Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Angeanza mwanzo wa msimu angebeba ile wsl nadhani
Nafikiri hivyo pia. Zile points alizopoteza Jonas Eidevall mwanzoni zilitugharimu. Lakini pia baada ya kuwachapa Madrid na Lyon tulipigwa kama game 2 mfululizo kizembe zembe. Pia nafikiri Chloe Kelly tunaye kwa mkopo tu kwa sasa. Alianzia Arsenal na sasa yuko Man City, ila nadhani tunapaswa kumrudisha nyumbani.
 
Waliobetia Arsenal wameula.
 
Kelly nadhani nafsi yake ipo Arsenal kuliko City walio m-dump
 
Kwenye matukio ya kihistoria, kama hukuwepo ni vigumu kuelewa context.

Manyumbu na Spurs wamepambania Europa na Spurs akashinda. Kwenye ligi mpaka sasa Spurs ni wa 17 akiwa na GD ya 2 huku Manyumbu ni wa 16 na GD ya -12. Miaka 10 na zaidi baadae watu watasoma tu kuwa Spurs walikuwa mabingwa wa Europa 2025 na wanakombe la Ulaya. Hawatajua kuwa timu mbovu imebahatika kushinda kombe mwaka fulani. Hii inanikumbusha Greece walivyoshinda Euros za 2004.

Wanawake wa Arsenal on the other hand, wamepambana nyumbani na kushika nafasi ya 2 kwenye ligi. Walianza vibaya ila wakapindua meza na kupanda. Kwenye Champions League pia wamefika fainali kwa kusota haswa. Nakumbuka ile 5-2 tuliyochapwa na Bayern. Wamelazimika kupindua meza baada ya kupoteza mechi za kwanza na Juventus, Real Madrid na Lyon, zote timu kali sana na wakakutana na Barcelona, vinara wa soka la wanawake kwenye fainali na kushinda.

Historia itaonyesha Spurs na Arsenal Women wote ni washindi ila haitaonyesha kuwa Spurs walibahatisha na Arsenal huenda walistahili.

Anyways...

This is Arsenal. North London is Red.

Mpango wa kuirejesha Arsenal kileleni mwa ulimwengu wa soka kila idara kuanzia watoto, wanawake mpaka wanaume unaendelea vizuri.

Tumelia sana. Hivi punde tu tutafurahi.
 
Baada ya kupewa habari za arsenyani akaamua kuachana na jezi πŸ˜‚

Your browser is not able to display this video.
 
I like Sheffield. I wish they should have made it to EPL but Sunderland had other plans
 
Pale London mwanaume ni mmoja tu Chelsea ni makosa sana kuilinganisha Chelsea na false hopers et kwasababu hopers wana makombe mengi miaka ya Giza huko 1952 πŸ˜‚πŸ˜‚ .
Naona huko juu kuna list ndefu ya comparison between Chelsea and false hopers daah nimehuzunika sana.

Team yenyewe UEFA LONDON nzima unafananisha na kituko assnall
 
For 30 years Chelsea
EPL :5
UEFA: 2 as champion 1 as runner up
FIFA CLUB WORLD CUP :1
EUROPA :2
The only team in London to win UEFA champions.

For 30 years FALSE HOPERS(ARSENAL)
EPL : 3
UEFA : 0
EUROPA 0
In short zero European / international trophy .
Ukianza ku punguza miaka 5 /10 utajua why false hopers ni genge la vichekesho.
Tottenham huyu hapa ni worse season kwa epl lakini ana EUROPA πŸ†.
Nyinyi katika peak ubingwa ni kumfunga Madrid and kumaliza nafasi ya 2πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Maelezo mengi (sugu voice) tuonyeshe kombe uliobeba mwaka huu au kukuonaa huruma miaka 5 nyuma .
Miaka 5 nyuma Chelsea Ana UEFA na league vipi kikundi chako kina nini???
Miaka 10 nyuma still Chelsea ana UEFA na ligi vipi wewe team yako ina nini??
 
Maelezo mengi (sugu voice) tuonyeshe kombe uliobeba mwaka huu au kukuonaa huruma miaka 5 nyuma .
Miaka 5 nyuma Chelsea Ana UEFA na league vipi kikundi chako kina nini???
Miaka 10 nyuma still Chelsea ana UEFA na ligi vipi wewe team yako ina nini??
Mtoto wa kambo umefika
 
Nilikua X nafikiri wiki 2 zimepita nikakuta page moja inafananisha msimu wa city na wa Arsenal ikaonyesha city na ubovu wake ina trophy ambayo ni community shield na inawania nafasi ya pili ya ligi.

Muda hii page inaandika hivi Arsenal tulikua tunaongozwa mbili bila na liver. Na netizens wakaipokea habari wakachambua ubovu wa msimu wa Arsenal na kuisifu city kwamba pamoja na msimu mbovu ila city ana kombe.

Baada ya game kuisha Arsenal akasuluhu kuna shabiki wa Arsenal akauliza kwanini Arsenal inasemwa haijashinda kombe kwa miaka mitano nyuma wakati kombe hilohilo kwa City litahesabiwa na Klopp aliagwa huku likitajwa. Na hata ilivyoonekana Arsenal anaweza kukosa nafasi ya 2 ikaonekana ni failing ila kwa city ni success?

Likaja jibu kwamba "Because our floor is their ceiling"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…