Arusha na CCM

Arusha na CCM

magufuli hakuwa onekana bungeni akipambana na mafisadi kama olesendeka. tatizo letu ni mafisadi! mheshimiwa alishasema aeakamatiki na akaomba waludishe pesa!!. tunataka mtu atakae wavalisha mafisadi kabtura mtaani anaweza? timu yake imewashindwa. ila timu ya ukawa ndio inamachungu na mafisadi adi mate yanawamwagika! timu ukawa yote ndio inawaweza na wao wanajua. ukawa ndio abali ya jiji. na taifa.
 
magufuli hakuwa onekana bungeni akipambana na mafisadi kama olesendeka. tatizo letu ni mafisadi! mheshimiwa alishasema aeakamatiki na akaomba waludishe pesa!!. tunataka mtu atakae wavalisha mafisadi kabtura mtaani anaweza? timu yake imewashindwa. ila timu ya ukawa ndio inamachungu na mafisadi adi mate yanawamwagika! timu ukawa yote ndio inawaweza na wao wanajua. ukawa ndio abali ya jiji. na taifa.

Huyo Magufuli naona vimada wataongezeka safari hii na watajengewa maghorofa kuliko yule wa awali.
 
Naomba kudeclare interest. Mimi siamini kuwa tutapata rais bora toka CCM hata wakimteua nani. Ila naona kitendo cha kumtema Lowassa na wakifanikiwa kumtema Membe, wapinzani tutakuwa na kazi kweli kweli. Watakaobaki wachache ndani ya CCM watakuwa wamoja na wakichanganya na nguvu ya dola na watendaji wakuu wa ngazi zote serikalini CCM watapata ushindi mkubwa kwa kutumia kura na bao la mkono.

Lowasa hatathubutu kuhama chama maana atapelekewa bill ya kodi ya michango yoote aliyopokea kutoka kwa marafiki zake (Kumbuka waliopata hela ya escrow walidaiwa kodi). Pili, Mawaziri wakuu wanaotakiwa kupata marupurupu ya kustaafu ni wale waliostaafu na sii waliojiuzulu. Lowasa alijiuzulu na si alistaafu. Kama atathubutu kuingia chama kingine haya marupurupu yatakatwa.

Sababu nyingine ni kuwa Watanzania ni wepesi kusahau. Baada ya wiki moja utasikia wale wale waliokuwa kindaki ndaki team lowasa watakuwa kindaki ndaki wa mgombea atakayeteuliwa na jina Lowasa litakuwa limefutika midomoni mwao.

Kwa maamuzi haya ya CCM utashangaa upinzani tusipokuwa makini tutapoteza hata baadhi ya majimbo tulonayo.

Hahahaaa bora we umejionea mbali...
 
Acheni ubaguzi wenu wa ukanda mbona kina Mwakyembe, Prof Mwandosya wamekatwa pia hamna waliolalamika kuwa kanda yao inabaguliwa.

Kuna makabila yana haki ya kulalamika yanatengwa lakini siyo nyinyi wa kaskazini idara zote za serikali, mashirika ya umma, wizara nyingi tu mmejazana huko bado mnalalamika daah!!.

Ndiyo maaana mnataka kuanzisha taifa lenu la kaskazini mlivyokuwa wabaguzi.

Mawaziri wakuu wangapi wametoka kaskazini au nyie mnataka rais tu.

ritz msumari huo ushakuchoma nyuma mbele
 
Magufuli anafaa na miongoni mwa wachapakaz ndan ya serikali wakimchukia huyo ntawaita moja kwa moja wabinafsi labda wapitishe hao wake zao! akipita magufuli mechi itakuwa tamu sana ya slaa na magufuli kwan haitotabilika

