Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Chama langu jana nimeshangaa sana.
Hivi ni kweli walikuwa PRE-SEASON au walienda HONEYMOON?
1.Saliba miguu imepoteza ushirikiano na mpira kabisa.
2.Zubimendi achukue video za partey ajifunze kitu, sijui ni game ya kwamza, pia ana uchaguzi mbovu wa sehemu ya kupasia.
3. Kiungo chetu jana kilikuwa exposed mnooo, zaidi ya mipira mi3 inatoka kwa bayindir bey mpaka kwa mido ya man u na anapokea mpira easy, ana turn kwwtu easy na anaachia pasi.
4. Kale ka odegaard kamezidisha ubishoo, kuna muda anachelewesha mpira ili tu afosi kupiga vipasi vyake vya kunyanyua, jana kuna mipira ya kuachia yeye anafosi kwenda nayo..
5. Gyokeres aambiwe arelax, akofosi na kucheza kwa presha atakuwa flop.

Jana tumeshinda ndio hivyo mpira sio ngumi kusema kuna point, ingekuwa hivyo jana ushindi haukuwa wetu, manunu fc walikuwa bora zaidi yetu karibia kila sehemu.

Ngoja tuone game zijazo ili tujue msimu huu ni kugombea top 4 ama top 6
 
Hongereni...arteta alikuwa vizuri na game ame win kikatili sana km Mourinho sometimes inatokea na kumbuka hii ni big matches.
Man united Huwa tunakuwa Bora na team zenye playing style kama yenu mfano man city anaweza akafa akija OT.
gyokeres awe anaanzia benchi ana pressure ya kuprove uwezo wako hasa record yake ya msimu uliopita ya G/A 67...awe makini hasa kocha ndio anapaswa kumuongoza na kumshusha pressure.

martin odergad muwe naye makini asiwacheleweshe kufika mnakotaka
 
Ø jana ni mchezaji bora kwa upande wetu, achilia mbali makosa machache aliyofanya, infact Ø wa jana ningependa kuona muendelezo ule, hali ya kujiamini na ku take risk imerudi kwake, good.
 
Naamini au tutoe kuamini, najua team yoyote inaweza kubeba EPL kasoro Arsenal tu. Arsenal hatakaa abebe ubingwa unalijua hilo ila umeamua kukaza fuvu ikifika May unaliachia fuvu lipoee 😂
Mtu wa chelsea unabishana nae nini sasa ww arsenal ?team ina world club cup 2 , uefa champion2 chelsea haijawahi kuwa league yenu, ww upo na sisi huku wote tuna zero 🏆
 
Mkuu linapokuja suala la Ulaya yaani UEFA Huwa nakaa kimya kwasababu huko Sina history nzuri ila hii ligi ya ndani tutaongea sana maana Kila pahala tumegusa kombe na sasahivi tunasakamana na watu pale juu...nyukesto mlijitahidi kukimbiakimbia hii miaka 2 kutaka kukaa pale juu na Hili ni kosa la Manunu ile nafasi mliyopo ilitakiwa awepo Manunu pale....sasa wakubwa wanakuja wananyofoa wachezaji hata wale wanaobeba timu....kaanza Isak next Gordon baadae Bruno....hii inaonesha ww BDO ni bwana mdgo sana....huna influence ya kutosha...kama kwa kutulia bwana mdgo
 
Ligi ya ndani unaongelea nini mkuu?? Jana nilikua nacheki ball lenu ila kabla ya match kulikua na mabishano asee ni ngumu sana kuitetea arsenal .
Ligi ya ndani utaongea nafasi ya 2 mkuu au utaongea mambo ya 2004 huku kweli? Nan atakuelewa kwa mfano zaidi sana ataona umechanganyikiwa , fabregas Kacheza mpaka saivi ni kocha habari utakayoongelea ni kabla ya fabregas kuanza mpira.
 
Haya yakina Isak tuache tutayamaliza wenyewe, ngoja atue kwanza wissa Au nkunku Then atauzwa tu.
Wachezaji kugoma hajaanza isak tu hata kwenu wapo waliogoma mpaka wakaongezea hela ili tu wasepe arsenal.
Sisi tunataka tu Liverpool waletee kitita cha maana kabisa 150 huko ndo asepe.
VIPI MWAKA HUU NDO PHASE YA MAKOMBE AU???😂
 
Unaambiwa Mikel Arteta kashinda mechi 8 kati ya 12 dhidi ya Nyumbu, hapo toa zile za kusare, unadhani watampenda wale mabwana? lazima tu wamchukie
Kwa akili hizi za mashabiki wa Arsenyau Tetea Kiwigi apewe tu Life Contract hapo Arsenyo.
Nilidhani Kiwigi miaka 12 ya uwepo wake hapo Arsenyani atatetewa walau kwa kubeba kombe hata moja la Epl au Europa, kumbe anatetewa na kushangiliwa kwa kumfunga Nyumbu mechi 8 kati ya 12 walizocheza?
Haya maneno ya Will Jr yamenifikirisha sana na kunifanya nikumbuke ile kauli ya marehemu Jomo Kenyata kwamba kule Arsenal Tetea Kiwigi anatawala Maiti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…