Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Mbape anajiona ana gundu sana, ameenda timu kubwa yenye mastaa wengi Kwa mbwembwe nyingi na ameishia kutolewa kwenye mashindano ila timu yake aliyotoka imesonga mbele kwenye hatua ya Semi final.

Luis Enrique ni bonge la kocha jinsi alivyoifanyia mabadiliko PSG kutoka kuwa timu ya Galacticos kuwa timu ya vijana wadogo wenye vipaji inathibitisha ubora wake.
 
Walete timu yao iliyo bora

Acha waendelee kupiga ramli mpaka mwisho wa msimu, mwisho wa siku wataanza kusema "mna bahati tu timu zote shiriki zilikuwa mbovu" hapo ni baada kazi kuwa imekamilika...!!
 
Wewe utakuwa pacha wangu wa nje! Haiwezekani mfanano huu!
Mimi ni YANGA, ARSENAL, FRANCE ( Kwa sababu ilikuwa na wachezaji wengi wa Arsenal plus Zidane)
 
Wewe utakuwa pacha wangu wa nje! Haiwezekani mfanano huu!
Mimi YANGA, ARSENAL, FRANCE ( Kwa sababu ilikuwa na wachezaji wengi wa Arsenal plus Zidane)
Mimi niliipenda France kwa sababu ya Wenger, kisha Henry and of course Zidane pia.

Nikufahamishe tu, Zidane ndiye mchezaji wangu bora wa muda wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…