unasukumwa na kitu cha ziada! Lakini kama kuchangaza wewe ndo unashangaza...maximum weight limit ni 56 tonnes; so hapa hakuna cha kuzidi tani 3 au 100 coz' hapakuwa na sababu hiyo! Kama maximum weight ni 56 tonnes basi watu lazima wa-comply na hiyo condition, PERIOD!
 
NassDaz nakubaliana na wewe. Sasa kuzuia malori ni soltution ya long run au? My point is , this trend has been there for many years and probably with Magufulis knowledge. Ukizidisha tani unalipia,Tatizo ni wanaokudai ulipe wanakudai kidogo nyingine wanatia ndani.Sasa tuanzie wapi, kupaki malori au kupakua hao wala rushwa kwenye mizani. Uamuzi wa kuwaambia wasfirishaji wapaki ulikuwa wa kitoto zaidi. He had so many alternatives to reach a prudent decision.
Mkuu Mfamaji,
Maghufuri hakuzuia malori kuingia barabarani alichokuwa amefanya yeye ni kuondoa ile nafuu ya 5%! Lakini vilevile kuweka kwamba wanaozidisha mizigo wanalipa faini haina maana kwamba inaruhusiwa kuzidisha mzigo in exchange to kulipia faini; suala la kulipa faini liliwekwa kwa ajili ya ku-discourage uzidishaji wa uzito na sio ku-approve for extra payment. Wakenya wao sheria yao ndo ngumu ile mbaya kuliko yetu; wao first conviction unapigwa faini ya KShs. 200,000/= (about TZS 4,000,000/=) na ukipatikana na kosa kwa mara ya pili, unapigwa KShs. 400,000/-. Tena labda wabadilishe sasa, wao Maximum Load limit up to 2012 ilikuwa only 48 tonnes spreading equally throughout all axels wakati TZ ni 56 tonnes.
 
Last edited by a moderator:
Hivi wakala wa vipimo hahusiki na hizi mizani za TANROADS? yeye ni mizani za sukari tu? je hizi variations zinatokana na nini? na hazirekebishiki?
Ina maana Maghufuli ameshindwa kabisa kuset standard za hizi mizani badala ya kukaa na kuonekana mbabaishaji?
Mkuu NasDaz umeandika ukweli mtupu lakini nataka nikuhakikishie jambo moja tu kwamba weigh bridges zetu zina matatizo makubwa sana. Niliwahi kupata fursa ya kuwa karibu na hao jamaa wa Tanroads kwahiyo ninafahamu matatizo ya mizani zao,Zina variations kubwa sana Kati ya mzani mmoja na mwingine ukipima mzigo huo huo.

KUna siku ilitokea transporter mmoja aligoma kulipa faini mzani wa Kibaha na akawaambia Yuko tayari kujaza gari mafuta aondoke na mtu wa Tanroads Kibaha warudi na gari waipime upya katika mizani zote kuanzia Kibaha,Chalinze,Msata na Himo.
Jamaa wakakubali na zoezi likaanzia Kibaha,baada ya hapo wakaenda Chalinze wakapata vipimo tofauti na walivyopata Kibaha,Kisha wakaenda Msata napo wakapata vipimo tofauti na walivyopata Kibaha na Chalinze ( Gross Vehicle Mass-GVM),na zoezi la kurudia vipimo likaishia hapo Msata.

Kwa uzoefu wangu na mizani za Tanroads Kuna variations kubwa sana baina ya mzani mmoja na mwingine. Kwahiyo provision ya 5% ilikuwa ni fair kabisa kwa wafamyabiashara kwakuwa hata kiutaalamu unapotengeneza machine au mtambo lazima unaweka hiyo provision either plus or minus.
 
Last edited by a moderator:
Wote Pinda na Magufuli wanamakosa japo makosa ya Pinda nimakubwa zaidi kwani hakupaswa kumwanika hadharani waziri wake, Magufuri nae kauli zake zinatia kichefu chefu hata kama anakua anafuata sheria
 
Ile kuendelea kumuita Makufuli badala ya jina lake halisi inaonesha kwamba unasukumwa na kitu cha ziada! Lakini kama kuchangaza wewe ndo unashangaza...maximum weight limit ni 56 tonnes; so hapa hakuna cha kuzidi tani kwa3 au 100 coz' hapakuwa na sababu hiyo! Kama maximum weight ni 56 tonnes basi watu lazima wa-comply na hiyo condition, PERIOD!
Kama logic ya kumuita Makufuli haijakuingia ni wazi hata huo mfumo wa sheria huujui unanitaka nitaje majina ya watu ili iweje. Sheria zimewekwa kuhudumia watu sio watu kuhudumia sheria ndio maana zinarekebishwa na kufutwa kama zinabomoa zaidi ya kujenga wewe umeng'ang'ana tu sheriaaa sheria wakati hata makusudi yake hauko tayari kuyatafakari. Kuhusu asilimia ni kwamba overload ya tani 50 kwa asilimia 5 ni tani mbili na nusu na overload ya tani 56 kwa asilimia hiyohiyo ni tani mbili na kilo mia nane zote hizo ni chini ya tani tatu na hicho ndicho waziri mkuu alichoruhusu kiendelee kuzidishwa anayezidisha juu ya hapo anapambana na sheria kama kawaida. Mimi nahoji mambo wewe unajibu period hiyo maana yake nini kama sio kuishiwa hoja; toa majibu mstari kwa mstari tukusikie unavyobwabwaja.
 
