Arsenal (The Gunners) | Special Thread

"Our floor is their ceiling" πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

 
Wazee wa kutukana mamba kabla hamjavuka mto Mkohoti na Labyrinth 84 leo naona mmoja wenu au wote wawili mkiingia Europa League.

Angalau Herzogg ana uhakika kidogo wa kuingia UCL.

Ila pia yote kwa yote, natambua kuwa mnapaswa kupongezwa maana nyie mmepanda kutoka msimu uliopita huku akina Herzogg na sisi tumeshuka msimu huu. Sisi kwa viwango vyetu, huu msimu umekuwa mbovu kwetu lakini nyie kwa viwango vyenu, hasa hawa mijusi milia, huu ni msimu wa mafanikio katika historia ya timu yenu. Hongereni.

Tukutane tena msimu ujao muendelee kuchangia points sita sita katika kampeni yetu ya kuchukua ubingwa na makombe tele.
 
By now ni sahihi kusema Arsenal women ina msimu bora kuliko timu zote za ligi ya Uingereza kwa ligi zote za wanaume na wanawake
Akili kubwa sana hii. Umetumia mantiki ile ile wanayotumia Manyumbu, kenge, kuku na mijusi wanayotumia kupima mafanikio, lakini hapa hawatakuelewa.
 
Matokeo ninayotamani ni villa ashinde halafu hao waliobaki wadrop point au wapigwe kabisa.

Milio itakayosikika hapo siyo poa
Acha roho mbaya mkuu, mbona wakati mnahangaika kutafuta team mtakayocheza nayo final kati ya Inter na barca tulihangaika wote kuwatafutia team nzuriii bila kujali kuwa mpo robo final πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Nyumbu hii game hana faida nayo. Atapelekewa moto hadi basi.

Kwamba Hakika Ruben amewaambia wachezaji yeye bado ni kocha wa nyumbu na amemwambia Garnacho atafute timu.

Kuna website ya kipuuzi inaitwa transferfeed, baada ya hii ripoti tu tayari wakamlink Garnacho na Arsenal. Nikasoma walichoandika, kwamba "Arsenal might be interested" hiki walichoandika ndiyo mfano wa ripoti za siku hizi yaani mtu akihisi tu mchezaji fulani anaondoka anamlink na Arsenal that's it.

Hii ilisababisha Tajiri Miluzi apotezwe kuwanunua wakina Nkunku na Madueke
 
Usitegemee msimamo kama utabadilika, ni hivyo hivyo kama ulivyo.
 
Na ukiwauliza hayo makombe yao wameyaona mangapi? Kuna wengine hata moja hawajaliona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…