Ushindi ni hata kwa bao la mkono
 
Hayo ni mawazo ya kujidanganya,ccm mmesha buuugi sana

Siamini na sitakaa niamini kuwa CCM wanaweza wakatupa Rais mzuri. Ila kitendo chao cha kuwaondoa wenye makundi makubwa na uadui, kinawafanya wawe wamoja na sasa vyama vya upinzani kazi imekuwa ngumu zaidi. CCM wakiwa na umoja wanaweza kutumia mbinu zote hata kufunga goli kwa mkono. Wale mamluki woote waliokuwa wanapandikizwa kwa wagombea wengine sasa wanahamishiwa vyama vya upinzani hasa vinavyounda UKAWA na hivyo vurugu ndani ya vyama hivyo itaanza.
Huwa waswahili tunasema, Adui Muombee njaa. maelewano yalikuwemo ndani ya UKAWA kwa kiasi kikubwa kwa sababu CCM walikuwa wanalumbana. Sasa wameelewana na Lowasa apende asipende lazima ampigie kampeni mgombea anayekuja. Nguvu yoote CCM sasa inahamishiwa kuiumiza UKAWA. Ni muhimu sasa Ukawa kuaminiana na kuwa makini.
 
Acheni ubaguzi wenu wa ukanda mbona kina Mwakyembe, Prof Mwandosya wamekatwa pia hamna waliolalamika kuwa kanda yao inabaguliwa.

Kuna makabila yana haki ya kulalamika yanatengwa lakini siyo nyinyi wa kaskazini idara zote za serikali, mashirika ya umma, wizara nyingi tu mmejazana huko bado mnalalamika daah!!.

Ndiyo maaana mnataka kuanzisha taifa lenu la kaskazini mlivyokuwa wabaguzi.

Mawaziri wakuu wangapi wametoka kaskazini au nyie mnataka rais tu.


Mtoto wa raisi ndugu Ridhiwan kupitia umoja wao wa vijana UVCCM walishatoa tamko na juzi nae kalirudia kwa uwazi dhahiri bila kificho kuwa "Raisi wa nchi hii hatatoka kaskazini". Kauli hii pamoja na zilizotangulia ni nani ktk CCM alizikemea kaa dhati mkuu ?.
 
Huyo Magufuli naona vimada wataongezeka safari hii na watajengewa maghorofa kulikot yule wa awali.
Sawa si dume? si tunachotaka ni kaz tu👳👍✌ hata ww hatukujui tabia zako anazijua mungu
 
kwa pigo hili sidhani kama ccm ina kitu imebakiza arusha na kilimanjaro nadhani ndio wamejifukuza kabisa hata kile kidgo kilicho kuwa kimebaki wamepoteza, ngome imekuwa ya ukawa moja kwa moja.

bavicha acha kujidanganya ccm sio kama chadema!
Ccm itapata kura za kutosha huko na lowasa atatoa support....! Kilio cha samaki hiki..
 
Halafu hao mawaziri wakuu walotoka huko wooote wamevuruga tu, wana maekari ya kutosha tu, tanzanite inapatikana kwao lkn nchi fulan ndio inaongoza kwa kuiuza km hilo tu mmeshindwa kusimamia ndio tuwape nchi thubutu, kifupi hamwezi kuongoza nenden rombo kwanza mtulize kashfa ya pombe haramu ndio mje tuongee

Maekari mbona wanayo hapa chuga kila kiongozi wenu wa CCM.

Hiyo tanzanite mbona anamiliki JK kupitia mtoto wake.
 
Duuu jamaa angeshinda nadhani iliyokuwa kamati teule ya richmond wangekimbia nchi maana hali ingekuwa mbaya sana kwao
 
Kwa pigo hili sidhani kama CCM ina kitu imebakiza Arusha na Kilimanjaro nadhani ndio wamejifukuza kabisa hata kile kidgo kilicho kuwa kimebaki wamepoteza, ngome imekuwa ya UKAWA moja kwa moja.

Wewe ni punda wa nyerere au punda wa ccm manji?
 
