Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kepa kwangu is a perfect signing. Ameibeba Bournemouth pakubwa Kosa kubwa is to let Partey go. Tukimkosa Eze will beanother grave mistake.I still stand with Gyokeres
 
Mtazamo wako sio sahihi, kukosa pure striker sio tatizo, unaweza kutumia false 9 lakini je huyo F9 amezungukwa na wachezaji gani, i mean wide attackers, km real striker hauna that means you need killers outwide, case ya Mane, Firmino & Salah, Martinelli game yake inashuka day by day, Saka amekuwa injury kwa muda gani last season? kuna msimu tumepoteza ubingwa just for 5 points dhidi ya City bora iliyochukua treble, kuna msimu kipindi tunajitafuta we're on the title race mara pah injury ya Saliba, mara injury Partey sasa leo kocha akisajili watu km Mosquera kuongeza quality depth that means hata Saliba kaumia there will be replacement available na yenyewe inaleta kelele tena, washabiki wa Arsenal sijui huwa tuna shida gani! vitu vingine ni kuchanganua IQ yako kabla hujajenga hoja za kijinga.
 
Jamani kukosoa haimanishi utaonekana una hoja sana za kimpira, i wish hili jukwaa siku moja nione hoja positive tu kutoka kwa mashabiki wa Arsenal. Tusiwe kama layman bana. Mtu yupo humu miaka mingi ana experience lakini everyday negative thoughts! why bro?
 
Sikubaliani nawe kwa case ya Dec Rice, hakufeli isipokuwa ndiye mchezaji anayetupa output kubwa kwenye Lcm, hata pep alimprofile Dec kwenye role hii km replacement ya Guendogan, ukumbuke Rice alikuwa haendi kumuweka Rodri bench but to play lcm. he is still the best holding mid itw, Nadhani tungoje Euro mwakani hili tuone je Thomas Tuchel atamprofile Dec kwenye role ipi.

point ilikuwa ni kum-upgrade TP kwenye holding role lakini ikaonekana Dec anatupa optimal volume kwenye Lcm thats why tuka Move kwa Zubi.

Kingine Viera si replacement ya Xhaka, hii ni depth kwa Martin Odegaard, He is a no 10, he is RCM.
 
Kiukweli ndugu yangu watu wa aina yako ndio wanaosababisha Arsenal iwe hapa ilipo maana hata ujinga mtasifia tu.

Hao wachezaji wakusaidia wachezaji tegemeo kwanini wasisaidie hao unaosema wameumia.Kwanini sterling alishndwa kusaidia nafasi ya Saka na aliletwa na Arteta.

Soma hoja uelewe ndio ujibu,sio ujibu ili mradi uonekane umejibu.

Nikiiangalia Liverpool naona ni wachezaji watatu tu ambao wanawazidi wachezaji wa Arsenal iwe kiuwezo au juhudi binafsi uwanja.Wa kwanza Salah huyu kamzidi Saka uwezo anaetaka tubishane abishane peke yake.Wa pili Trent huyu alichotoa Liverpool kwa nafasi yake ni kikubwa sana kuliko beki zetu waliocheza nafasi ile.Wa3 ni McAllister huyu jamaa amejitolea sana kuisaidia Liverpool last season katika mechi nyingi.

Wengine waliobaki wameendana sana kiuwezo na wachezaji wa Arsenal.Kocha mwenye akili timamu hawezi kutegemea Kai ampe Epl,Uefa n.k.
 
Mazingira ya mpira yalivyo sio kila mchezaji ana uwezo sawa na yule mbadala wake, anachokupa peak Saka sio sawa na anachokupa Aging Sterling, lakini kwanini tunamsajili Sterling cuz tunaamini ana capacity ya ku balance the team's dynamics(not per 100%) if the other factors are constant( na hii ni case ya ku economize kwenye transfer market lengo likiwa to get the best out of a limited budget), but if the other factors( i.e injury to key players) are also depreciated, so dont expect to get the best out of him, na ndio unaona the introduction of Ethan Nwaneri as Saka's replacement, tatizo ni kwamba you have a Black & white thinking, your mind cant vibrate at this level of frequency. Im sorry to say this tho.
 
Umeandika na kiingereza mwenyewe ili uonekane unaujua kweli kweli mpira aisee.

Kabsa mtu na akili zake timamu anaweza kuunga mkono Sterling kuletwa Arsenal na aone ni sajili nzuri kwa kuisaidia timu kwa muda.

