Sehemu ya mahojiano na Wakili wa utetezi, Moses Mahuna ilikuwa hivi.
Mahuna: Kwanini ulipopigiwa simu uende dukani kwako hukwenda.
Shahidi: Nilisikia mabishano pale dukani ndio nikapata hofu.
Mahuna: Je? Baada ya tukio hilo uliliripoti polisi
Shahidi: Hapana.
Wakili Dancon Oola: Una uthibitisho gani kuwa Sabaya na wenzake waliiba Sh 2,769,000 milioni.
Shahidi: Niliwaona kwenye CCTV camera
Oola: Je wewe uliamini vipi kama wao ndio wameiba?
Shahidi: Niliambiwa na Noman Jasin.
Wakili: Je uliripoti polisi?
Shahidi: Sijaripoti lakini niliandika barua TRA
Wakili: Unasema Februari 17 ulirudi Arusha na kuipeleka familia Kenya, Je? Ulipima Covid maana siku hiyohiyo umetoka Simanjiro ulikwenda Nairobi.
Shahidi: Hapana.
Wakili Chavula aliieleza Mahakama kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na mashitaka matatu ya unyang'anyi wa kutumia silaha Sabaya na wenzake.
NB. Uongo hauishi milele