Kama logic ya kumuita Makufuli haijakuingia ni wazi hata huo mfumo wa sheria huujui unanitaka nitaje majina ya watu ili iweje. Sheria zimewekwa kuhudumia watu sio watu kuhudumia sheria ndio maana zinarekebishwa na kufutwa kama zinabomoa zaidi ya kujenga wewe umeng'ang'ana tu sheriaaa sheria wakati hata makusudi yake hauko tayari kuyatafakari. Kuhusu asilimia ni kwamba overload ya tani 50 kwa asilimia 5 ni tani mbili na nusu na overload ya tani 56 kwa asilimia hiyohiyo ni tani mbili na kilo mia nane zote hizo ni chini ya tani tatu na hicho ndicho waziri mkuu alichoruhusu kiendelee kuzidishwa anayezidisha juu ya hapo anapambana na sheria kama kawaida. Mimi nahoji mambo wewe unajibu period hiyo maana yake nini kama sio kuishiwa hoja; toa majibu mstari kwa mstari tukusikie unavyobwabwaja.
Kwa jinsi unavyoniona ni mtu wa kuishiwa hoja? We vp?????/ Nilichokuambia hakuna sababu ya hiyo 5% coz' sheria ni 56 tonnes na hilo la +5% halipo katika sheria! Liliwekwa tu baada ya kuona malalamiko hayaishi lakini sheria ambayo ilipitishwa na bunge ni 56 tonnes bila kujali kuna variations...na hivyo ndivyo ilivyo kwa kila nchi! Hilo la 5% linatoa kwa viongozi wabovu kama huyo unayemtetea! hoja kwamba hiyo 5% haizidi 3 tonnes haina mashiko coz' haitakiwi kuzidi hata hiyo single tonne!

Sheria ndiyo zimewekwa kuhudumiwa watu, na ndio maana kwa mujibu wa sheria mtu hatakiwi kuzidisha 56 tonnes....uzito utakaokuwa spread equally throughout all axles. Pinda ana-prove tu udhaifu wake anapoendelea kuendekeza malalamiko ya wafabiashara wachache ambao kila mwenye akili timamu anafahamu ni utamaduni wao kuvunja sheria!!!
 
Kwa jinsi unavyoniona ni mtu wa kuishiwa hoja? We vp?????/ Nilichokuambia hakuna sababu ya hiyo 5% coz' sheria ni 56 tonnes na hilo la +5% halipo katika sheria! Liliwekwa tu baada ya kuona malalamiko hayaishi lakini sheria ambayo ilipitishwa na bunge ni 56 tonnes bila kujali kuna variations...na hivyo ndivyo ilivyo kwa kila nchi! Hilo la 5% linatoa kwa viongozi wabovu kama huyo unayemtetea! hoja kwamba hiyo 5% haizidi 3 tonnes haina mashiko coz' haitakiwi kuzidi hata hiyo single tonne!

Sheria ndiyo zimewekwa kuhudumiwa watu, na ndio maana kwa mujibu wa sheria mtu hatakiwi kuzidisha 56 tonnes....uzito utakaokuwa spread equally throughout all axles. Pinda ana-prove tu udhaifu wake anapoendelea kuendekeza malalamiko ya wafabiashara wachache ambao kila mwenye akili timamu anafahamu ni utamaduni wao kuvunja sheria!!!
Sasa si utajiona mjinga sana kesho hiyo sheria ikipelekwa bungeni na kuidhinishwa hiyo 5%? au hata 7% allowable load? hitaji limekwishaonekana ni hilo sheria ndio imeanza kuwekwa sawa administratively kufanya maisha yaendelee na mwisho wa siku itarekebishwa kwani tatizo ni nini hatuna haja ya kuaccomodate ukichaa katika uendeshaji serikali. calculation niliyokupa relevance yake ni kuonyesha kiwango kilichoruhusiwa na waziri mkuu kwamba ni less than three tons na hakina uhusiano na hilo jungu lako la tano 30 unalokurupuka nalo; wewe unaiona haina mashiko kwa kuwa hufuati logic.
 
