Arusha: Ukikutwa umevaa Suruali ya kubana, Sketi fupi Faini Tsh. 50,000

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Kutokana na kuporomoka kwa maadili hasa kwa vijana katika maeneo mengi nchini, uongozi wa Kijiji cha Olevolosi, Kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru, Mkoa wa Arusha umeweka sheria ndogo mbalimbali na kupitishwa na mkutano mkuu wa kijiji.

Miongoni mwa yaliyopitishwa ni pamoja na kupiga marufuku wasichana au wanawake kuvaa suruali za kubana au sketi fupi 'vimini', kijana wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa na kuacha nywele katikati 'kiduku', kuvaa hereni au kuvaa suruali inayoonyesha makalio na adhabu za makosa hayo ni faini Sh50,000.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa kijiji hicho, Mtendaji wa Kata hiyo ya Kimnyak, Joshua Mollel, aliwasilisha sheria hizo kwa niaba ya mtendaji wa kijiji hicho, ambazo zilipitishwa na mkutano huo.

"Marufuku kwa msichana au mwanamke yoyote kuvaa suruali ya kubana na kuonyesha maungo yake au kimini ukibainika faini yake ni Sh50,000 na kama hauna hapo kuna akina mama walioandaliwa tumeambiwa tuwaletee," amesema.

"Marufuku kwa kijana yoyote wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa,na kuacha katikati ‘kiduku' au kuvaa suruali mlegezo inayoonyesha makalio au kuvaa suruali iliyotobolewa, faini yake ni Sh50,000 na kama huyo kijana hana kuna adhabu nyingine wazee wamependekeza," amesema mtendaji huyo.

Sheria nyingine ni kupiga marufuku kijana wa kiume kuvalia hereni, marufuku kijana mwenye nguvu kutokufanya kazi na atakayeonekana kijiweni asubuhi bila kufanya kazi atatozwa faini Sh50,000, ni kosa kupika au kuuza pombe haramu ya gongo na adhabu yake ni kupelekwa mahakamani na atakayekutwa na anauza pombe muda wa kazi atatoza faini Sh50,000.

Baada ya kusoma mapendekezo hayo ya sheria ndogo hizo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Olevolosi, Emanuel Ngauliva aliuliza wananchi hao walioshiriki kikao hicho endapo wanapitisha sheria hizo, ambapo wananchi hao waliridhia na kuzipitisha kama sheria ndogo.

"Imepita kwa kishindo kuanzia leo ukikamatwa na makosa hayo utapewa akaunti namba utaenda kuweka fedha hizo na kuna kamati husika itafanya hiyo kazi. Kama kuna aliyevaa suruali hapa tuanze kufanya naye kazi hapa kama kuna kijana amenyoa kiduku au amevaa hereni tufanyie kazi hapa na tutakuwa na sungusungu wanapita katika vitongoji kukagua," amesema.

Mmoja wa wananchi hao, Olariv Robert amesema yeye ni miongoni mwa walioshirikiana na viongozi kuunda sheria hizo ndogo kufuatilia matukio yaliyotokea kijijini hapo ya vijana waliouawa kwa kudaiwa kuiba na kuwa waliona hilo limesababishwa na maadili kuporomoka.

"Uongozi wa kijiji na wazee wa ukoo wakakubalia sheria ndogondogo zitumike na sisi kama wananchi tumekutana kupitisha jamii irudi katika mstari wa mbele," amesema.

Naye Lily Lazaro amesema wanaamini sheria hizo zinasaidia kubadili maadili kwa jamii hasa watoto.

Aidha kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima imepongeza jitihada za kijiji hicho kutunga sheria ndogo hizo zitakazowaongoza kukabiliana na mmomonyoko wa maadili.

Amesema kuwa changamoto ya mmomonyoko wa maadili imezidi kuchukua sura mpya kila siko katika jamii, huku Serikali kwa kushirikiana na wadau ikifanya jitihada mbalimbali kukabiliana na hali hiyo ikiwemo programu zinaziratibiwa na wizara hiyo za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kwa lengo la kuhakikisha wanakuwa katika misingi bora ya maadili mema.

"Hatua hiyo ni kubwa kwa jamii yetu kuamua yenyewe kutunga sheria zao kuhusu maadili, kwani kila wakati mmekua mkitoa wito kwa viongozi hasa wa mamlaka za serikali za mitaa kubeba ajenda ya kusaidia jamii kwenda mbele hasa katika maadili, fursa za kiuchumi na kupinga ukatili," imesema taarifa hiyo.

MWANANCHI
 
Kutokana na kuporomoka kwa maadili hasa kwa vijana katika maeneo mengi nchini, uongozi wa Kijiji cha Olevolosi, Kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru, Mkoa wa Arusha umeweka sheria ndogo mbalimbali na kupitishwa na mkutano mkuu wa kijiji...
Ushamba unawasumbua, pamoja na kuvaa vizuri tumegundua nini cha ajabu kuwazidi wazungu wakaa uchi
 
Kutokana na kuporomoka kwa maadili hasa kwa vijana katika maeneo mengi nchini, uongozi wa Kijiji cha Olevolosi, Kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru, Mkoa wa Arusha umeweka sheria ndogo mbalimbali na kupitishwa na mkutano mkuu wa kijiji.