Unadhani c.c.m ni ya lowassa? na mang'ombe yake c.c.m ni kama mto rufiji haikauki wanachama nchi nzima
 
Wakati watu wanaongelea Rais wa Tanzania, rais msafi mwenye uwezo wa kukemea rushwa wao wanaongea rais wa kaskazini bila kujali hata kama ni mla rushwa, this is too low!

Mkuu Mimi nipo huku kaskazini lakini lowasa nilikuwa namuona Kama shetani.
 
Mkuu umemiumiza tena kidonda kilichotaka kupona, hakika nimemchukia Kikwete sana, ni mnafiki asiye na hata chembe ya aibu.Bora hata angempitisha kwenye tano bora...ila kwa kujua kwakwe Lowassa anakubalika ikabidi amchinjie baharini.
Hata hivyo nimemkubali sana mwanaume Lowassa kwa ujasiri wake, laiti ningekua mimi nisingeweza kujongea meza kuu kwa dhuluma ile.

Mkuu, mimi nilikuwa na rafiki mswahili nawajua walivyo. wakati anashida atakunyenyekea kweli. Ila mambo yake yakishakamilika tu atakuona takataka. Baada ya kumgundua, nilishasema maisha siyo lazima uwe na rafiki. Unaweza kuishi bila rafiki na mambo yako yakaenda tu. Waswahili siyo watu mkuu. Wewe angalia tokea 1995, Kikwete alikuwa na hela gani kukodi ndege wakati ule kama siyo Lowassa kumbeba? 2005, Lowassa kamuachia aanze yeye na kampa support 100% bila kinyongo. Leo hii jamaa kamgeuka kataka kumpa ndugu yake. Ila Mungu alivyowaajabu hiyo imeshindikana. Make mpango uliokuwepo ni Membe kuchukuwa na Lazima angeingia tu madarakani. Mke wa Kikwete si atagombea Lindi Mjini? huyo angekuwa waziri mkuu, Riziwani Waziri wa nishati na Madini. Baada ya miaka 10 Riziwani ndo angekuwa mgombea wa Uraisi kupitia CCM. Sasa Mungu naye kamuumbua mnafiki mipango yake imebuma
 
Mtoto wa raisi ndugu Ridhiwan kupitia umoja wao wa vijana UVCCM walishatoa tamko na juzi nae kalirudia kwa uwazi dhahiri bila kificho kuwa "Raisi wa nchi hii hatatoka kaskazini". Kauli hii pamoja na zilizotangulia ni nani ktk CCM alizikemea kaa dhati mkuu ?.
Hiyo kauli unayosema ndiyo kauli ya chama? Ngoja nikukumbushe Nassari alivyosema Chadema wataanzisha taifa la kaskazini huo ndiyo msimamo wa Chadema?
 
Kwa pigo hili sidhani kama CCM ina kitu imebakiza Arusha na Kilimanjaro nadhani ndio wamejifukuza kabisa hata kile kidgo kilicho kuwa kimebaki wamepoteza, ngome imekuwa ya UKAWA moja kwa moja.

kama rizi1 na wengine wanaapa raisi hatakaa atoke kaskazini ni inatubidi sisi wa kaskazini kikifutilie mbali chama chao maana ni cha kibaguzi.
 
Hii ndo tabia ya watu wa Kaskazini.Hata wale tuliokuwa nao opp.walishatuhama na kwenda kwa Lowasa.Nafuu amepgwa chini vingnevyo Dr angepata wakati mgumu huko Kaskaz.Lakn hii tabia ni mbaya sana na tuelewa kuwa hali hii ikiendelea, itawafanya tukose hata kwingne.Karibu 35% ya Watz wanapatikana kanda ya ziwa.Chadema kwa mfano tuna wabunge wengi kanda ya ziwa kuliko hata huko Kaskaz.

Huyo si anaandika tu nae ilimradi apate cha kusimulia kwamba ameanzisha uzi JF. Tusipoangalia ukabila utatutafuna.
 
Back
Top Bottom