Online nimekuta same complains kwamba timu za kaliba ya Westham, Crystal Palace, Brentford, Wolves n.k. zinapaki basi dhidi ya Arsenal pekee.
Goli la 3 la City dhidi ya Westham Arsenal ya sasa hatuwezi kulipata kwakua tumeshakua kwenye positions za vile mara nyingi na atakayepata mpira akili yake ya kwanza ni kusubiri wenzake waje zianze sideways passes na back passes.
Goli la 1 na la 2 la City dhidi ya Westham hatuwezi kulipata kwakua hatufanyi high pressing siku hizi. Tumefanya high pressing dhidi ya Spurs na matokeo yalikuaje?
Kwanini tunahofia kufanya high pressing wakati tumeshacheza hivyo? Hapo sijui na ni maamuzi ya kocha jinsi tunavyocheza kama maroboti yasiyotaka kuacha kucheza yalivyokua programmed.
Kuna mashabiki wanasema shida yetu ni kwamba "We don't take risks" hapa sasa ndiyo inamaanisha hatuwezi kupata goli la 3 la City dhidi ya wapaki basi. Una Midfield ambayo haibaki nje ya 18 kusubiri looseballs, una wings zisizofosi ku-cut in na kushoo, una CBs zisizopiga long balls, una LBs wawili ila ni mmoja tu anajaribu ku-overlap na bado winger hapeleki pasi akipeleka ni pasi ya kifala, una AM anayegawa mipira upande wa kulia na kurudisha mpira nyuma na hapigi through passes kwa ST wake.
Mechi dhidi ya Everton tuna shots 13, on target ni 2, katika hizo 2 moja ni ile penalty. For 96 minutes huo ndiyo upuuzi Arsenal inayotaka makombe ilikua inaufanya mule ndani. Na hii ni timu ambayo mechi ya mwisho kabla ya hii ilicheza siku 5 nyuma.
Hakuna kisingizio cha uchovu bali inamaanisha akili ya mwisho ni hiyo. Tukaambiwa hawa watu walikasirika kilichotokea game ya Wolves mpaka wakaambiana ukweli n kujitathmini. Halafu next game, siku tano mbele, unarudia ujinga uleule.
Second team ya Arsenal ilitakiwa istruggle kupata ushindi dhidi ya Everton, kwamba itashinda ila kwa mbinde, ila hiyo ni first team ambayo kakosekana Magalhaes.
KAma mnahisi shida ni wapinzani wanapaki basi Arteta akalalamike kama Slot alivyolalamika kwamba watu wanampiga low blocks na long balls na yeye hajui cha kufanya wakishamfanyia hivyo.