Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 10,414
- 18,438
Kijana mmoja ajulikanae Kwa jina la jimmy au almaarufu Baba Adriana, mwenye umri wa miaka 30 mkazi wa Lemara ameokolewa akitaka kujinyonga baada ya mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 6 aliyekuwa nae kwenye pikipiki yake kusombwa na maji wakati wakivuka mto.
Tukio Hilo limetokea njiro mtaa wa Dabo B ambapo mvua kubwa na ya aina yake ilinyesha jioni ya jumapili jijini Arusha na hivyo kusababisha mito kufurika maji na barabara kujaa maji na baadhi ya mitaa maji kuingia ndani,.
jimmy baada ya kutoka katika kazi zake alipitia watoto wake walipokuwa wameshinda Kwa bibi Yao ili aende nao nyumbani lakini mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 4 alikataa katakata kuondoka , na hivyo kuondoka na mtoto mkubwa ambae ndo huyo Adriana huku mvua ikinyesha walivyofika sehemu yenye mto ili avuke daraja baadhi ya watu akiwemo mtoto Wake(mtoto alimwambia baba tusivuke maji ni mengi haya) walimkataza Kwa kumwambia kuwa maji ni mengi hivyo asivuke daraja lakini jimmy hakusikia.
Akiwa darajani maji yalimzidi nguvu mtoto akaanguka kwenye pikipiki na kubebwa na maji. Hadi Leo mtoto hajapatikana Bali begi lenye madaftari na nguo zake TU ndio vimepatikana, ila mwili Bado.
Baada ya tukio Hilo Jimmy alichanganyikiwa na hivyo kwenda kujitundika kitanzi baada ya watu kuingia ndani na kumkuta akining'inia ndipo walipomuokoa na kumfunga kamba miguuni na mikononi baada ya akili kumruka.
Hadi Sasa Bado Hali ya Baba huyo haijawa sawa na Bado kafungwa kamba miguuni na mikononi ili asijidhuru.
Update...........
Hatimae yule mtoto aliyesombwa na maji Fuvu lake limepatikana Leo tarehe 11 yaani siku ya nane baada ya mtoto huyo ajulikanae Kwa jina la Andriana mwenye umri wa miaka sita kusombwa na maji wiki iliyopita wakati akiwa kwenye pikipiki yeye na babayake.
Ni baada ya watu waliokuwa wakichunga ng'ombe kuona fisi akimalizia kula kitu kama fuvu la binadamu, ndipo walipomfukuza fisi huyo na kukuta ni kichwa Cha mtoto kimebakia sehemu kidogo TU ya kichwa huku ubongo nao ukiwa umeliwa.
Tukio Hilo limetokea njiro mtaa wa Dabo B ambapo mvua kubwa na ya aina yake ilinyesha jioni ya jumapili jijini Arusha na hivyo kusababisha mito kufurika maji na barabara kujaa maji na baadhi ya mitaa maji kuingia ndani,.
jimmy baada ya kutoka katika kazi zake alipitia watoto wake walipokuwa wameshinda Kwa bibi Yao ili aende nao nyumbani lakini mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 4 alikataa katakata kuondoka , na hivyo kuondoka na mtoto mkubwa ambae ndo huyo Adriana huku mvua ikinyesha walivyofika sehemu yenye mto ili avuke daraja baadhi ya watu akiwemo mtoto Wake(mtoto alimwambia baba tusivuke maji ni mengi haya) walimkataza Kwa kumwambia kuwa maji ni mengi hivyo asivuke daraja lakini jimmy hakusikia.
Akiwa darajani maji yalimzidi nguvu mtoto akaanguka kwenye pikipiki na kubebwa na maji. Hadi Leo mtoto hajapatikana Bali begi lenye madaftari na nguo zake TU ndio vimepatikana, ila mwili Bado.
Baada ya tukio Hilo Jimmy alichanganyikiwa na hivyo kwenda kujitundika kitanzi baada ya watu kuingia ndani na kumkuta akining'inia ndipo walipomuokoa na kumfunga kamba miguuni na mikononi baada ya akili kumruka.
Hadi Sasa Bado Hali ya Baba huyo haijawa sawa na Bado kafungwa kamba miguuni na mikononi ili asijidhuru.
Update...........
Hatimae yule mtoto aliyesombwa na maji Fuvu lake limepatikana Leo tarehe 11 yaani siku ya nane baada ya mtoto huyo ajulikanae Kwa jina la Andriana mwenye umri wa miaka sita kusombwa na maji wiki iliyopita wakati akiwa kwenye pikipiki yeye na babayake.
Ni baada ya watu waliokuwa wakichunga ng'ombe kuona fisi akimalizia kula kitu kama fuvu la binadamu, ndipo walipomfukuza fisi huyo na kukuta ni kichwa Cha mtoto kimebakia sehemu kidogo TU ya kichwa huku ubongo nao ukiwa umeliwa.