Sterling kacheza Liverpool,kaenda city pale Chelsea yenyewe kaenda akiwa anaonekana kabsa mchezaji kaisha na bdo wajinga wakakaa wakajadiliana wakaona anafaa.Tatizo hilo.

Kwanza ili uone Arsenal kuna ujinga mwingi ni kufikiria kusajili makapi ya Chelsea.Hili tu linaonesha hii timu ina watu wenye akili za namna gani.

Wanasajili wale wachezaji ambao Chelsea imewachoka wao wanawabeba.Hii yote inaonesha Chelsea ni timu kubwa kuliko Arsenal.
 
Depth kwa Odegaard? Sipo sure.

Notice kwamba hawa wawili washacheza wote kwenye baadhi ya mechi na Vieira akawa deployed LCM, sikumbuki competitive match ambayo Vieira aliwahi kucheza RCM.

Uko sahihi kwamba Rice anaoffer vingi LCM kuliko current squad tuliyonayo ila hajafikia alichotoa Xhaka misimu miwili kabla hajaondoka.

Martinelli anaonekana wa hovyo kwakua hachezi na Xhaka.
 
Wanasajili wale wachezaji ambao Chelsea imewachoka wao wanawabeba.Hii yote inaonesha Chelsea ni timu kubwa kuliko Arsenal.
Kuna kipindi Arsenal tulikua hatuwezi kuvutia wachezaji wenye vipaji/ wakubwa. Tulikua hatuwezi kuwavuta kwa uwanjani tulivyo au ambitions za timu na pia tuna ubahili ndani yetu hivyo hatukuwavuta kwa pesa pia.

Hii ikapelekea Arsenal tutegemee academy (Emile, Willock, Saka, Niles, Balogun, Nketiah), tutegemee vipaji vinavyochipukia/ potential (Saliba, Lokonga, Kiwior, Marquinhos, Nuno) au tuchukue wachezaji ambao ni experienced ila ndiyo ambao hawana game time kwa timu zingine (Cech, Cedric, William, Jorginho)

Tulishindwa kuwavuta wachezaji hawa kutokana na kutokua na ambitions au hapohapo hatukuweza kutumia pesa (Dusan, Aouar, Mudryk, Martinez)

Kuchukua wachezaji Chelsea haiwahalalishii wao kua timu kubwa. Bayern anachukua wachezaji Dortmund, haipiti misimu mitatu hajachukua mchezaji pale. Kuna mtu aliwahi kusema Chelsea ina wachezaji 60+ kutokana na alivyosajili hovyo so timu nyingi zitajikuta zinachukua wachezaji kutoka Chelsea.
 
arteta kafanya signings 3 (fábio vieira ,kai na merino ;wote ni left footers hao) za kuziba pengo la xhaka na zote hazijalipa ,alichokosea hapo ni kutaka kumtafuta messi mwingine duniani kitu ambacho ni kigumu.. kila mchezaji ana haiba yake tofauti na mwingine.

kumchezesha declan hapo ni imebidi tu iwe hivyo mana yeye kidg nd anajitahidi kuipa team balance wakati ina mpira na imepoteza mpira japo mimi namuona zaidi declan pale anapocheza partey ingawa pia namkubali zaidi partey.

now tunazungumzia kai na merino kuwachezesha kama F9 na bado hawatoshei vya kutosha kwenye hiyo role ,afadhali kidg ya merino anajua kuscore na kwenye link up play yuko vizuri.

ni wakati wa kuhoji uwezo wa kocha.. hususani kwenye chaguzi za wachezaji anaowasajili lbd kakosa washauri sahihi pia na pengine mbinu zake ndio zimefikia mwisho.. aje mwalimu mwengine.. aendeleze gurudumu mbele.
 
Kwamba mbinu mwisho siamini bado
 
Brentford wanagoma kuwauzia Nyumbu Mbeumo kwa 62.5M

Hiki ndiyo nilichomaanisha kwamba inabidi uwavute kwa pesa au ambitions zako. Nyumbu ambitions zake ni unknown kwa sasa so ni sawa kabisa anavyorely kwenye pesa.

Same na kenge alivyofika Roman mpaka leo kwa Todd
 
ishu ya eze imefikia wap mkuu?
 
Tatizo lipo kwa Brentford na sio mchezaji, maana mbeumo ameshaweka wazi kuwa anataka kuja man united.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…