Miongoni mwa yaliyopitishwa ni pamoja na kupiga marufuku wasichana au wanawake kuvaa suruali za kubana au sketi fupi 'vimini', kijana wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa na kuacha nywele katikati 'kiduku', kuvaa hereni au kuvaa suruali inayoonyesha makalio na adhabu za makosa hayo ni faini Sh50,000.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa kijiji hicho, Mtendaji wa Kata hiyo ya Kimnyak, Joshua Mollel, aliwasilisha sheria hizo kwa niaba ya mtendaji wa kijiji hicho, ambazo zilipitishwa na mkutano huo.

"Marufuku kwa msichana au mwanamke yoyote kuvaa suruali ya kubana na kuonyesha maungo yake au kimini ukibainika faini yake ni Sh50,000 na kama hauna hapo kuna akina mama walioandaliwa tumeambiwa tuwaletee," amesema.

"Marufuku kwa kijana yoyote wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa,na kuacha katikati ‘kiduku' au kuvaa suruali mlegezo inayoonyesha makalio au kuvaa suruali iliyotobolewa, faini yake ni Sh50,000 na kama huyo kijana hana kuna adhabu nyingine wazee wamependekeza," amesema mtendaji huyo.

Sheria nyingine ni kupiga marufuku kijana wa kiume kuvalia hereni, marufuku kijana mwenye nguvu kutokufanya kazi na atakayeonekana kijiweni asubuhi bila kufanya kazi atatozwa faini Sh50,000, ni kosa kupika au kuuza pombe haramu ya gongo na adhabu yake ni kupelekwa mahakamani na atakayekutwa na anauza pombe muda wa kazi atatoza faini Sh50,000.

Baada ya kusoma mapendekezo hayo ya sheria ndogo hizo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Olevolosi, Emanuel Ngauliva aliuliza wananchi hao walioshiriki kikao hicho endapo wanapitisha sheria hizo, ambapo wananchi hao waliridhia na kuzipitisha kama sheria ndogo.

"Imepita kwa kishindo kuanzia leo ukikamatwa na makosa hayo utapewa akaunti namba utaenda kuweka fedha hizo na kuna kamati husika itafanya hiyo kazi. Kama kuna aliyevaa suruali hapa tuanze kufanya naye kazi hapa kama kuna kijana amenyoa kiduku au amevaa hereni tufanyie kazi hapa na tutakuwa na sungusungu wanapita katika vitongoji kukagua," amesema.

Mmoja wa wananchi hao, Olariv Robert amesema yeye ni miongoni mwa walioshirikiana na viongozi kuunda sheria hizo ndogo kufuatilia matukio yaliyotokea kijijini hapo ya vijana waliouawa kwa kudaiwa kuiba na kuwa waliona hilo limesababishwa na maadili kuporomoka.

"Uongozi wa kijiji na wazee wa ukoo wakakubalia sheria ndogondogo zitumike na sisi kama wananchi tumekutana kupitisha jamii irudi katika mstari wa mbele," amesema.

Naye Lily Lazaro amesema wanaamini sheria hizo zinasaidia kubadili maadili kwa jamii hasa watoto.

Aidha kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima imepongeza jitihada za kijiji hicho kutunga sheria ndogo hizo zitakazowaongoza kukabiliana na mmomonyoko wa maadili.

Amesema kuwa changamoto ya mmomonyoko wa maadili imezidi kuchukua sura mpya kila siko katika jamii, huku Serikali kwa kushirikiana na wadau ikifanya jitihada mbalimbali kukabiliana na hali hiyo ikiwemo programu zinaziratibiwa na wizara hiyo za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kwa lengo la kuhakikisha wanakuwa katika misingi bora ya maadili mema.

"Hatua hiyo ni kubwa kwa jamii yetu kuamua yenyewe kutunga sheria zao kuhusu maadili, kwani kila wakati mmekua mkitoa wito kwa viongozi hasa wa mamlaka za serikali za mitaa kubeba ajenda ya kusaidia jamii kwenda mbele hasa katika maadili, fursa za kiuchumi na kupinga ukatili," imesema taarifa hiyo.

MWANANCHI
Hao ni wajinga tu ushindwe kulea kijana wako vizuri alafu uje uweke faini watu wanafikiri na makalio sio bure
 
Kutokana na kuporomoka kwa maadili hasa kwa vijana katika maeneo mengi nchini, uongozi wa Kijiji cha Olevolosi, Kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru, Mkoa wa Arusha umeweka sheria ndogo mbalimbali na kupitishwa na mkutano mkuu wa kijiji.

