Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ndugu yangu Labyrinth 84 naona kwa makusudi kabisa umeamua hawa Arsenyau wasifurahie pilau lao la sikukuu, yaani hiki unachowafanyia ni sawa na kusubiria kidonda kinaanza kukauka halafu unakisugua na msasa.
 
Hili halina msaada nyinyi kubeba EPL , mbona Jorginho ile 22 alipiga goli la ushindi vs Aston villa , kila siku cashmoney analalamika kuongezewa hela kwa jorginho😂😂
Ungesubiri kidogo mkuu ndiyo uhamie kwa mijusi milia. Sisi hapa tunasubiri makombe mawili watayonyang'anywa mama C115y wataposhushwa daraja. Halafu bado muda si mrefu tutachukua mengi tu ya kushinda kwa kuongoza ligi.
 
Ungesubiri kidogo mkuu ndiyo uhamie kwa mijusi milia. Sisi hapa tunasubiri makombe mawili watayonyang'anywa mama C115y wataposhushwa daraja. Halafu bado muda si mrefu tutachukua mengi tu ya kushinda kwa kuongoza ligi.
Hizi ndoto na false hope nilizikataa sasa nipo kwa geordie tunanyanyua makombe tu kule na hapo tunatafuta beki 1 world classic tupambanie EPL
 
Hizi ndoto na false hope nilizikataa sasa nipo kwa geordie tunanyanyua makombe tu kule na hapo tunatafuta beki 1 world classic tupambanie EPL
Mabeki world class wote tumewachukua sisi wamejazana pale Emirates. Tatizo letu ni striker tu na ndiyo hivyo kiangazi tunakuja hapo kumchukua Isak. Next season makombe yatakuwa mengi kwetu mpaka tutajenga ukumbi mkubwa tu wa kuyahifadhi.
 
Leo chama la wana lipo dimbani kutoa burudani ya soka safi na magoli ya video

Wale wa pira magimbi pira kande pira papatu papatu pira gombania goli (nyumbu, kenge n.k) mnakaribishwa
 
Mabeki world class wote tumewachukua sisi wamejazana pale Emirates. Tatizo letu ni striker tu na ndiyo hivyo kiangazi tunakuja hapo kumchukua Isak. Next season makombe yatakuwa mengi kwetu mpaka tutajenga ukumbi mkubwa tu wa kuyahifadhi.
Tatizo false hopers mnaamini sana halafu ni wepesi wa kusahau.
Umenikumbusha 2008 Gallas kakaa chini uwanjani haamini kama aliondoka chelsea akaja kwa team yenye false hope kiasi kile😂.
Game zilikua zimebaki sijui 10 mchukue ubingwa mara paap clichy huyo kafanya rafu tuta likawekwa hope za ubingwa zikageuka kuwa false hope.

Mpira ni burudani na furaha sadly ukiwa arsenal fan ni opposite kwa miaka 20 yote nyinyi ni huruma na simanzi always si kwa mashabiki , kocha hata wachezaji.
Hakuna story ya furaha kwa arsenal labda tu pale unapoitaja arsenal mbele ya mashabiki wa chelsea, man utd , man city , Liverpool lazima watacheka 😂😂😂
 
Berta amezungumza na camp ya Victor.

Mashabiki tumegawanyika kuna wanaoprefer Victor na wengine Isak but financially ni sahihi zaidi kudeal na Victor.

Argument wanayompinga Victor ni umri na kwamba alishafeli EPL. But De Bruyne na Salah walishafeli EPL kabla ya kurudi tena.

Upingaji kwa Isak ni price tag ambayo ni kama 130M. Ukitoa hii inabidi usisajili baadhi ya nafasi. Hata hivyo binafsi naona Isak atafanya vizuri zaidi Liverpool au United kuliko kwetu pia alishakosa mechi kadhaa kwaajili ya injury.

That being said I think ni bora tudeal na Victor.
 
Sijui Viktor na Isak wanaushindani gani kwenye timu ya taifa na sijui hata Swedden wanatumia mfumo gani, ila nafikiri Isak yuko mbele yake kwenye uchaguzi. Nafikiri akija Viktor atakuwa na usongo wa kupambana kwenye EPL na kuonyesha kuwa anaweza kumpiku Isak kama main striker wa Sweden.

Ngoja tuone lakini.
 
Victor is a total waste of money. Takataka nyingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…