Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ingekuwa EPL, ile penalty tusingepewa. Merino aliangushwa na wala hakulala na kulalamika bali aliamka chap chap na kuanza kurudi kudefend. VAR wakamuita refa aangalie screen, tukapata penalty yetu halali.

Ingekuwa EPL, ile penalty aliyopewa Mbappe kwa kujiangusha isingefutwa. Rice asingepewa yellow card bali angepewa red card. Pia, VAR wasingeangalia kuwa Mbappe alikuwa offside. Penalty ingepigwa tu tupende tusipende.

Tusisahau kuwa tumeshadhulumiwa zaidi ya 10 points na marefa na VAR kwenye EPL na tungekuwa karibu zaidi ya Liverpool au juu yao kama isingekuwa kwa hizo dhulma zao hao wabaya wetu.
 

Ninavyoona mimi, kama Rice anakumbuka namna ya kuwa DM, ningependa Rice acheze nafasi ya Partey halafu Merino acheze LCM huku Ode akikaa RCM na Trossard awe CF kwa sababu tu hatuna striker mwingine na napendelea Merino na Rice washirikiane kuwazuia kina Vitinha kuliko Jorginho na Rice.

Katika kushambulia, kama Trossard akiitendea haki nafasi ya striker basi tutakuwa na matumaini.
 

Wote Waingereza. Au alitaka kutaja watatu tu na ikatokea tu kuwa ni Waingereza. Mimi nilifurahia zaidi kazi ya Timber na Kiwior kwa jana na hata ile mechi ya kwanza.

Ila Timber ni noma aisee. Nadhani hata kadi ya njano moja hakupata katika mechi hizi mbili na hapo mwamba kakutana na Vini Jr na Mbappe.
 
Unajustify uzembe wetu kwa vitu vidogo tu ni kweli EPL tulidhulumia baadhi ya mechi ila tumekosa ubigwa mwaka huu, sababu kubwa majeraha na kutosajili striker wa maana kule mbele tunahitaji Mshambuliaji wa maana na winger mwingine level za Saka hawa Martineli plus Trossard hawawezi kutupa ubigwa ikubukwe ligi ni marathon unatakiwa uwe fit September to May .
 
Hapana, lengo langu siyo kujustify ama kuficha madhaifu yetu bali kusema tu kwamba pamoja na madhaifu hayo, kama kikosi finyu, majeraha, viwango vya chini vya baadhi ya wachezaji, nk, nasema pia kuna uhuni mkubwa tu tulifanyiwa ambao umetuumiza kutoka kwa waamuzi. Ni kuonyesha tu utofauti wa viwango vya waamuzi Ulaya na Uingereza.
 
Pepe na Ramos nadhani walikua na addiction ya red cards wao hawakujali dakika wala mechi watakazokosa.
Kwa dakika mechi ilipofikia, aggregate na current score ya dakika zile ingekua dumb kutafuta red ambayo itafanya usicheze mechi tatu zijazo mkirudi CL.

Beki alikua sahihi kutofanya faulo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…