Miongoni mwa yaliyopitishwa ni pamoja na kupiga marufuku wasichana au wanawake kuvaa suruali za kubana au sketi fupi 'vimini', kijana wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa na kuacha nywele katikati 'kiduku', kuvaa hereni au kuvaa suruali inayoonyesha makalio na adhabu za makosa hayo ni faini Sh50,000.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa kijiji hicho, Mtendaji wa Kata hiyo ya Kimnyak, Joshua Mollel, aliwasilisha sheria hizo kwa niaba ya mtendaji wa kijiji hicho, ambazo zilipitishwa na mkutano huo.

"Marufuku kwa msichana au mwanamke yoyote kuvaa suruali ya kubana na kuonyesha maungo yake au kimini ukibainika faini yake ni Sh50,000 na kama hauna hapo kuna akina mama walioandaliwa tumeambiwa tuwaletee," amesema.

"Marufuku kwa kijana yoyote wa kiume kusuka nywele au kunyoa pembezoni mwa kichwa,na kuacha katikati ‘kiduku' au kuvaa suruali mlegezo inayoonyesha makalio au kuvaa suruali iliyotobolewa, faini yake ni Sh50,000 na kama huyo kijana hana kuna adhabu nyingine wazee wamependekeza," amesema mtendaji huyo.

Sheria nyingine ni kupiga marufuku kijana wa kiume kuvalia hereni, marufuku kijana mwenye nguvu kutokufanya kazi na atakayeonekana kijiweni asubuhi bila kufanya kazi atatozwa faini Sh50,000, ni kosa kupika au kuuza pombe haramu ya gongo na adhabu yake ni kupelekwa mahakamani na atakayekutwa na anauza pombe muda wa kazi atatoza faini Sh50,000.

Baada ya kusoma mapendekezo hayo ya sheria ndogo hizo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Olevolosi, Emanuel Ngauliva aliuliza wananchi hao walioshiriki kikao hicho endapo wanapitisha sheria hizo, ambapo wananchi hao waliridhia na kuzipitisha kama sheria ndogo.

"Imepita kwa kishindo kuanzia leo ukikamatwa na makosa hayo utapewa akaunti namba utaenda kuweka fedha hizo na kuna kamati husika itafanya hiyo kazi. Kama kuna aliyevaa suruali hapa tuanze kufanya naye kazi hapa kama kuna kijana amenyoa kiduku au amevaa hereni tufanyie kazi hapa na tutakuwa na sungusungu wanapita katika vitongoji kukagua," amesema.

Mmoja wa wananchi hao, Olariv Robert amesema yeye ni miongoni mwa walioshirikiana na viongozi kuunda sheria hizo ndogo kufuatilia matukio yaliyotokea kijijini hapo ya vijana waliouawa kwa kudaiwa kuiba na kuwa waliona hilo limesababishwa na maadili kuporomoka.

"Uongozi wa kijiji na wazee wa ukoo wakakubalia sheria ndogondogo zitumike na sisi kama wananchi tumekutana kupitisha jamii irudi katika mstari wa mbele," amesema.

Naye Lily Lazaro amesema wanaamini sheria hizo zinasaidia kubadili maadili kwa jamii hasa watoto.

Aidha kupitia taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima imepongeza jitihada za kijiji hicho kutunga sheria ndogo hizo zitakazowaongoza kukabiliana na mmomonyoko wa maadili.

Amesema kuwa changamoto ya mmomonyoko wa maadili imezidi kuchukua sura mpya kila siko katika jamii, huku Serikali kwa kushirikiana na wadau ikifanya jitihada mbalimbali kukabiliana na hali hiyo ikiwemo programu zinaziratibiwa na wizara hiyo za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kwa lengo la kuhakikisha wanakuwa katika misingi bora ya maadili mema.

"Hatua hiyo ni kubwa kwa jamii yetu kuamua yenyewe kutunga sheria zao kuhusu maadili, kwani kila wakati mmekua mkitoa wito kwa viongozi hasa wa mamlaka za serikali za mitaa kubeba ajenda ya kusaidia jamii kwenda mbele hasa katika maadili, fursa za kiuchumi na kupinga ukatili," imesema taarifa hiyo.

MWANANCHI


Huko sio Arusha, ni vijijini.
 
Jamhuri ya ovyo; limtu linaamka linajiamulia tu; no kufuata sheria linajiamulia tu na umaskini wetu Upo pale pale; hawa watu bila kuchinja mmoja kwa mmoja baada ya mwingine no change will come
 
Hawataweza.
Hawataweza ng'oo
Huo muda Kwanza wametoa wapi wa kujadili mavazi ya mtu hizi ni dalili za kukosa Kazi za kufanya..
Maisha yakikaza hata muda wa kuvaa hovyo hawawez kuwaza
Hawataweza?
Hizo adhab zipo siku nyingi sana na zinatekelezwa kikamilifu ,tena huwa inatumika hiyo adhabu nyingine ambayo haijawekwa wazi wamesema tu kuna adhabu imependekezwa, ukitaka kuijua wewe ni wakiume nenda ukiwa umesuka na umevaa hereni utarudisha ushahidi mzuri kuwa wameweza au hawajaweza
 
Back
Top Bottom