Hivi wakala wa vipimo hahusiki na hizi mizani za TANROADS? yeye ni mizani za sukari tu? je hizi variations zinatokana na nini? na hazirekebishiki?
Ina maana Maghufuli ameshindwa kabisa kuset standard za hizi mizani badala ya kukaa na kuonekana mbabaishaji?
Ndugu yangu,
Si mara zote kwamba kutokea kwa variations kunatokana na kwamba mizani ni mbovu; la hasha! System yenyewe ya upimaji ndiyo mara nyingi huleta variations. Kinachotokea ni kwamba, kama Load Limit ni 56 tonnes (as per Tanzania); hiyo 56 tonnes inakuwa equally distributed kwenye number of axles. Maana yake ni kwamba, ikiwa gari ina 7 axles, hapo maana yake ni kwamba wakati wa kupima hakuna axle inayotakiwa kuzidi 8 tonnes! Sasa ikiwa huko barabarani mlikuwa mnafukuzana to the point mzigo ukaegemea upande mmoja; then it's obvious kule ambako mzigo utaegemea axle weight itazidi hata kama hapo kabla ilikuwa sawa! Kwahiyo wanaposema kuna variation not necessarily kwamba mizani huwa zinakuwa mbovu; no! Lakini hata hivyo, hivyo ndivyo inavyofanyika katika kila nchi duniani....axle weight considered na hakuna suala la +5%!! But all in all, tusisahau kwamba variation kwenye measurement si jambo la ajabu hata kidogo. Ukitoka filling station A na kuweka lita 10 kisha ukaenda station B, it's more likely kutakuwa na variation tu!

Lakini ukija upande mwingine, Tanzania ni miongoni mwa nchi duniani amako maximum load weight ni kubwa sana; yaani hiyo 56 tonnes! Nchi zingine za East African Community ilibidi mwaka jana zibadilishe viwango vyao ili kuendana na hivi vya Tanzania ili kuweza pia ku-facilitate transportation. Before that, Tanzania ilikuwa ndo nchi pekee inayoruhusu uzito mkubwa; coz' Uganda na Burundi wao; and i think na Rwanda ilikuwa 53 tonnes wakati Kenya ilikuwa only 48 tonnes ambazo hata hivyo walisema wasingebadilisha hadi 2015. TANROAD ya Kenya, KeNHA washapelekwa sana Mahakamani na kusababisha migomo ya malori mara kadhaa, lakini waliendelea kukomaa coz' wanafahamu wanachojali wafanyabiashara ni faida tu na si vinginevyo!

Kwa bahati mzuri, wafanyabiashara wa Tanzania wakacheza na akili za Watanzania na watu wakawa upande wao bila kufahamu kwamba ilikuwa ni ghiriba tu.
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Kuna ka kampuni ka mkubwa wetu kana tusemi trela kiasi kidogo tu kama mia nne hivi, sasa makufuri analeta ujuaji bila ku konsult mukubwa ili iweje, ili iweje???!
 
Sasa si utajiona mjinga sana kesho hiyo sheria ikipelekwa bungeni na kuidhinishwa hiyo 5%? au hata 7% allowable load? hitaji limekwishaonekana ni hilo sheria ndio imeanza kuwekwa sawa administratively kufanya maisha yaendelee na mwisho wa siku itarekebishwa kwani tatizo ni nini hatuna haja ya kuaccomodate ukichaa katika uendeshaji serikali. calculation niliyokupa relevance yake ni kuonyesha kiwango kilichoruhusiwa na waziri mkuu kwamba ni less than three tons na hakina uhusiano na hilo jungu lako la tano 30 unalokurupuka nalo; wewe unaiona haina mashiko kwa kuwa hufuati logic.
Sheria inaweza kubadilishwa kupitia viongozi wabovu kama Pinda lakini kiongozi anayeweka mbele maslahi ya nchi hawezi kuunga mkono!! Halafu ulivyo-stick kwenye suala la logic sijui ni logic gani unayozumgumzia wewe!! Hoja hapa ni Pinda kutetea upuuzi na jana upuuzi anaotetea umedhihiri bila kujali ikiwa alichoruhusu yeye ni tani 3 na zilizozidishwa ni tani 300!! Wavunja sheria wamepewa kiburi na huyo Pinda wako; kwamba hata siku wakigoma na kutokubali any any additional charge; basi viongozi wasiozingatia sheria kama Pinda wataingilia kati.Hapa hoja ya msingi ni ku-entertain upumbavu; kiongozi makini hawezi ku-entertain upumbavu! Uki-entertain upumbavu matokeo yake ndo hayo watu wanapitiliza hata kile ambacho walitetewa!
 
Back
Top Bottom