Kwenye matukio ya kihistoria, kama hukuwepo ni vigumu kuelewa context.
Manyumbu na Spurs wamepambania Europa na Spurs akashinda. Kwenye ligi mpaka sasa Spurs ni wa 17 akiwa na GD ya 2 huku Manyumbu ni wa 16 na GD ya -12. Miaka 10 na zaidi baadae watu watasoma tu kuwa Spurs walikuwa mabingwa wa Europa 2025 na wanakombe la Ulaya. Hawatajua kuwa timu mbovu imebahatika kushinda kombe mwaka fulani. Hii inanikumbusha Greece walivyoshinda Euros za 2004.
Wanawake wa Arsenal on the other hand, wamepambana nyumbani na kushika nafasi ya 2 kwenye ligi. Walianza vibaya ila wakapindua meza na kupanda. Kwenye Champions League pia wamefika fainali kwa kusota haswa. Nakumbuka ile 5-2 tuliyochapwa na Bayern. Wamelazimika kupindua meza baada ya kupoteza mechi za kwanza na Juventus, Real Madrid na Lyon, zote timu kali sana na wakakutana na Barcelona, vinara wa soka la wanawake kwenye fainali na kushinda.
Historia itaonyesha Spurs na Arsenal Women wote ni washindi ila haitaonyesha kuwa Spurs walibahatisha na Arsenal huenda walistahili.
Anyways...
This is Arsenal. North London is Red.
Mpango wa kuirejesha Arsenal kileleni mwa ulimwengu wa soka kila idara kuanzia watoto, wanawake mpaka wanaume unaendelea vizuri.
Tumelia sana. Hivi punde tu tutafurahi.